Mimi nimeoa msabato, mimi ni mkatoliki. Ndoa tulifungia kanisani kwetu (katoliki), wakatoliki tuna utaratibu wanaita "ndoa mseto", kama mmoja wa wanandoa ni wakatoliki, mwingine sio, ndoa inafungwa ila kila mtu anaendelea na dini yake.
10 years down the line. If I were to go back in time, I would still choose her. Our two kids, wote wamekua wakatoliki. Dini tofauti haijakua kikwazo kwenye ndoa yetu au kutusababishia mikwaruzo/migongano.
Watoto wetu tuliwalelea katika misingi ya kumjua na kumuamini Yesu Kristu (tuna utaratibu wa kuomba kifamilia, kusoma biblia pamoja kifamilia, na pia watoto walivyokua wadogo, walikua wanaenda kanisani na mama yao kwa sababu mimi kazi yangu ilikua ya kusafiri sana, i was never at home-ila end of the day wote wameishia kuwa wakatoliki).
Sijui kama unaelewa mtifuano uliopo (kidini/kiimani) kati ya wakatoliki na wasabato. Kuna watabiri walitabiri kuwa hatutadumu, wanaendelea kusubiri hadi sasa, wanahesabu tu miaka, na wengine wametangulia mbele ya haki kabla ya kushuhudia walichotabiri.
Pia mkuu, kwani Mungu hayupo kwa mkuu wa wilaya? Mungu yupo kanisani tu? Si biblia inasema kuwa mamlaka yote yanatoka kwa Mungu? Na cheti mtakachopewa kwa mkuu wa wilaya ni kile kile ambacho aliefungia kanisani/msikitini anapewa pia. Kumkabidhi Mungu ndoa yako hauhitaji kuapa kanisani. It's you, and your God, in your heart.
Inawezekana ikiwa kinachowaongoza ni UPENDO.
Majighu2015