Kufuga mbwa

Kufuga mbwa

LEE VAN CLEEF

Member
Joined
Feb 28, 2013
Posts
29
Reaction score
5
Ndugu wana JF,

Naomba mwenye utaalamu anisaidie nataka kufuga mbwa mkali kama wa polisi, nitampata wapi, vyakula vyake ,matibabu yake nk. kwa ujumla jinsi ya kuweza kumiliki mbwa kama wa polisi.
 
Tafuta mbwa yoyote tu then tafuta Polisi wa Mbwa wamfundishe atakuwa mkali kama hao tu
 
Sema ulipo ili uambiwe uende wapi. Ukiandika, kabla hujapost soma ili uone kama swali lako likijibiwa utapata msaada sitahiki. Nikikuambia njoo hapa Namanyele kibaoni utaweza fika? Au umo kwenye kundi la wale wanaunda tume halafu ripoti ikiletwa hawakumbuka waliunda tume ya nini! Halafu ujue kuanzia leo kwamba si mbwa wote wa polisi ni wakali
 
Sema ulipo ili uambiwe uende wapi. Ukiandika, kabla hujapost soma ili uone kama swali lako likijibiwa utapata msaada sitahiki. Nikikuambia njoo hapa Namanyele kibaoni utaweza fika? Au umo kwenye kundi la wale wanaunda tume halafu ripoti ikiletwa hawakumbuka waliunda tume ya nini! Halafu ujue kuanzia leo kwamba si mbwa wote wa polisi ni wakali

Sawa mkuu nimekuelewa nipo Dar, na kuhusu kujua kama mbwa wote wa polisi si wakali ndo maana nimekuja humu jf ili nipate elimu.
 
Ndugu wana jf naomba mwenye utaalamu anisaidie nataka kufuga mbwa mkali kama wa polisi, nitampata wapi, vyakula vyake ,matibabu yake nk. kwa ujumla jinsi ya kuweza kumiliki mbwa kama wa polisi.

Mkuu, naomba nikuulize maswali yafuatayo:-

-Huyo mbwa kwa matumizi gani.
-Je eneo lako Lina hifadhi (uzio).
-Je Una mtu/watu watakae muhudumia.
-Uko tayari kumgharamia kimatunzo? (Chakula, usafi, tiba, mafunzo, upendo wa kuwa nae karibu Mara kwa Mara nk.)
-Unaishi wapi na eneo gani.
 
Ndugu yangu LEE VAN CLEEF usiumize sana kichwa !!
Kuna aina nyingi ya mbwa ila kama unahitaji mbwa kwa ajili ya ulinzi basi nakushauri tafuta hata hii mbegu ya kienyeji,awe ni dume ,kisha unamuhashi,kama hapo unapoishi kuna bucha jirani,ongea na mtu wa buchani kila siku awe anakukusanyia ile mifupa midogo midogo kisha unamchemshia, unachanganya na chakula cha dukani kinaitwa '' DOG SPECIAL DIETY''.
Baada ya miezi kadhaa utaniambia, ila kuna dondoo kadhaa za kumtunza mbwa ili awe mkali mfano
1. Mbwa anakula mara moja tu kwa siku,mfano mimi wa kwangu ni saa mbili usiku hadi saa mbili usiku, chakula na maji ya kutosha.
2.Mbwa mwiko kuona watu ovyo yaani anatakiwa kukaa kwenye banda mda wote isipokuwa usiku tu.
3.Zingatia sana dawa kama vile za minyoo,viroboto,kupe nk pia bila kusahau chanjo ya kichaa cha mbwa !!
NB,hizi njia ni kwa mujibu wangu mwenyewe wajuzi fungukeni zaidi tuelimishane !!

NWP_130413_0020.jpg
 
Mkuu, naomba nikuulize maswali yafuatayo:-

-Huyo mbwa kwa matumizi gani.
-Je eneo lako Lina hifadhi (uzio).
-Je Una mtu/watu watakae muhudumia.
-Uko tayari kumgharamia kimatunzo? (Chakula, usafi, tiba, mafunzo, upendo wa kuwa nae karibu Mara kwa Mara nk.)
-Unaishi wapi na eneo gani.
Mkuu Zinj mbwa namtaka kwa matumizi ya kawaida ulinzi wa nyumbani,uzio upo, mtu wa kumhudumia yupo, matunzo hayana tabu, na ninaishi Dar Ubungo.
 
  1. Kama unataka mbwa kama wa polisi nenda Kilwa road polisi kuna kikosi cha mbwa na farasi, unaweka order kulingana na unavyotaka (umri wa mbwa, mafunzo, jinsia etc) then watakwambia ni lini mbwa atapatikana
  2. Unaweza kupata wa aina hiyo kutoka kwenye vituo au madaktari wa wanyama (Victoria karibu na Knight support kuna vetenary technician pale ana kituo au Temeke Vetenary karibu na Wizara ya mifugo)
  3. SUA zamani walikuwa wanadhalisha mbwa – sijui siku hizi
 
Mkuu wana JF wengi wanapenda ku escalate mambo,mbwa wa polisi si issue kivile kumpata ukiwa dar,anapatikana,ila tatizo ni bei zake,Germany sherpher pure pupy ana range kuanzia laki 3 hadi laki 5,hapo unaongelea mbwa wa miezi mitatu tuu,ukitaka chini ya hapo unaweza kuingizwa mjini kwa kuuziwa brand ya Iringa,ipo like GSP lakini ni feki.

Mimi ni mfugaji mzuri wa mbwa,ninao GSP watatu,ila bado hawajaaliwa kuzaa,mwana JF mwenzangu ningekuzawadia kitoto bure!nisingechukua hata senti tano kutoka kwako.

Kwa hiyo kama upo serious na hela unayo,ni PM ili nimtafuta askari mmoja hivi yupo hapo Kurasini kwenye kikosi cha mbwa na farasi ndani ya week moja kitoto kitakua kimepatakana.Ila tafadhali usianze kuzingua manake kuna jamaa nilimuunganisha na huyo afande mara akaanza kumkimbia,sie wengine hatupendagi usanii.

Kila la heri na ufugaji mkuu.
 
Wasiliana na Kambaku ndio kazi inayo mweka mjini
 
Last edited by a moderator:
Kwanza, mbwa wa Polisi sio wakali, bali wanafuata command toka kwa Boss wao kwa hiyo kama unapanga kufuga mbwa hutatakiwa kuwa na mbwa kama wa polisi kwa sababu huna plan za kumtumia kukamata mtu au kukamata madawa bali unamfundisha kulinda nyumba yako, simply mbwa anayekufaa ni kama hao unaowaona nao polisi German Shephered au Bull bull, au hata rotweiller unamfundisha wewe unachotaka afanye, inatumia muda na energy nyingi mpaka kumfundisha mbwa aweze kufanya unachotaka, kwa hiyo lazima ujipange na kuwa na eneo la kutosha, nafasi, na vifaa vya kumfundishia kama guards nk. Kwa vyakula vinapayikana kirahisi kwa wanaoandaa vyakula vya mifugo, ila cha muhimu ni usiruhusu mbwa wako achanganyikane na mbwa wa mitaani. Ninafuga GSP na aina nyingine lakini kwa matumizi binafsi na nawapenda mbwa, kila la kheri na mafanikio
 
Wasiliana na Kambaku ndio kazi inayo mweka mjini

Nishaacha siku hizi, kwa sasa najishughulisha na biashara ya vileo vikali, kama unahitaji sema. Nina import TAKENGO kuja Dar es salaam na ndio sorely distributor!
 
Kupata taarifa za mbwa we google tu hao wote wanakupa taarifa hafifu sana, kwa mfano mtu anakwambia mbwa anakula mara moja tu kwa siku. Mbwa mkubwa ndio anakula mara moja lakini puppy wanakula zaidi ya mara 1 kutegemea na umri wake. Polisi nao hawana mbwa wazuri watakuongopea tu kuwa huyu german shepherd kumbe siyo eti kwasababu tu masikio yamesimama. Kunataarifa nyingi unatakiwa kupata toka umri na aina ya mbwa kwa matumizi unayotaka. Kwa ushauri zaidi nenda vet care oysterbay au victoria kwa dr. Kowero.
 
Tafuta mbwa yoyote tu then tafuta Polisi wa Mbwa wamfundishe atakuwa mkali kama hao tu

Ina maana mbwa atakuwa mkali kama hao PILISI WA MBWA au kama mbwa wa polisi??? Maana kama atakuwa kama hao POLISI nina wasiwasi na UAMINIFU wao baadaye kazini kwa mfugaji
 
Mkuu Zinj mbwa namtaka kwa matumizi ya kawaida ulinzi wa nyumbani,uzio upo, mtu wa kumhudumia yupo, matunzo hayana tabu, na ninaishi Dar Ubungo.

LEE VAN CLEEF
Kulingana na mahitaji yako nakushauri upate mbwa aina ya German Shepard au kwa jina lingine ni Alsecian. Mbwa wa aina hii wana tabia zifuatavyo:-
•Utii
•Wanafundishika
•Wanaupendo
•Wana resistance kubwa ya magonjwa ya tropiki.

Aidha, nenda kwenye vet clinic mkabala na O'bay Police Kwa Dr. Sinare huwa wanapatikana, hata ukipata cross breed sio mbaya.

Tahadhari, usichukuwe mbwa aina ya Rotweiler, Mkuu Mbwa huyu noma!! hatabiriki,very aggressive,hata wewe saa zote uwe makini. Kwa mafunzo wasiliana na mkuu sithole.
 
Nishaacha siku hizi, kwa sasa najishughulisha na biashara ya vileo vikali, kama unahitaji sema. Nina import TAKENGO kuja Dar es salaam na ndio sorely distributor!

Hahahaha, umeimiss sana takengo, eti? Ngoja nifanye mpango nikutumie kidogo wangu. ila huko kwenu uchange tankengo na jina ya kijiji chenu si balaa? Hahaha
 
Back
Top Bottom