Kufilisika a.k.a kufulia......

Tatizo hapa ni uwezo gani ulionao!! Mtu anakuja kuomba msaada haangalii hali uliyo nayo. Kama kusaidia is what makes you happy, help your relatives hata kama kiasi ulicho nacho ni kidogo. Kwa hiyo, kusaidia mtu ni relative term, it is not a fixed parameter. Utamsaidia mtu kiasi hicho, lakini hakitamkomboa.

Kusaidia kivipi?

Kama unasaidia ili jamaa yako aweze kujitegemea baadae ni vizuri,lakini kama unasaidia ili watu wakusifu tu mitaani huku wewe ukiteketea na nduguyo unaye msaidia anadumaa ni uzembe.

Fundisha mtu kuvua samaki, mpe nyavu, kisha mpige ban asikanyage kwako tena kuomba omba. Huo ndio msaada, kinyume na hivyo ule mzunguko wa ulofa unaongezeka ktk jamii yako.
 
Wakuu mara nyingi hili jambo huwakuta watu wengi. Kuna wanaodai mali ya dhuluma lazima ije kupotea kabisa japo wapo wenye kupata mali kihalali na wanafilisika. Mimi nimemshuhudia jirani yetu ambaye alikuwa na pesa nyingi sana miaka ya 90, wakati huo alikuwa akifanya biashara za Zambia. Yule jirani alikuja kufilisika kabisa..na hakuweza kurudia hali ya mwanzo mpaka sasa. Je wewe umekutana na watu wa aina hiyo/umewahi filisika? Je sababu hasa huwa ni nini? Inawezekana mali ya halali na uliyotafuta mwenyewe, ikaisha na ukashindwa kunywa hata chai? Tukienda kwa mifano naamini tutajifunza mengi, hasa kwa tunaoyaanza maisha. NB: Masikini huwa hafulii

Kwangu mimi kufilisika kupo but sio lazima ufulie na kushindwa kunywa chai. Matajiri wakubwa, huko ughaibuni na hata hapa Tanzania wanatumia kufilisika "bankrupt" kama stratergy ya kukwepa madeni wanayodaiwa.Kwa mfano kampuni ya Scandinavia Express ilipooona inashindwa kulipa madeni baada ya kila mtu kuchukua chake ikadeclare "bankrupt" na hivyo kuingia unnder receivership. Nini kilitokea??

Jamaa (shareholders) wapo osterbay wanakula kuku kwa mrija, na kampuni mpya "GREEN STAR" inaoperate kama kawaida(wanasema ya mdogo mtu) .The same wine but different bottle. Na huu ndio uzuri wa kuincorporate a Limited Liability Company, kwani kisheria mali za kampuni ni tofauti za washikadau wake mmoja mmoja. Sasa hapo looser ni nani? Bank au Scandnavia?. Hivi umewahi kujiuliza ni kwa nini wahindi wanabadilisha majina sana? WAKE UP PEOPLE

Poor Tanzanians, wengi bado tunapambana na sole propriatorships & firms. Wakati hali ibiashara ikibadilika hata pa kulala utakosa kwa sababu ya kufidia madeni, na hata ukisema umefilisika bado asset zako binafsi zitafidia madeni (lets join this conspiracy of the rich). Halafu hawa matajiri huwa very smart. Wanatenganisha kila kitu kwa kuoutsource, kwa mfano ownership ya Yard, na baadhi ya operation kama Cargo Transportation zilikuwa outsourced kwenye kampuni nyingine (wanazomiliki wao wenyewe) mwisho wa siku wakisema wamefilisika hizo operation wanabaki wakizimiliki kwani hazikuwa sehemu ya Kampuni husika.

Hii stratery ipo kisheria, na wajanja wanaitumia kwa faida yao. Usihadaike kumuona Mtu alikuwa na hela nyingi na ghafla akasema amefilisika, just wait for his the greatest comeback. Ingawa wenzangu na mimi wakesema wamefilisika ndio for good kwa namna wanavyokuwa wamestructure biashara zao lazima wapoteze kila kitu

Tuamke watanzania, tutumie sheria zetu kwa faida yetu
 
Mkuu,suala la kufilisika linategemea sana na muundo na historia ya jamii.Ukiangalia jamii za wenzetu ,nikimaanisha wenzetu wa Asia,bara arabuni,america na ulaya zipo koo ambazo zimekuwa consistently tajiri kwa vizazi vingi hata zaidi ya vitano (old money).Jamii hizi zimejijengea uwezo mkubwa wa:
1.-kuheshimu utajiri
2.kuweka akiba
3.kutokutumia zaidi ya kipato chao,hata kiwe kikubwa vipi.
hizi tabia wamezipandikiza kizazi hadi kizazi.
Turudi kwa wabongo:
wenzetu wahindi na waarab wamekuwa wafanyibiashara miaka mingi na Nyerere aliwapa fursa ya kuendelea na utaratibu wao,na mpaka leo wako bomba,wakiishi Upanga na kushea apartment tunawacheka kumbe ndo kutengeneza savings,nywele ngumu tuliambiwa na Mwalimu kuwa 'ubepari ni unyama' tukakubali tukaishia aidha kuishi kwa mshahara au kuwa wakulima.
Ogopa limbukeni anayeibuka ghafla,Mzee Mwinyi ndo alitufungulia milango ya kushika hela,kwa ushamba wetu ndo maana yanatokea hayo uliyosema hapo juu.
Mkuu it is only a matter of time na sisi nywele ngumu tutajifunza namna ya kuheshimu na kutunza hela,haya mambo ya kupata hela kila mwanamke Dar ukamnunulia rav4 tutaacha.

Ha haa haaaa nice one.
 
Mimi niko tofauti kidogo! Angalia umepigana toka chini hadi umefika juu. Hapo ndo unakuta kila ndugu anakuja kuomba msaada na hizi tabia zetu za kuoneana aibu! basi unaanza kusaidia kila kichwa. Kwa nini usifilike? Kwa hiyo extended family, tamaduni zetu, namna ambavyo tusivyojua kuongeza faida kutokana na mikubwa tunayokuwa nayo ni matatizo makubwa yanayowakumba watu ambayo hupelekea kufilisika.
Ahsante kwa maada nzuri.

Ni kweli rafiki yangu nakubaliana na wewe inatokea tu huruma na utu inabidi kusaidiana,lakini kwa upande mwingine rafiki yangu hawa wenzetu waasia wao nao wanatabia ya kubebana kwa mfano kuna koo kama wakina sijui Gulam,dewji na wengine wengi unakuta ukoo mzima matajiri kwa hiyo hata mtu wa kusaidia ndani ya ndugu zao hamana.
Hawa jamaa wana style wanayotumia ambayo ni nzuri sana naona wachaga wameanza kuitumia kidogo kidogo lakini hawatafanikiwa kwa kiwango kikubwa nitaelezea hapa chini kwa nini.Style yenyewe ni ya kuwezeshana kibiashara.
Natoa mfano umeenda kwenye duka la mhindi unataka shati au suruali akiona inalipa na kama hana atapiga pass kwa ndugu yake kama ndugu yake hana atapiga pass kwa jamaa yake wa asili hiyohiyo ya kiasia.Style hii ni nzuri sana ambayo wachaga wameanza itumia na inawapeleka mbele.

Kitu kingine ambacho ni kikubwa hawa waasia wamefanikiwa sana kujijengea uaminifu,kwa kweli sio uongo kwa hawa wenzetu waasia ukimpa mzigo akuuzie akikuambia baada ya wiki mbili uje chukua hela kama ukienda utapata hela yako kama hamna hela atakurudishia mzigo wako huo ni mfano,hii uaminifu imewapa umaarufu sana wahindi vigogo wengi biashara zao wakakimbilia kuingia share nao hii ndio imewachangia kuwaweka stable.Hapo tofauti na wenzetu wachaga uaminifu hamna ndio maana nikasema hawa jamaa hawatafika mbali kufilisika kutakua kama kawa.
 
Kusaidia kivipi?

Kama unasaidia ili jamaa yako aweze kujitegemea baadae ni vizuri,lakini kama unasaidia ili watu wakusifu tu mitaani huku wewe ukiteketea na nduguyo unaye msaidia anadumaa ni uzembe.

Fundisha mtu kuvua samaki, mpe nyavu, kisha mpige ban asikanyage kwako tena kuomba omba. Huo ndio msaada, kinyume na hivyo ule mzunguko wa ulofa unaongezeka ktk jamii yako.

Na hicho ndicho huwa nafanya!! Lakini mtu mwingine anamsaidia mtu mlo wa siku 7, ukiisha anarudi tena!! hiyo haisaidii.
 
Back
Top Bottom