Kufikiri kwa usahihi na kufikiri ili kutoa maoni

Gelion Kayombo

Senior Member
Feb 17, 2018
149
193
Kuna tofauti kubwa kati ya kufikiri kwa usahihi (Accurate Thinking), na kufikiri ili kutoa maoni( Critical Thinking). Tofauti na maana za maneno haya ni kubwa. Na hii imekuwa inawachanganya watu wengi kutofautisha maana za maneno haya, hali inayopelekea watu wengi kushindwa kuelewa kufikiri kwa usahihi ni nini na kufikiri ili kutoa maoni ni nini.

Watu wengi hawafikiri kwa usahihi, bali wanafikiri ili kutoa maoni. Hapa nitaeleza kwa ufupi tofauti ya maneno haya mawili yanayochanganya watu wengi.

Kufikiri kwa usahihi, ni pale unapokaa peke yako au na watu wengine na unajiuliza/ mnajiuliza maswali ya kina na kutafuta majibu ya maswali hayo. Maswali hayo unaweza kujiuliza wewe mwenyewe au unawauliza watu wengine wakupe majibu ya maswali yako. Maswali kama kwanini tatizo fulani linatokea mara nyingi, na kutafuta, na kupata majibu ya swali hilo hiyo ni kufikiri kwa usahihi. Na kuna kundi dogo la watu wanaojiingiza kwenye kazi hii: kazi ya kufikiri kwa usahihi. Henry Ford alipata kusema " kufikiri ni kazi ngumu sana, na ndio sababu, watu wachache sana wanajishughulisha nayo"

Kufikiri ili kutoa maoni, (Critical Thinking), ni pale ambapo mtu au watu wanachukua jambo lililozungumzwa na mtu au watu na kulichambua na kutoa maoni yao. Hii inafanywa kwa kulichambua tatizo au maelezo yaliyotolewa na mtu au kundi fulani la watu na kuchambua mazungumzo au tatizo hilo ili kutoa maoni binafsi au maoni ya watu wengi waliochambua. Wanatoa maoni yao na mtazamo wao juu ya mazungumzo aliyofanya mtu fulani, au watu fulani. Tofauti na kufikiri kwa usahihi(accurate thinking), hapa watu wengi wanaingia kwenye kundi hili.

Asante kwa kusoma, andiko hili. Pia karibu kwa maoni, na utoe uelewa wako juu ya kufikiri kwa usahihi na kufikiri ili kutoa maoni.

#Gelion Kayombo
 
Kuna tofauti kubwa kati ya kufikiri kwa usahihi (Accurate Thinking), na kufikiri ili kutoa maoni( Critical Thinking). Tofauti na maana za maneno haya ni kubwa. Na hii imekuwa inawachanganya watu wengi kutofautisha maana za maneno haya, hali inayopelekea watu wengi kushindwa kuelewa kufikiri kwa usahihi ni nini na kufikiri ili kutoa maoni ni nini.Watu wengi hawafikiri kwa usahihi, bali wanafikiri ili kutoa maoni. Hapa nitaeleza kwa ufupi tofauti ya maneno haya mawili yanayochanganya watu wengi.

Kufikiri kwa usahihi, ni pale unapokaa peke yako au na watu wengine na unajiuliza/ mnajiuliza maswali ya kina na kutafuta majibu ya maswali hayo. Maswali hayo unaweza kujiuliza wewe mwenyewe au unawauliza watu wengine wakupe majibu ya maswali yako. Maswali kama kwanini tatizo fulani linatokea mara nyingi, na kutafuta, na kupata majibu ya swali hilo hiyo ni kufikiri kwa usahihi. Na kuna kundi dogo la watu wanaojiingiza kwenye kazi hii: kazi ya kufikiri kwa usahihi. Henry Ford alipata kusema " kufikiri ni kazi ngumu sana, na ndio sababu, watu wachache sana wanajishughulisha nayo"

Kufikiri ili kutoa maoni, (Critical Thinking), ni pale ambapo mtu au watu wanachukua jambo lililozungumzwa na mtu au watu na kulichambua na kutoa maoni yao. Hii inafanywa kwa kulichambua tatizo au maelezo yaliyotolewa na mtu au kundi fulani la watu na kuchambua mazungumzo au tatizo hilo ili kutoa maoni binafsi au maoni ya watu wengi waliochambua. Wanatoa maoni yao na mtazamo wao juu ya mazungumzo aliyofanya mtu fulani, au watu fulani. Tofauti na kufikiri kwa usahihi(accurate thinking), hapa watu wengi wanaingia kwenye kundi hili.

Asante kwa kusoma, andiko hili. Pia karibu kwa maoni, na utoe uelewa wako juu ya kufikiri kwa usahihi na kufikiri ili kutoa maoni.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom