Jaji Mfawidhi
JF-Expert Member
- Feb 20, 2016
- 14,047
- 20,412
Miaka 70 kuanzia leo yaani 2110. Sisi Sote tutakuwa makaburini
pamoja na jamaa
zetu na marafiki zetu
. Watu tusiowajua wataishi katika majumba
na maeneo yetu.
MALI
zetu zooote zitamilikiwa na watu tusiowajua. Watu hao wala hawatotukumbuka. Hivi ni wangapi kati yetu wanaowakumbuka mababu wa mababu zao?.
Majumba yetu ya Goba na Masaki yatakuwa yanamilikiwa na watu wengine kabisa; Drea house yako uliyozika ndugu yako ili mtu asiuze hilo kaburi litahamishiwa Kimbiji na nyumba itavunjwa kufanuywa night club.
Majumba yetu huku Masaki yatakuwa yamemezwa na bahari kutokana na uharibifu wa mazingira huku maenep ya magomeni na manzese ndio itakuwa beach
Tutabaki kuwa historia
kwa vizazi vyetu na wakati huo huo watu watatusahau hata majina yetu na maumbile yetu.
Wakati huo tutakuja kugundua jinsi tulivyokuwa wajinga
na jinsi tulivyojidanganya kutaka kupata kila kitu kwa njia yeyote
.
Tutaomba angalau tupewe uhai
kwa muda mfupi ili tutubie ikiwa ni pamoja na kutoa sadaka
lakini itakuwa haiwezekani.
Zingatia kuwa, Leo tuna nafasi kutenda wema kwa ajili ya faida yetu wenyewe na wengine. Kitu pekee kitakachobaki milele ni matendo yetu mema katika Dunia hii na maisha baada ya kifo. Muda bado tunao. Fanya matendo mema kabla hujachelewa sana
*Mungu atusaidie katika hili.
Tunamuomba Mwenyezi Mungu atuwezeshe kutenda wema na kupata mwisho mwema.
--
MALI
Majumba yetu ya Goba na Masaki yatakuwa yanamilikiwa na watu wengine kabisa; Drea house yako uliyozika ndugu yako ili mtu asiuze hilo kaburi litahamishiwa Kimbiji na nyumba itavunjwa kufanuywa night club.
Majumba yetu huku Masaki yatakuwa yamemezwa na bahari kutokana na uharibifu wa mazingira huku maenep ya magomeni na manzese ndio itakuwa beach
Tutabaki kuwa historia
Wakati huo tutakuja kugundua jinsi tulivyokuwa wajinga
Tutaomba angalau tupewe uhai
Zingatia kuwa, Leo tuna nafasi kutenda wema kwa ajili ya faida yetu wenyewe na wengine. Kitu pekee kitakachobaki milele ni matendo yetu mema katika Dunia hii na maisha baada ya kifo. Muda bado tunao. Fanya matendo mema kabla hujachelewa sana
*Mungu atusaidie katika hili.
Tunamuomba Mwenyezi Mungu atuwezeshe kutenda wema na kupata mwisho mwema.
--