Pulchra Animo
Platinum Member
- Jun 16, 2016
- 8,439
- 14,762
Wakuu zipo sababu kibao ambazo tukizitaja zinaweza kuwa mwiba mchungu sana lakini itabidi tuzitaje ili kuuboresha mji wa Dodoma ambao umepewa hadhi ya jiji ikiwa kimuonekano baado sana
1. Geografia ya mji wa Dodoma
Mkoa huu ni miongoni mwa mikoa mikame na yenye asili ya jangwa kwa maana hauna mvua za kutosha ikiwa wastani wa mvua zake ni miezi mitatu au minne kasoro. Hivyo uoto wa asili muda wote ni ukame. Najiuliza sana serikali yetu imetenga bajeti kuwekeza katika eneo lenye ukame na kulifanya liwe la kuvutia au wamekurupuka tu.
Tukiangalia miji ya Dubai, Misri yenye hali kama hii ya ukame wametumia gharama kubwa kufanya miji ipendeze.pia ukiacha ukame kuna bonde la ufa limepita pale ambalo kitaalamu linakufanya usijenge majengo marefu kwenda juu.
2. Mzunguko wa pesa
Kwa sasa mkoa huu umekuwa na mzunguko wa pesa kwakuwa kuna uuzwaji mkubwa wa viwanja lakini baada ya hapo sidhani kama kutakuja kuwa na mzunguko wa pesa. Pia uwekezaji unaofanyika hauendani na ungezeko la watu.
Yaani unajenga majengo ya gharama mbali na miji ya watu halafu watu waje wajae kama maji ya bahari ni kitu kigumu sana.
Hii itatokea kwa miaka ya mbele kama 40 au zaidi. Kinachofanyika sasa ni kuharibu pesa za walipa kodi ambazo kurudi kwake itatugharimu miaka mingi.
3. Ni mji wa kisiasa (Makao makuu ya CCM)
Kwa mitazamo ya kawaida tunajua huu mji Nyerere na serikali waliufanya uwe makao makuu ya Chama cha Mapinduzi. Kimsingi sio wazo baya ila Nyerere mwenyewe alishtuka kuufanya katika kuufanyia maendeleo kwa kuwa kisiasa watu watajitambua na CCM itapoteza taswira. Serikali hii imevunja kanuni ya huu mji haukutakiwa kuendelezwa ili CCM itawale.
Yapo mengi ya kuelezea kwangu mimi. Wadau kama mnayo kuhusiana na mji huu mnaweza kutiririka.
Mkuu huu mji ni balaa..lakini wamagharibi na wivu wao hawataki kabisa ulimwengu waujue.Brasilia
Ndiko ninakoishi ila sijawahi kuona tatizo lolote kwa hawa wenyeji wangu.Hahaha! Nenda kaishi Dodoma
Dar haiwezi potea katika historia ya nchi hii.....yaani utabaki ni mji mkuu usiotambulika...Dodoma ni makao makuu ya CCM tuBwana we DSM ndio ishapotea hivyo watu watamiminika Dodoma yaani kufikia 2025 mji uta"double" kama sio ku"triple" kabisa
Mkuu umeongea point sana kwakweli TUACHE KUKURUPUKA KISIASA TUWEKE MIPANGO YA MUDA MREFU TENA TUKIWA NA SABABU ZA KIUCHUMI
View attachment 1272671
Huu ni mji wa dubai uwekezaji wake na muda waliotumia si sawa na serikali kuingia madarakani na kuanza kuwekeza katika kipindi cha miaka mitatu tu dodoma imekua jiji na unataka kushindana kimapato na majiji mengi ni kudanganya tu wakuu ina hitaji muda na fedha za kutosha kuwekeza na sio siasa za majukwaani
Usalama wa nn mkuu dunia ya leo ni utandawazi ina maana mji ukiwa kando ya bahari sio salama nikuafahamishe tu dodoma ilianza kuwa makao makuu toka 1973 mpaka sasa hakuna cha maana zaidi ya siasa uchwara tuPumba tupu hujui kujenga hoja watu walifocus usalama zaidi afu watu wa Dar ni tabu tupu ukiwa Dar ni full foleni full stress makazi duni joto Kali shida tupu
Makao makuu ya miji kibao mkuu imechangamka sana sisi miaka yote tulikuwa wapi na kwann ijengwe kwa haraka haraka kwa miaka mitatu ya ujenzi tu haitaifanya ichangamkeSisi tuliosoma zamani vitabu vyetu vya Geographia ilikuwa mkiichambua nchi mnaangalia mji wa makao makuu ya serikali na mji mkuu wa biashara
Dodoma ni mji mkuu wa serikali yani kutakuwa kunapatikana Ikulu ,mawizara na maofisi mengine muhimu ya serikali
Dar es salaam ni jiji la biashara kuna bandari kuu na international airport
Na makampuni kibao
Sasa nyi vijana sijui mnafeli wapi mnataka mji wa makao makuu ya serikali uwe sawa na mji mkuu wa biashara yani ina maana hamjui tofauti na tabia za miji ya aina hii kweli kiwango cha elimu Tanzania kimeshuka
Mwanza nako kubaya tu watu wamejenga juu ya mawe daahWangeamiaga Mwanza tu...
Hadi makao makuu yapo mlimani kwanMwanza nako kubaya tu watu wamejenga juu ya mawe daah
Dar es salaam ilipewa majukumu yote kama makao makuu ya serikali pia ni kama jiji la biashara lakini sasa Dar imesha jaa sana hivyo hakuna namna lazima serikali irudi DodomaMakao makuu ya miji kibao mkuu imechangamka sana sisi miaka yote tulikuwa wapi na kwann ijengwe kwa haraka haraka kwa miaka mitatu ya ujenzi tu haitaifanya ichangamke
Mkuu unajua sababu ya kupeleka makao makuu Dodoma?MARA MIA MJI UNGEJENGWA MOROGORO KWA KUIKATA KATIKATI UKATENGENGWA MKOA MMOJA UKAITWA MAKAO MAKUU
KWASABABU NI KARIBU NA DAR ES SALAAM
JAMAA ITAKUWA NI MTUMISHI WA UMMA HUYU,WATUMISHI WA UMA SIJUI WAMEINGILIWA NA MDUDU GANI VICHWANI MWAO YANI UWEZO WA KUFIKIRI NA KUCHANGANUA MAMBO UMEKUWA TATIZO KWAO,NA NDIO MAANA AWAMU HII HAWANA NAFASI KABISAMWALISHAONEKANA NI MZIGOWakuu zipo sababu kibao ambazo tukizitaja zinaweza kuwa mwiba mchungu sana lakini itabidi tuzitaje ili kuuboresha mji wa Dodoma ambao umepewa hadhi ya jiji ikiwa kimuonekano baado sana
1. Geografia ya mji wa Dodoma
Mkoa huu ni miongoni mwa mikoa mikame na yenye asili ya jangwa kwa maana hauna mvua za kutosha ikiwa wastani wa mvua zake ni miezi mitatu au minne kasoro. Hivyo uoto wa asili muda wote ni ukame. Najiuliza sana serikali yetu imetenga bajeti kuwekeza katika eneo lenye ukame na kulifanya liwe la kuvutia au wamekurupuka tu.
Tukiangalia miji ya Dubai, Misri yenye hali kama hii ya ukame wametumia gharama kubwa kufanya miji ipendeze.pia ukiacha ukame kuna bonde la ufa limepita pale ambalo kitaalamu linakufanya usijenge majengo marefu kwenda juu.
2. Mzunguko wa pesa
Kwa sasa mkoa huu umekuwa na mzunguko wa pesa kwakuwa kuna uuzwaji mkubwa wa viwanja lakini baada ya hapo sidhani kama kutakuja kuwa na mzunguko wa pesa. Pia uwekezaji unaofanyika hauendani na ungezeko la watu.
Yaani unajenga majengo ya gharama mbali na miji ya watu halafu watu waje wajae kama maji ya bahari ni kitu kigumu sana.
Hii itatokea kwa miaka ya mbele kama 40 au zaidi. Kinachofanyika sasa ni kuharibu pesa za walipa kodi ambazo kurudi kwake itatugharimu miaka mingi.
3. Ni mji wa kisiasa (Makao makuu ya CCM)
Kwa mitazamo ya kawaida tunajua huu mji Nyerere na serikali waliufanya uwe makao makuu ya Chama cha Mapinduzi. Kimsingi sio wazo baya ila Nyerere mwenyewe alishtuka kuufanya katika kuufanyia maendeleo kwa kuwa kisiasa watu watajitambua na CCM itapoteza taswira. Serikali hii imevunja kanuni ya huu mji haukutakiwa kuendelezwa ili CCM itawale.
Yapo mengi ya kuelezea kwangu mimi. Wadau kama mnayo kuhusiana na mji huu mnaweza kutiririka.