Kufeli kwa Serikali kuhamia Dodoma

Kufeli kwa Serikali kuhamia Dodoma

scatter

JF-Expert Member
Joined
Feb 15, 2013
Posts
1,671
Reaction score
940
Wakuu zipo sababu kibao ambazo tukizitaja zinaweza kuwa mwiba mchungu sana lakini itabidi tuzitaje ili kuuboresha mji wa Dodoma ambao umepewa hadhi ya jiji ikiwa kimuonekano baado sana

1. Geografia ya mji wa Dodoma
Mkoa huu ni miongoni mwa mikoa mikame na yenye asili ya jangwa kwa maana hauna mvua za kutosha ikiwa wastani wa mvua zake ni miezi mitatu au minne kasoro. Hivyo uoto wa asili muda wote ni ukame. Najiuliza sana serikali yetu imetenga bajeti kuwekeza katika eneo lenye ukame na kulifanya liwe la kuvutia au wamekurupuka tu.

Tukiangalia miji ya Dubai, Misri yenye hali kama hii ya ukame wametumia gharama kubwa kufanya miji ipendeze.pia ukiacha ukame kuna bonde la ufa limepita pale ambalo kitaalamu linakufanya usijenge majengo marefu kwenda juu.

2. Mzunguko wa pesa
Kwa sasa mkoa huu umekuwa na mzunguko wa pesa kwakuwa kuna uuzwaji mkubwa wa viwanja lakini baada ya hapo sidhani kama kutakuja kuwa na mzunguko wa pesa. Pia uwekezaji unaofanyika hauendani na ungezeko la watu.

Yaani unajenga majengo ya gharama mbali na miji ya watu halafu watu waje wajae kama maji ya bahari ni kitu kigumu sana.

Hii itatokea kwa miaka ya mbele kama 40 au zaidi. Kinachofanyika sasa ni kuharibu pesa za walipa kodi ambazo kurudi kwake itatugharimu miaka mingi.

3. Ni mji wa kisiasa (Makao makuu ya CCM)
Kwa mitazamo ya kawaida tunajua huu mji Nyerere na serikali waliufanya uwe makao makuu ya Chama cha Mapinduzi. Kimsingi sio wazo baya ila Nyerere mwenyewe alishtuka kuufanya katika kuufanyia maendeleo kwa kuwa kisiasa watu watajitambua na CCM itapoteza taswira. Serikali hii imevunja kanuni ya huu mji haukutakiwa kuendelezwa ili CCM itawale.

Yapo mengi ya kuelezea kwangu mimi. Wadau kama mnayo kuhusiana na mji huu mnaweza kutiririka.
 
Aisee sasa kipi ni kipi maana mengi yanasemwa kuhusu Makao Makuu Dodoma.
 
Aisee sasa kipi ni kipi maana mengi yanasemwa kuhusu Makao Makuu Dodoma.
Ukweli ndio huo mkuu huu tuangalie miji mikuu ya nchi mbalimbali duniani haikujengwa kama tunavyofanya sisi hapa tanzania kwa kuhamia dodoma

Fuatilia majiji kama ABUJA , KAMPALA, PARIS, TUNIS halafu uangalie na tunachokifanya sisi utajua kuna siasa za kipuuzi ..hebu jiulize bajeti ya kuujenga mji mkuu dodoma imetengwa na nan ?? Kama sio tunafanya kwa sifa za kisiasa
 
Kama utaki ndo ushakua kaandamane bas we mkeo na familia yko jiwe ndo kaamua sasa
Sijakataa uamuzi wa serikali ila hapo baadae tutakuja kujilaumu kwa uwwkezaji
Kama utaki ndo ushakua kaandamane bas we mkeo na familia yko jiwe ndo kaamua sasa
Sijakataa uamuzi wa serikali.inabidi tukubaliane uwekezaji wake sio wamiaka mitano kama inavyolazimishwa kuhamia huko.. amini nikuambiavyo watendaji wengi wa serikali kimoyo bado wapo dar es salaam .kwa sababu dodoma hakuvutii kwa sasa
 
Angalau wangeyapelekaga Singida aisee kama mikoa ya maana waliikosa.
Dodoma tatizo lake kubwa ni watu na si kingine Wagogo watawakomesha naona bado hamjawajua
MARA MIA MJI UNGEJENGWA MOROGORO KWA KUIKATA KATIKATI UKATENGENGWA MKOA MMOJA UKAITWA MAKAO MAKUU
KWASABABU NI KARIBU NA DAR ES SALAAM
 
Bwana we DSM ndio ishapotea hivyo watu watamiminika Dodoma yaani kufikia 2025 mji uta"double" kama sio ku"triple" kabisa
Kujaa kwa watu mkuu sio kua BIG CITY halafu kwann tuanze upya katika karne ya 21 kuwekeza makao makuu ni too cost mkuu Miji mikuu ya wenzetu haikujengwa kwa kipindi kifupi hivi .tunalishana uongo wakuu
 
Naishauri serikali kuepuka majengo marefu na hasa yasiyopangiliwa wala kuwa na udhibiti. Hali ya hewa ya joto lililokithiri la Dar es salaam limechangiwa sana na ushamba wa kukariri kuwa na majengo marefu ambayo yanazuia upepo. BURE KABISA
sasa kwa Dodoma ambayo haina hata bahari, sijjui itakuaje?!!
 
😝😝😝 Mzee lengo la wazee wa CCM ilikuwa ni kuweka makao makuu katikati ya nchi na si vinginevyo! Na Nyerere aliwakamatia kigezo cha usalama.

Dar Es Salaam ni kamji kadogo sana kama serikali ingeendelea kuwepo huko miaka 20 ijayo unadhani patakuwaje? Hivi tu kuna watu 5 million mmebanana vibaya mno.

Dodoma ni sehemu poa ila tu ina mapungufu makubwa ambayo yatafanya mji uwe mzuri kupita Dar Es Salaam na moja ya pungufu kubwa umeliainisha ni mvua.

Nilipasema Singida, pale ndio katikati kabisa sasa mwa Tanzania pia CCM ndo nyumba yake ya pili baada ya Dodoma Singida kuna vile viziwa angalau kungevutia na mawe mawe yale kama Rock city japokuwa Singida nayo ni semidesert 😝 ila ina kaunafuu!

Pengine haikuchaguliwa huenda miaka hiyo palikuwa chaka sana😝😝
Naisapoti sana serikali kuondoka Dar kwakweli hapafai padogo mno
Singida inawezakana ..ila kwa dodoma itibidi artificial lake and rivers waje wazitengeneze kwa baadae😄😄 mji gani hauna maporomoko na maji ya kule ni ya chumvi tu ukioga unapauka ngozi .UNGEWEKWA MKAKATI WA 20 YEARS WAKUFANYA MABADILIKO YA KWELI
 
Naishauri serikali kuepuka majengo marefu na hasa yasiyopangiliwa wala kuwa na udhibiti. Hali ya hewa ya joto lililokithiri la Dar es salaam limechangiwa sana na ushamba wa kukariri kuwa na majengo marefu ambayo yanazuia upepo. BURE KABISA
sasa kwa Dodoma ambayo haina hata bahari, sijjui itakuaje?!!
Ushauri wako mzuri sana mkuu
 
Wakuu zipo sababu kibao ambazo tukizitaja zinaweza kuwa mwiba mchungu sana lakini itabidi tuzitaje ili kuuboresha mji wa Dodoma ambao umepewa hadhi ya jiji ikiwa kimuonekano baado sana

1. Geografia ya mji wa Dodoma
Mkoa huu ni miongoni mwa mikoa mikame na yenye asili ya jangwa kwa maana hauna mvua za kutosha ikiwa wastani wa mvua zake ni miezi mitatu au minne kasoro. Hivyo uoto wa asili muda wote ni ukame. Najiuliza sana serikali yetu imetenga bajeti kuwekeza katika eneo lenye ukame na kulifanya liwe la kuvutia au wamekurupuka tu.

Tukiangalia miji ya Dubai, Misri yenye hali kama hii ya ukame wametumia gharama kubwa kufanya miji ipendeze.pia ukiacha ukame kuna bonde la ufa limepita pale ambalo kitaalamu linakufanya usijenge majengo marefu kwenda juu.

2. Mzunguko wa pesa
Kwa sasa mkoa huu umekuwa na mzunguko wa pesa kwakuwa kuna uuzwaji mkubwa wa viwanja lakini baada ya hapo sidhani kama kutakuja kuwa na mzunguko wa pesa. Pia uwekezaji unaofanyika hauendani na ungezeko la watu.

Yaani unajenga majengo ya gharama mbali na miji ya watu halafu watu waje wajae kama maji ya bahari ni kitu kigumu sana.

Hii itatokea kwa miaka ya mbele kama 40 au zaidi. Kinachofanyika sasa ni kuharibu pesa za walipa kodi ambazo kurudi kwake itatugharimu miaka mingi.

3. Ni mji wa kisiasa (Makao makuu ya CCM)
Kwa mitazamo ya kawaida tunajua huu mji Nyerere na serikali waliufanya uwe makao makuu ya Chama cha Mapinduzi. Kimsingi sio wazo baya ila Nyerere mwenyewe alishtuka kuufanya katika kuufanyia maendeleo kwa kuwa kisiasa watu watajitambua na CCM itapoteza taswira. Serikali hii imevunja kanuni ya huu mji haukutakiwa kuendelezwa ili CCM itawale.

Yapo mengi ya kuelezea kwangu mimi. Wadau kama mnayo kuhusiana na mji huu mnaweza kutiririka.
Punguza wivu wa kike
 
hoja ya kitoto sana hii, kuwa karibu na Dsm ndio nn sasa?
Ni hoja sahihi kwa sababu
-kuiuchumi naamanisha mtu anaweza fanya shughuli zake dar na morogoro kwa urahisi bila kutumia gharama kubwa.
-ukuaji maeneo ya ubungo kibaha mlandizi na morogoro yatakwenda kwa kasi sana kuufuata mji mkuu kama ungekuwa morogoro.
-morogoro ni mji ambao unavivutio vya kiuchumi mfano milima ya urugulu, mbuga ya selous, mbuga ya mikumi kuwa mji mkuu utakuza uchumi wa mtu mmoja mmoja na nchi kwa ujumla kama utadizainiwa kwa mastar plan ya kueleweka hizi ndio sababu zangu
 
Hilo la maji ya chumvi 😂😂😂 wamelistukia ndio maana majengo yao wakayaweka Chamwino kule kachumvi kapo kwa mbali 😝😝😝
Mafuriko ya jangwani tu serikali wameshindwa kutafuta engineering solution 😂😄 waneenda dodoma kwenye matetemeko. Hizo gharama za kukarabati nyufa za majengo endapo kuna matetemeko sijui zipo au ndio siasa tu
 
Hilo la maji ya chumvi wamelistukia ndio maana majengo yao wakayaweka Chamwino kule kachumvi kapo kwa mbali
Viwanda vya maji kama Kilimanjaro, Dasani nk wawekeze kwa wingi Dodoma maana maji yao mabalozi watanunua kwa wingi sio kwa akili ya kunywa tuu bali hata kuogea ili wasipauke kwa chumvi!
Hakika mzee wetu ni mbunifu wa kuendeleza viwanda, pongezi kwake!
 
Wakuu zipo sababu kibao ambazo tukizitaja zinaweza kuwa mwiba mchungu sana lakini itabidi tuzitaje ili kuuboresha mji wa Dodoma ambao umepewa hadhi ya jiji ikiwa kimuonekano baado sana

1. Geografia ya mji wa Dodoma
Mkoa huu ni miongoni mwa mikoa mikame na yenye asili ya jangwa kwa maana hauna mvua za kutosha ikiwa wastani wa mvua zake ni miezi mitatu au minne kasoro. Hivyo uoto wa asili muda wote ni ukame. Najiuliza sana serikali yetu imetenga bajeti kuwekeza katika eneo lenye ukame na kulifanya liwe la kuvutia au wamekurupuka tu.

Tukiangalia miji ya Dubai, Misri yenye hali kama hii ya ukame wametumia gharama kubwa kufanya miji ipendeze.pia ukiacha ukame kuna bonde la ufa limepita pale ambalo kitaalamu linakufanya usijenge majengo marefu kwenda juu.

2. Mzunguko wa pesa
Kwa sasa mkoa huu umekuwa na mzunguko wa pesa kwakuwa kuna uuzwaji mkubwa wa viwanja lakini baada ya hapo sidhani kama kutakuja kuwa na mzunguko wa pesa. Pia uwekezaji unaofanyika hauendani na ungezeko la watu.

Yaani unajenga majengo ya gharama mbali na miji ya watu halafu watu waje wajae kama maji ya bahari ni kitu kigumu sana.

Hii itatokea kwa miaka ya mbele kama 40 au zaidi. Kinachofanyika sasa ni kuharibu pesa za walipa kodi ambazo kurudi kwake itatugharimu miaka mingi.

3. Ni mji wa kisiasa (Makao makuu ya CCM)
Kwa mitazamo ya kawaida tunajua huu mji Nyerere na serikali waliufanya uwe makao makuu ya Chama cha Mapinduzi. Kimsingi sio wazo baya ila Nyerere mwenyewe alishtuka kuufanya katika kuufanyia maendeleo kwa kuwa kisiasa watu watajitambua na CCM itapoteza taswira. Serikali hii imevunja kanuni ya huu mji haukutakiwa kuendelezwa ili CCM itawale.

Yapo mengi ya kuelezea kwangu mimi. Wadau kama mnayo kuhusiana na mji huu mnaweza kutiririka.
Bonds la ufa! Japani kuna matetemeko mengi sana kuliko Dodoma, hata hivyo Japani inamajengo marefu kuliko yaliyopo Tanzania.
Ukame, pamoja na ukame lakini mji wa Dodoma hauna tofauti na Dar!
Mzunguuko wa pesa, makao makuu ya serikali si mji wa kibiashara, wengi wanadhani ndiko biashara zote zitakakofanyika, mji wa biashara utabaki kuwa Dar.
Makao makuu ya CCM, hili kwa sasa halina uhusiano na makao makuu ya serikali, vyama vyote vikohuru kujenga Dodoma.
 
Back
Top Bottom