Elections 2015 Kuelekea Uchaguzi Mkuu 2015: Ajenda ya UFISADI ni Kama IMEFIA kwa Magufuli na kuzikwa Kwa Lowassa

Mkuu ukiambia you ignorant, usilalamike kuwa unatukanwa, ignorant maana yake ni mjinga, na mjinga ni kutojua, ukishaufuta ujinga, unakuwa sio mjinga tena maana sasa umejua!, kwa vile ulichoandika hapa ulidhani unajua, kumbe hujui, huo ni ujinga!, kazi yangu ni kukuelimisha tuu ili ujue!.

  1. Richmond kweli ni kampuni hewa!, lakini mitambo ya Richmond sio mitambo hewa, ni mitambo ya ukweli!. Gharama za milioni 152 kwa siku, sio za gharama za kulipia jina la Richmond, ni gharama za kuilipia hiyo mitambo kwa siku!, na hapo bado gharama za kulipia umeme unaofuliwa na mitambo ile, na umeme huo huo sio umeme hewa ni umeme kweli!. Ungekuwa na akili, ungeuliza hizo fedha milioni 152 kwa siku zinalipwa kwa nani?!.
  2. Lowassa hakusaini chochote kwenye dili ile, bali alikuwa akipeleka maelekezo ya mwenye mitambo yake!.
  3. Kamati ya Mwakyembe aliposhauri mkataba uvunjwe tuu na hakuna kitakachotokea, mkataba ukavunjwa, Tanzania tukapigwa faini ya bilioni 90, bungeni wakaahidiwa hatulipi. Kwa taarifa yako, tozo ile tumeilipa kisiri siri!, umeme umepandishwa kufidia na Watanzania tunakamuliwa hadi kesho!. Ungekuwa na akili ungeuliza kama serikali iliahidi hailipi, imekuwaje tena tumelipa?, kwa nini tulipe kisiri siri/, na hizo fedha zimelipwa kwa nani?!. Na baada ya kulipishwa waliojitia kimbelembeli kuwa eti hatulipi, wako wapi, wamefanywa nini?!, Tanzania inhekuwa Chini, saa hizi hao jamaa ingekuwa ni historia tuu!.
  4. Zitto akashauri ama tuitaifishe mitambo au tuinunue!, maji yalipopungua, serikali yetu ikaamua kuiwasha mitambo ya IPTL yenye kutumia gharama mara 100 ya Dowans, huki ikituchafulia sasa hizi ni akili au matope!.
  5. Sasa kwa taarifa yako, ule mkataba wa kinyonyaji wa Richmond, bado upo, na ile capacity charge ya shilingi milioni 152 bado inalipwa daily!. Mitambo ya Dowans ndio hii, mitambo ya Simbion na mkataba ndio ule ule!, walio ilaani Richmond ndio walio ishangilia Simbion!. Nilifikiri ungetaka kujua ilikuwa tunaendelea kulipa, na anayelipwa hizi fedha ni nani?!.
Laiti ungelijua Lowassa kabeba zigo la nani, na kavumilia kiasi gani, utakubaliana na mimi, kama nampa pekee ya kumshukuru ni kumpatia urais kama asante yake, bora hata huo urais apewe, tusonge mbele, kuliko akinyimwa na akaamua kusema, huo ndio utakuwa mwisho wa kitu kinachoitwa CCM.

Laiti mngelijua Simbion ndio ile ile Richmond na capacity charge ile ile, mkataba ule ule, watu humu msingesema, mngejinyamazia tuu kama Lowassa!. Hutuoni watu humu tumejinyamazia usidhani ni wajinga!, tuna maana yetu!.

Pasco

Huyo Lowasa wako mwenyewe aliahidi ataongelea sakata la Richmond pale Arusha lakini hakuluongelea na anakimbia kuliongelea. Unafikiri ni kitu gani anaficha kuhusu Richmond? Kama alibeba msalaba ambao sio wake kwa nini asituambie wapiga kura huo msalaba ulikuwa wa nani kwa nini afiche?
Ni wakina nani a najaribu kuwalinda.
Hebu jibu hapo Pasco.
 
Huyo Lowasa wako mwenyewe aliahidi ataongelea sakata la Richmond pale Arusha lakini hakuluongelea na anakimbia kuliongelea. Unafikiri ni kitu gani anaficha kuhusu Richmond? Kama alibeba msalaba ambao sio wake kwa nini asituambie wapiga kura huo msalaba ulikuwa wa nani kwa nini afiche?
Ni wakina nani a najaribu kuwalinda.
Hebu jibu hapo Pasco.
Subiri kidogo vikao vya maamuzi vya CCM, vilikate jina la Lowassa, then utajua kila kitu, ila pia Ikulu, CCM itafanya kuisikia tuu!.

Pasco
 
See
Subiri kidogo vikao vya maamuzi vya CCM, vilikate jina la Lowassa, then utajua kila kitu, ila pia Ikulu, CCM itafanya kuisikia tuu!.

Pasco

Ha ha ha ha haya Mr. Pasco. Lakini pia moja ya changamoto kubwa mliyonayo ndani ya chama ni tabaka la watu wachache wenye fedha kuwa na nguvu sana ndani ya chama kiasi kwamba wana uwezo wa kuchagua nani awe rais kwa sababu ndo wafadhili wakubwa wa kampeni na kwa bahati Mbaya tabaka hili ndo lina picha mbaya sana kwa wapiga Kura kwani wengi wao ni mafisadi na baadhi yao wameonekana wazi kuwa karibu na Lowasa kama vile Rostam Aziz na Nazir Karamagi. Swala hili Bwana Pasco unalizungumziaje hasa ukizingatia chama kimeshindwa kabisa kuachana na kikundi hiki cha mafisadi.
 
Subiri kidogo vikao vya maamuzi vya CCM, vilikate jina la Lowassa, then utajua kila kitu, ila pia Ikulu, CCM itafanya kuisikia tuu!.

Pasco

Kwa hiyo kuna blackmailing hapa!

Pasco tuelimishe sisi wajinga kitu kimoja....kama hili dubwana nyonyaji la richmond na sasa simbion litasitishwa rasmi iwapo EL ataingia madarakani ???

Yaani tungependa kuona hili ndio suala la kwanza kabisa kuanza nalo ukiachana na foleni ya Dar.

Tunataka sikia wale wapigaji wa escrow wasiosafishwa wanapigwa tukio na mzee wa maamuzi magumu.

Tunataka kusikia sauti kali na kuona dhamira na vitendo vya kuukomesha ufisadi iwe imetoka kwa shetani(fisadi) au malaika.

Na hii ndio italeta maana ya kuwa ajenda kuu ya mwaka huu ni ufisadi na atakayepewa ridhaa ni yule tu anayepambana na kuweka malengo na mpango wa kuung'oa ufisadi.


Napata shida kuona watia nia wakijaribu kutuletea hadaa zao za 'uchumi kupaa' na blah blah nyingine.

cc: Pasco
 
Last edited by a moderator:
Ndugu wanajamii Nawaza kwa Sauti,

Imagine CCM wangemteua Lowasa kuwa mgombea nafasi ya Urais kwa tiketi ya chama chao, ni ipi ingekuwa ajenda namba 1 ya upinzani kwa wananchi dhidi ya CCM baada ya Katiba mpya?

KUCHAGULIWA KWA MAGUFULI na CCM ni kama KUUA hoja hii ya ufisadi kwa upinzani kwani rekodi yake ya utendaji kazi iko wazi na Ufisadi wake wa nyumba za Serikali ni wa kutafuta kwa tochi na aueleweki vizuri kwa wapiga kura wa kawaida..

KUKARIBISHWA KWA LOWASSA UKAWA ni mazishi ya Ajenda hii kwani nguvu kubwa itaelekezwa katika kutangaza sera za ukawa na KUMSAFISHA Lowasa na "Washkaji" zake atakaoamia nao UKAWA. kuna msemo kuwa "USIMCHOKOZE CHIZI WAKATI UPO KTK NYUMBA YA VIOO" kuishutumu CCM kwa ufisadi ni sawa na kumchokoza chizi.

MCHANGA WA MWISHO KTK KABURI LA AJENDA hii ni kauli za viongozi wa ukawa wakiongea na wanahabari kuwa mtu awezi kuitwa fisadi mpaka athibitishwe na MAHAKAMA! lol. kwa maneno haya Zee la Makengeza, Rosta, Tiba,na wote wa ESCROW, MEREMETA, EPA nk ni watu safi mpaka mahakama itakapothibitisha vinginevyo. Mafisadi labda ni Mramba na Yona.

Kwa kuwa wanasiasa ni opportunists usishangae kuona baadhi ya viongozi na wagombea ubunge/udiwani wakitoka CDM, NCCR, NLD, CUF kuelekea ACT kutake advantage ya Ajenda hii kutetea nafasi zao.

Vyovyote itakavyokuwa UFISADI si tu kete ya kisiasa bali ni janga la kitafa.

Mwisho wa kuwaza kwa sauti.
 
Umewaza vyema sana...
Wamemdhalilisha sana Dr Slaa...mzee huyu alipambana sana kwaajili ya Chadema..Leo wanamwambia akae pembeni ili fisadi awe dereva!
Huyo Zombie waliomchukua ataishia kuwa rais wa UKAWA...
 
SIASA ni mchezo mchafu, vikao vilivyokaa mfululizo vya CDM juu ya majadiliano na LOWASA ndio vimezaa kukubalika kwake na viongozi wa CDM, hembu tujiulize kama LOWASA aliwahakikishia CDM kuwa hahusiki na RICHMOND na ushahidi akauweka mezani munadhani huko CCM kuna usalama, maana itakuwa zile tetesi kuwa MZEE WA KAYA anahusika labda zina ukweli, naamini CDM sio wajinga wanajua wafanyalo.......LOWASA mwenyewe mara kadhaa keshasikika akisema hahusiki na RICHMOND ila alijiuzuru kuiponya iliyokuwa SERIKALI yake na JK akaita kuwa ni ajali ya kisiasa.........CCM na CDM vyote ni vyama vya SIASA na wote wanasubiria kosa la mmoja ndio wafanye ngazi ya kupandia, ccm wamefanya kosa kwa LOWASA wenzao wamepata pa kushika.
 
Trust me hiyo agenda ni pana sana na hakuna atakayebaki kuanzia CCM hadi huko UKAWA.
Unaweza ukawa unajidanganya kuwa wapo wasafi ila nakuhakikishia sio CCM wala UKAWA, kote pameoza ukitumia kigezo hiki cha Ufisadi.
Tafakari mara mbili mbili.
Ukihadithiwa madubwasha wanayofanya viongozi unaowadhani ni wasafi utaomba masikio yako yasingekuwa yanasikia.
Luku vere

Bora hukunihadithia mkuu
 
Mnataka kumfanya Lowassa ahairishe zoezi ..CCM tunatengeneza mahakama maalumu la kudeal na mafisadi chini ya Magufuri ili tuwafunge akina Lowassa
 
Katika uchaguzi wa mwaka huu agenda kubwa inayopaswa kuzungumzwa na kila mgombea hasa wanaogombea nafasi ya uraisi inapaswa iwe UFISADI kwani katika yale mambo matatu aliyoyasema Baba wa Taifa yanayoturudisha nyuma, yaani MAGONJWA, UMASIKINI, na UJINGA, tatizo la nne ni UFISADI ambao unaweza pia ukawa ndio msingi wa hayo matatu.

Hivyo basi raisi ajaye anapaswa atuambie atafanyaje ili kupunguza ama kuondoa kabisa UFISADI? naita compulsory agenda kwasababu msingi mkubwa wa wananchi kutaka mabadiliko ni juu ya suala la UFISADI. Wagombea tuelezeni juu ya kuondoa ufisadi asiyeweza basi hafai.
 
CCM waliuasisi UFISADI miaka yote sasa wanapowaambia wanasema maovu yao.Huwezi kuzungumzia CCM bila kutaja UFISADI
 
Back
Top Bottom