meningitis
JF-Expert Member
- Nov 17, 2010
- 8,349
- 4,674
Mwaka 2010 hoja ya udini na ufisadi zilitawala katika kampeni na kupelekea kosakosa ya Chadema kuingia magogoni.
Tunapoelekea oktoba 2015 tunaona hoja ya UFISADI ikiibuka tena kama dhambi ya kuiadhibu ccm.
Fikiria kuhusu watuhumiwa wa Escrow, wale waliosafishwa vs walioachwa bila kusafishwa vs walioachwa bila kutuhumiwa.
Taarifa ya CAG imekuja wakati mbaya sana, hata kama upotevu wa matrillion 2014 ni sawa na upotevu wa mabilioni mwaka 2010.hoja itabaki kuwa ni upotevu mkubwa.
Mgombea kutoka pande yoyote ni lazima awe tayari kujibu hoja dhidi ya ufisadi na kutoa ahadi dhidi ya mafisadi.
Nani ni nani? Tusubiri tuone!
-----------
July 27
Tunapoelekea oktoba 2015 tunaona hoja ya UFISADI ikiibuka tena kama dhambi ya kuiadhibu ccm.
Fikiria kuhusu watuhumiwa wa Escrow, wale waliosafishwa vs walioachwa bila kusafishwa vs walioachwa bila kutuhumiwa.
Taarifa ya CAG imekuja wakati mbaya sana, hata kama upotevu wa matrillion 2014 ni sawa na upotevu wa mabilioni mwaka 2010.hoja itabaki kuwa ni upotevu mkubwa.
Mgombea kutoka pande yoyote ni lazima awe tayari kujibu hoja dhidi ya ufisadi na kutoa ahadi dhidi ya mafisadi.
Nani ni nani? Tusubiri tuone!
-----------
July 27
Ndugu wanajamii Nawaza kwa Sauti,
Imagine CCM wangemteua Lowasa kuwa mgombea nafasi ya Urais kwa tiketi ya chama chao, ni ipi ingekuwa ajenda namba 1 ya upinzani kwa wananchi dhidi ya CCM baada ya Katiba mpya?
KUCHAGULIWA KWA MAGUFULI na CCM ni kama KUUA hoja hii ya ufisadi kwa upinzani kwani rekodi yake ya utendaji kazi iko wazi na Ufisadi wake wa nyumba za Serikali ni wa kutafuta kwa tochi na aueleweki vizuri kwa wapiga kura wa kawaida..
KUKARIBISHWA KWA LOWASSA UKAWA ni mazishi ya Ajenda hii kwani nguvu kubwa itaelekezwa katika kutangaza sera za ukawa na KUMSAFISHA Lowasa na "Washkaji" zake atakaoamia nao UKAWA. kuna msemo kuwa "USIMCHOKOZE CHIZI WAKATI UPO KTK NYUMBA YA VIOO" kuishutumu CCM kwa ufisadi ni sawa na kumchokoza chizi.
MCHANGA WA MWISHO KTK KABURI LA AJENDA hii ni kauli za viongozi wa ukawa wakiongea na wanahabari kuwa mtu awezi kuitwa fisadi mpaka athibitishwe na MAHAKAMA! lol. kwa maneno haya Zee la Makengeza, Rosta, Tiba,na wote wa ESCROW, MEREMETA, EPA nk ni watu safi mpaka mahakama itakapothibitisha vinginevyo. Mafisadi labda ni Mramba na Yona.
Kwa kuwa wanasiasa ni opportunists usishangae kuona baadhi ya viongozi na wagombea ubunge/udiwani wakitoka CDM, NCCR, NLD, CUF kuelekea ACT kutake advantage ya Ajenda hii kutetea nafasi zao.
Vyovyote itakavyokuwa UFISADI si tu kete ya kisiasa bali ni janga la kitafa.
Mwisho wa kuwaza kwa sauti.