Waridi
JF-Expert Member
- Mar 30, 2008
- 1,025
- 172
Wakuu,
Habari za uhakika ni kuwa leo katika mkutano wa waandishi wa habari, NCCR kimekuwa chama cha tatu kumtaja mgombea wake mtarajiwa.
Yaelekea ukawa utapambanisha wasomi.
CUF wanakuja na Profesa
NCCR wanakuja na Dokta
NLD nao wamemtaja Dokta
CHADEMA bado kimya, lakini yaelekea watamtaja Dokta.
Habari zaidi kwenye media leo na kesho.
Habari za uhakika ni kuwa leo katika mkutano wa waandishi wa habari, NCCR kimekuwa chama cha tatu kumtaja mgombea wake mtarajiwa.
Yaelekea ukawa utapambanisha wasomi.
CUF wanakuja na Profesa
NCCR wanakuja na Dokta
NLD nao wamemtaja Dokta
CHADEMA bado kimya, lakini yaelekea watamtaja Dokta.
Habari zaidi kwenye media leo na kesho.
Ni miaka takribani ishirini tangu Watanzania tulipoanza kuchagua viongozi wetu wa nchi tukiwa ndani ya mfumo wa vyama vingi. Katika miaka yote hiyo CCM imeweza kushinda chaguzi katokana na uchanga wa vyama vya siasa vilivyoshiriki uchaguzi miaka hiyo ya nyuma.
Pia uzoefu wa chama tawala katika siasa za Afrika umesaidia sana katika ushindi wao. Katika chaguzi za karibuni yaani kuanzia mwaka 2000, chama cha Upinzani cha CUF kilionekana kukubalika sana miongoni mwa Watanzania, CCM kwa kuona hatari iliyokuwa ikiwakabili huko mbele wakatafuta eneo la udhaifu lililoko ndani ya CUF kisha wakalitengenezea propaganda ili kuidhohofisha CUF, na kwa vile CUF hawakuwa wamejiandaa kukabiliana na propaganda za na namna ile kutoka CCM wakajikuta wanayumba na kudhohofika kisiasa.
Kuanzia mwaka 2010 CHADEMA wakaibuka kama chama chenye nguvu zaidi kisiasa kiasi kuitikisa CCM vilivyo katika mwaka huo wa uchaguzi. Lakini kama ilivyokuwa kwa CUF, CCM walifanikiwa kuona upenyo wa kuishambulia CHADEMA kwa propaganda zile zile walizozitumia dhidi ya CUF. Kwa mara nyingine tena Watanzania wakakawizwa kupata utawala walio utamani wa chama mbadala.
Muungano wa vyama vya siasa nchini ni jambo lililokuwa linangojewa kwa hamu kubwa na Watanzania wengi katika uchaguzi mkuu wa mwaka huu 2015 katika wakati ambao wananchi wameichoka mno CCM,hasa huu muungano unaohusisha vyama viwili vyenye wafuasi wengi hapa nchini vya CHADEMA na CUF. Hii ni hatua moja kubwa sana kuelekea kuiondoa CCM madarakani,hatua inayofuata kwa UKAWA ili kuitoa CCM madarakani ni kumtafuta mgombea wa urais atakayekubalika kirahisi na pande zote mbili.
Kama atapatikana mgombea wa urais atakayeweza kukubalika na WanaCUF na WanaCHADEMA kwa urahisi basi kazi ya kuifurusha CCM madarakani itakuwa rahisi kama kuvunja biskuti kwa meno. Mgombea wa urais wa UKAWA licha ya kuwa na sifa stahiki za kuongoza ofisi kubwa kama ya urais lakini pia aweze kukubalika na Watanzania wa imani tofauti tofauti hasa miongoni mwa wafuasi wa imani kubwa mbili hapa Tanzania, za Wakristu na Waislamu.
Mgombea wa urais atakayeweza kuzileta imani hizi mbili pamoja dhidi ya adui mmoja ambaye ni CCM. UKAWA (CHADEMA, CUF,NCCR-Mageuzi na NLD) tunaamini busara yenu katika kutuletea mgombea sahihi wa urais atakayeweza kuing'oa CCM madarakani