Kudhulumiwa na mtu unayemuheshimu

Kudhulumiwa na mtu unayemuheshimu

Pesa ni shetani mkuu hata Mimi imewahi kunitokea nikadhulumiwa na MTU niliyekuwa namkubali sana kumuheshimu sana.

Akachukulia udogo wangu kama fimbo ya kunichapia alafu akanijibu hakuna mkamilifu. Kufupisha story pesa zangu alilipa na tukikutana yeye ndio hunipa heshima. Mshenzi sana yule nilimnyoosha akanyooka

Naomba utupe mbinu kaka, ulimfanya nini, maana nami nina mjomba wangu amenizurumu laki 6 , na siwezi kata tamaa siwez ipotezea hii laki 6 razima niipate kwa mbinu yoyote,[emoji35]
 
Mkuu nakushauri.

Kamwe Usithubutu kumkopesha Hela mwafrika hasa mtanzania.

Tena kiasi kikubwa cha pesa, Usithubutu

Mimi hata mtu anililie shida kiasi gani siwezi kumkopa.

Nitampa kiasi kidogo tu, kama msaada,Baada ya hapo kila mtu apite na hamsini zake.

Sent from my Infinix X657B using JamiiForums mobile app
Sawa mkuu ni funzo zuri Sana umenipatia na ntajitahidi Kuwa makini
 
Pia kuna mbinu wanatumiaga matajiri unakuta anakuomba nikopesha laki 7 ntarejesha na riba labdah.......kwakuwa unamwamini na uwezo wake unaonekana ni mzuri baasi unamkopesha

Muda ukifika wa marejesho ni kalenda tu....na akiona unambabaisha Sana anakutishia maisha ila una uwakika uwezo anao wakukulipa

Hivo swala la kukopesha mtu linahitaji umakini mkubwa sana
 
Mmh umempa au amaejichukulia tu
Kuna pesa tulipewa ya mgawo kutoka serekaliNi kufidia eneo serekali imechukuwa Sasa kila mtu kapew ten ten m

Pesa ziliingia kwenye account ya mdg angu nikamuambia dogo akae na hzo pesa nitafute kiwanja akalipie siku ya siku nimepata kiwanja namjulisha dogo akafanye malipo nashangaa dogo anasema sister kachukua hzo pesa zote a atarudisha tareh 7 nikamuuliza ulitoaje pesa bila kunijulisha mm au ssiter anachukuaje bila kuniambia mm dogo kimya Hadi leo Sina kiwanja wala hyo milion 10 ssiter Hana amaekwenda kufungua baishra na biashra imekuwa ngumu Ni tafrani

Jana nimetoka kuongea na mam ili angilie Kat swal hili mnk tunakokwenda kutakuwa na ugomvu mkubwa mno

Na Hapa nikimaliza namtumia msg huyu dad angu na mkopi na dogo Kisha nampigia Tena mama nimsikikize kwa Mara ya mwisho kabla sijaenda kutaifisha Mali zake
 
Pesa ni shetani mkuu hata Mimi imewahi kunitokea nikadhulumiwa na MTU niliyekuwa namkubali sana kumuheshimu sana.

Akachukulia udogo wangu kama fimbo ya kunichapia alafu akanijibu hakuna mkamilifu. Kufupisha story pesa zangu alilipa na tukikutana yeye ndio hunipa heshima. Mshenzi sana yule nilimnyoosha akanyooka
Pole sana mkuu. Watu wakatili sana. Huwa hawajali hisia na maumivu ya wengine. Mimi huwa sihangaiki sana nikishaona wanisumbua. Huwa nakusamehe tu kulinda ujamaa wetu ili na mimi nisiumie. Pesa haijawahi kukaa ktk usalama. Pesa huwa waislam wanasemaga imekaa kwenye moto
 
Pesa sio vizuri umkopeshe MTU mtaishia kuonana wabaya so kwa wazee wa dirt Money they knows about this .

LOVE ur Money
Spend it wisely for ur own and not anybody else.

Mtu usimpe PESA mpe vitu vingine maana pesa sio kitu Cha kugawa Mtu Kama anahitaji pesa Mwambie aende aweke vitu vyake bond au katika Taasisi za PESA.
 
Huu uzi nimeuona muda mbaya sana.. kuna jamaa hapa anataka nimuazimishe kama 200k hivi.. mwisho wa huu mwezi atanipa.

Sasa.. mbona kama naanza kuogopa ogopa.. maana hapo ni kilo 20 za sato hizo. Kulaleki.
Wanasemaga hivyo hivyo kwamba mwazime baada ya wiki kadhaa kuna fedha anatarajia kuzipata atarudisha mpe sasa hiyo fedha,ana anza kukuona tena wewe ndio adui badala ya rafiki .Kama ni mtu wa karibu na wewe mpe kama kumpa potelea mbali kiasi kidogo cha fedha kuondoa lawama au kama ni mtu wa mbali akupe Bond kitu chochote chenye thamani then uumpe maokoto
 
Ishu nilimuachia afanye negotiation na watoa huduma fulani afu mimi ni focus na kazi sasa amount aliyokuja kuniambia mimi nikakubali sasa katika kuuliza na kutaka kujua ile huduma ina cost kiasi gani nimegundua jamaa kaninyoosha pakubwa sana.
Haujadhulumiwa mkuu piga kimya ila mkwepe
 
Wanasemaga hivyo hivyo kwamba mwazime baada ya wiki kadhaa kuna fedha anatarajia kuzipata atarudisha mpe sasa hiyo fedha,ana anza kukuona tena wewe ndio adui badala ya rafiki .Kama ni mtu wa karibu na wewe mpe kama kumpa potelea mbali kiasi kidogo cha fedha kuondoa lawama au kama ni mtu wa mbali akupe Bond kitu chochote chenye thamani then uumpe maokoto
Alafu sasa moja ya weakness yangu ni kudai hela. Swala la kudai mtu siliwezi kabisa.

Huwa naacha tu ingawa kichwani na moyoni nakuwa nishakudelete kabisa hata ukija kurudisha baadae ndio itabaki hivyo kwamba connection kati yetu haipo tena.
 
Inapokuja ishu ya pesa hakuna anayestahili kuaminiwa roho yangu inaniuma sana tena sana kwa mtu ambaye niliweka trust kwake kunipiga pesa ambayo kimsingi nilistahili kuipata kwa kuzingatia energy na time niliyowekeza katika kuhakikisha kila kitu kipo undercontrol.

Kuna roho inaniambia nikae kimya nimuachie Mungu lakini roho nyingine inaniambia huo ni Ujinga kila nikifikiria amount aliyonipiga natamani kulia.

Wakuu najua hayawahusu ila nimeona niandike hata humu atleast nipate relief nipo namuandalia waraka hata kama hatonipa hiyo pesa hajue nimeumia sana tena sana.
Shirikiana na Katibu wa TEC bwana Kitine, yule ni fundi wa kuandika WARAKA hutojuta🤣🤣🤣
 
Back
Top Bottom