Kudeka/ Kudekezwa

Unaweza kunipa mfano wa kudeka kwa mtu aliye mbali na mtu au watu wanaomdekeza?

Unaweza kunipa mfano au mifano ya mtu anayejitegemea na ambaye anadeka?

Nakushukuru kwa michango yako.

MTU WA MBALI:
mfano ni mtu ambaye haiishi siku bila kupiga siku kulalamikia (kwa anayemdekea) mazingira anayoishi na watu hata kama mazingira sio mabaya kihivyo.
Hiyo ni kwa sababu kuna mambo anayakosa kutoka kwa mdekezaji wake.
Kama umepitia maisha ya hosteli utaelewa hapa. Tena wengine hadi wanalia.
Kila jambo kwao ni baya pengine kwa sababu linafanywa tofauti na alivyozoeshwa.
WANAOJITEGEMEA:
mfano ni wale ambao kila likizo ya kazi lazima aende kwao (kama anadekezwa na mzazi) pia wapo tayari kuomba viruhusa au hata kuacha shughuli zao warudi kwao au kama ameoa hupenda kuishi na wazazi wake pia.
NB: Katika hiyo mifano inawezekana pia wakawa wanafanya hvyo kwa sababu zingine na sio kudeka.
 
kuna siku tulikuwa na safari ya kikazi tukatumia gari ya work mate wangu.ni mkaka anaejipenda sana,very smart ila mtoto wa mama sana japo hakai na wazazi.yaani buti ya gari imejaa nguo chafu zimetupwa ovyo kabisa!kuna viatu,na underwears chafu!anatembea hadi na pasi(iron box!).sipati picha ya huko nyumbani kwake ni kuchafu kiasi gani!hata kama nguo utasaidiwa kufua shurti zikae kwa utaratibu pia.kama anapika ndio itakuwa balaa.ni mfano tu,japo kwa nje anaonekana smart,ila anadeka

Duh! huyo sasa kazidi. Hakuna kitu ninachokichukia kama uchafu. Na kuna watu wana tabia mbaya sana ya "kuishi" kwenye magari yao. Unakuta ana mazagazaga kibao kwenye gari kuanza chupi zilizokwishavaliwa, vyombo vya chakula, mifupa ya vipapatio vya kuku, tssue paper zilizotumika (usitake hata kujua zimetumikaje), miswaki kadhaa, makaratasi, vipande vya mikate vilivyokauka....heheheheeee we acha tu.


"
 
MTU WA MBALI:
mfano ni mtu ambaye haiishi siku bila kupiga siku kulalamikia (kwa anayemdekea) mazingira anayoishi na watu hata kama mazingira sio mabaya kihivyo.
Hiyo ni kwa sababu kuna mambo anayakosa kutoka kwa mdekezaji wake.
Kama umepitia maisha ya hosteli utaelewa hapa. Tena wengine hadi wanalia.
Kila jambo kwao ni baya pengine kwa sababu linafanywa tofauti na alivyozoeshwa.
WANAOJITEGEMEA:
mfano ni wale ambao kila likizo ya kazi lazima aende kwao (kama anadekezwa na mzazi) pia wapo tayari kuomba viruhusa au hata kuacha shughuli zao warudi kwao au kama ameoa hupenda kuishi na wazazi wake pia.
NB: Katika hiyo mifano inawezekana pia wakawa wanafanya hvyo kwa sababu zingine na sio kudeka.

Safi sana Da'Huuuus........
 
kudeka-kujua kufanya kitu ila kusuasua au kutokufanya mpaka afanyiwe ilhali anafahamu anapendwa na kuna mtu lazima atamsaidia. Siyo watoto tu hata watu wazima hudeka.

kudeka hii hii pia inanichanganya mana nahisi inaendana na upendo mkubwa juu ya mtu anaedeka na kudekewa. Ila suala la kujitegemea linaweza kuwepo hata kama mtu kadeka au kudekezwa.
 
KUDEKEZWA: Ni kupendwa sana kiasi kwamba hata ukifanya baya, au lisilo lizisha haukanwi unaachiwa tu, na kufichiwa mahovu yako kwa vile unapendwa. Na yule anae kupenda haoni yale makosa ni makubwa hata ukiua mtu, yeye anaona kama umeua paka. Na unafanyiwa kila utakalo. Unapewa yes tu, kila unachoomba taka. haupewi no. Na ukipewa no, basi ndani yake inaupendo na upole sana.
 
king'ast huyo workmate mwenzako ni mchafu wa asili. Kuna watu kibao wanadeka na ni very smart kila idara! Yani kuanzia room kwake,garini,sebuleni nk. Huo ni ulimbukeni c kudeka. Hi ya kudeka kwa kufuli zake pia, ni kali mtu mzima teh!
 
kudeka-kujua kufanya kitu ila kusuasua au kutokufanya mpaka afanyiwe ilhali anafahamu anapendwa na kuna mtu lazima atamsaidia. Siyo watoto tu hata watu wazima hudeka.

kudeka hii hii pia inanichanganya mana nahisi inaendana na upendo mkubwa juu ya mtu anaedeka na kudekewa. Ila suala la kujitegemea linaweza kuwepo hata kama mtu kadeka au kudekezwa.

So this is more intricate than I thought. It seems as if everything boils down to differences of opinion as to what exactly entails being spoiled. Perfectly understandable.

Sasa mtu anayejitegemea anadekaje?
 
So this is more intricate than I thought. It seems as if everything boils down to differences of opinion as to what exactly entails being spoiled. Perfectly understandable.

Sasa mtu anayejitegemea anadekaje?

inategemea anadeka kwa nani ,wakati gani na mahali gani!
 
mfano mi mwenyewe naishi mwenyewe lkn nikienda kwa mamangu nadeka ile mbaya pia kuna mfanyakazi mwenzangu anaishi mwenyewe lkn jamaa akitia maguu bnt anadeka kichizi. Mi nakushauri tafuta mtu anayekupenda kwa dhati muanze kudekezana uone how joyful it is!
 
mfano mi mwenyewe naishi mwenyewe lkn nikienda kwa mamangu nadeka ile mbaya pia kuna mfanyakazi mwenzangu anaishi mwenyewe lkn jamaa akitia maguu bnt anadeka kichizi. Mi nakushauri tafuta mtu anayekupenda kwa dhati muanze kudekezana uone how joyful it is!

Hahahaa neyro bana...you crack me up!
 
Definition siijuhi nachojua kila mtu anapenda kudeka akipata wa kumdekea na atakae kubali kumdekeza.
 
mi mwenzenu nina tatizo,sijui watu wananionaje.....watu wanapenda kunidekea ila mimi nikideka wanasema hata hufananii.....kinaniuma sana!

sina cha kuongeza kwemye definition,nakubaliana na tafsiri ya wengi.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom