Nehemia Raphael
New Member
- May 11, 2026
- 3
- 9
Mimi mkazi wa Tabora. Naomba kuwasilisha taarifa kuhusu mfumo unaotumia ahadi za ajira kuwavutia vijana kutoka maeneo mbalimbali nchini kwenda Mwanza kwa maelezo ambayo hayatoi ukweli kamili wa shughuli zinazofanyika.
Mimi binafsi nilielekezwa kuwa kuna nafasi za kazi ya kusambaza dawa katika hospitali mbalimbali nchini. Kutokana na maelezo hayo, nilisafiri kutoka Tabora kwenda Mwanza kwa matumaini ya kupata ajira ya kawaida.
Baada ya kufika Mwanza, nilitakiwa kufanya malipo mbalimbali yaliyoelezwa kuwa ni sehemu ya mchakato wa ajira. Malipo hayo yalihusisha:
• Kodi ya makazi ya miezi mitatu
• Ada ya semina
• Ada ya usajili/form
• Gharama za chakula
Jumla ya fedha nilizolipa ni Tsh 167,000.
Shughuli hizi nimezikuta zikifanyika katika kampuni linalojiita Natures Way (Empowered Consumerism), lililopo maeneo ya Mlango Mmoja, Mwanza.
Baada ya kuanza kushiriki kwenye shughuli hizo, niligundua kuwa hakukuwa na ajira ya kawaida kama nilivyoelekezwa kabla ya kuondoka Tabora. Badala yake, shughuli inayofanyika ni mfumo wa Network Marketing, tofauti kabisa na maelezo ya awali niliyopewa kuhusu ajira.
Kutokana na hali hiyo, nimeona nimepotezewa muda pamoja na fedha zangu kwa kupewa taarifa ambazo hazikuwa sahihi kuhusu kazi niliyokuwa naenda kufanya. Hadi sasa, baada ya kugundua ukweli huo, nimesitisha kushiriki kwenye semina hizo.
Aidha, kutokana na kujitoa kwenye mfumo huo, kwa sasa wanataka kuniondoa katika eneo nililolipia makazi ya miezi mitatu, huku nikiwa sina uwezo wa kupata nauli ya kurudi Tabora.
Nina wasiwasi kuwa bado kuna vijana wengi wanaendelea kuvutwa kwa ahadi kama hizo za ajira, kisha kuombwa kulipa fedha mbalimbali wakiamini wanaenda kuajiriwa.
Naomba mamlaka husika kufanya uchunguzi wa suala hili pamoja na kusaidia kupata ufumbuzi wa hali ninayopitia, ili kuzuia vijana wengine kuendelea kuathirika kwa namna hii.
Mimi binafsi nilielekezwa kuwa kuna nafasi za kazi ya kusambaza dawa katika hospitali mbalimbali nchini. Kutokana na maelezo hayo, nilisafiri kutoka Tabora kwenda Mwanza kwa matumaini ya kupata ajira ya kawaida.
Baada ya kufika Mwanza, nilitakiwa kufanya malipo mbalimbali yaliyoelezwa kuwa ni sehemu ya mchakato wa ajira. Malipo hayo yalihusisha:
• Kodi ya makazi ya miezi mitatu
• Ada ya semina
• Ada ya usajili/form
• Gharama za chakula
Jumla ya fedha nilizolipa ni Tsh 167,000.
Shughuli hizi nimezikuta zikifanyika katika kampuni linalojiita Natures Way (Empowered Consumerism), lililopo maeneo ya Mlango Mmoja, Mwanza.
Baada ya kuanza kushiriki kwenye shughuli hizo, niligundua kuwa hakukuwa na ajira ya kawaida kama nilivyoelekezwa kabla ya kuondoka Tabora. Badala yake, shughuli inayofanyika ni mfumo wa Network Marketing, tofauti kabisa na maelezo ya awali niliyopewa kuhusu ajira.
Kutokana na hali hiyo, nimeona nimepotezewa muda pamoja na fedha zangu kwa kupewa taarifa ambazo hazikuwa sahihi kuhusu kazi niliyokuwa naenda kufanya. Hadi sasa, baada ya kugundua ukweli huo, nimesitisha kushiriki kwenye semina hizo.
Aidha, kutokana na kujitoa kwenye mfumo huo, kwa sasa wanataka kuniondoa katika eneo nililolipia makazi ya miezi mitatu, huku nikiwa sina uwezo wa kupata nauli ya kurudi Tabora.
Nina wasiwasi kuwa bado kuna vijana wengi wanaendelea kuvutwa kwa ahadi kama hizo za ajira, kisha kuombwa kulipa fedha mbalimbali wakiamini wanaenda kuajiriwa.
Naomba mamlaka husika kufanya uchunguzi wa suala hili pamoja na kusaidia kupata ufumbuzi wa hali ninayopitia, ili kuzuia vijana wengine kuendelea kuathirika kwa namna hii.