Ajira hakuna ila kazi zipo tele

Ajira hakuna ila kazi zipo tele

Mwl Mwakujonga

JF-Expert Member
Joined
Jun 29, 2023
Posts
362
Reaction score
714
Ajira hakuna ila kazi zipo tele.

Je unacheti, au ujuzi au una afya njema au una ulemavu wowote?
Chochote ulichonacho ni fursa

Leo naongea na wewe ambae huko tu nyumbani au mtaani haujui uanzie wapi katika maisha aya.

Kuna habari niliiona katika mitandao ya kijamii, habari ya kina mama wa nyumbani ambao waliiona fursa wakati wengine wanaona ni changamoto wao waliona fursa

Wamama hao waliona vijana wengi ambao wanawatoto wadogo na kupatwa na changamoto za wadada wa kazi wanashindwa kutekeleza majukumu yao vizuri kutokana na kukosa watu wa kuwasaidia kulea watoto wao.

Wamama hao waliona hiyo ni fursa wakaanzisha biashara unaleta mtoto na wako unamwacha hadi jioni unawapa elfu mbili kwa siku watampa chakula watamtunza hadi utakaporudi kutoka kazini.

Wanandoa waliona changamoto ya wadada wakina mama waliona fursa ya kuanzisha daycare

Hata wewe hiko fursa bado tu ujapata kuitazama.

Umemalisha shule au ukusoma au kwa namna yoyote ile hauna shughuli ya kufanya ni kwamba haujaamua kumpa Mungu nafasi akuonyeshe fursa zinazokuzunguka

Kuna shuhuda nyingi ambazo nimeziona kwa macho yangu watu ambao walikuwa hawana chochote leo hii wanamaisha

Mfano kuns kaka ambaye anafanya biashara ya kuuza magari yeye mwenyewe anasema alikuwa mpiga picha tu lakini leo ni mfanyabiashara mkubwa tu wa magari

Kinachoniumiza ni kwmaba tuna vijana wengi lakini hawafanyi kazi, wako vijiweni au namakundi ambayo sio mazuri

Ni kweli ajira hakuna, kazi je ? Ajira zinaweza kukosekana lakini kazi ziko.

Hakuna mtu mkubwa ambaye alianzia juu, kila aliye na mafanikioa anahistoria yake

Changamoto tulizonazo tunatamani kuanzia juu, sio wote tutaweza kuanzi juu, wengine tutaanzia chini.

Leo hii unakutana na kijana anakuomba pesa ya kula na ni mzima tu hana shida yoyote ni aibu sana

Kuna wakina mama wanatunza familia kwa kazi ya kumwaga zege kwenye site za watu.

Unaweza kusema haha kaka mimi nimesoma chuo kikuu nikamwage zege?.

Sawa ni kweli umesoma sasa kama umesoma unashindwaje kutumia cheti chako kupata kipato

Wako vijana ambao hawakukaa kulalamika juu ya ajira kwa sababu hata ulilalamika hakuna ajira utafanyaje sasa kupa ajira? Wako vijana ambao hawakulalamika waliongia kazini mtaani leo hii sio kama walivyo jana

Nakumbuka miaka kadhaa kuna kaka mmoja alikuwa anafundisha tuition mitaa ya kwetu na kipindi hicho hakukuwa na shule nyingi za private miaka ikapita akafanikiwa kuansisha shule yake na shule yake ni miongoni mwashule bora mtaani kwetu kwa hiyo inawezekana

Mifano ni mingi shushuda ni nyingi, tunaweza kuandika shuhuda na shuhuda lakini kama hauataamua kuchukua atua na kupambana juu ya atima ya kesho yako utabakia hivyo hivyo.

Unakuta kijana anasimu ya bei kali lakini hana kazi ? Sasa hiyo simu yako inakusaidia nini?
Utaskia haha naafatilia michongo kwa wana sasa hiyo michongo mbona haijawai kufanikiwa ?

Waswahili wanausemi gari inayotembea ndiyo inashika mwendo, mafanikio ni atua.

Kuna watu wametumia simu zao vizuri unakutana na kijana kazi yake ni kupiga picha vitu madukani na kutafuta wataje, nawengine wanashuhudia kabla ya kumiliki maduka yao walikuwa wanapiga picha ya bidhaa za watu na kupost kwenye mitandao na leo hii wanamiliki ofisi zao.

Kuna kijana mmoja hata simjua hana kaa wapi nachojua nikiitaji kitu kutoka jijini najua nitamtumia fedha atakwenda dukani ataninunulia mzigo atanitimia nampa ya usumbufu maisha yanakwenda pia namuunganisha na watu wengine

Usitafute kisiingizio mara hoo mimi sikusoma wala wazazi wangu hawako, kama kweli waliosoma ndio wangefanikiwa basi tusingekuwa na matajiri ambao hawakwenda shule, lakini leo tuna matajiri wengi hawakwenda shule kabsa na wengine wameishia darasa la saba

Hacha kutafuta sababu za kutoakuanza hanza na ulichonacho, uwe umesoma au haujasoma we pambana na Mungu atakusaidia

Kuna mwingine anasema yeye ni yatima, utajiri au umaskini autegemeia unawazazi au hauna ila bidii na jitiada binafsi ndizo nguzo za mafanikio yako, simama na Mungu akusaidie.
 
Kuongea ni rahisi.....

Motovesheni sipika atakuambia ooh kijana huna kazi, weka degree pembeni nenda hata stand uza maandazi ....

Kubabake utasaga meno
 
Kuongea ni rahisi.....

Motovesheni sipika atakuambia ooh kijana huna kazi, weka degree pembeni nenda hata stand uza maandazi ....

Kubabake utasaga meno
Kukifanya Kwa vitendo inawezekana Kuna bodaboda hapa dom nawamejenga!
 
Kukifanya Kwa vitendo inawezekana Kuna bodaboda hapa dom nawamejenga!
Watu wengi wanatamani wakianza leo na mafanikio wapate leo, hakuna kanuni ya namna hiyo ni lazima ujue soko lako na watu wakujua wakuamini na wakupe fursa. Hata wale wanaofanya mazoezi wanakwambia kawaida matokeo ni baada ya mwezi angalau, hivyo hivyo hata kwenye maisha hauwezi kufanikiwa ndani ya siku moja
 
Watu wengi wanatamani wakianza leo na mafanikio wapate leo, hakuna kanuni ya namna hiyo ni lazima ujue soko lako na watu wakujua wakuamini na wakupe fursa. Hata wale wanaofanya mazoezi wanakwambia kawaida matokeo ni baada ya mwezi angalau, hivyo hivyo hata kwenye maisha hauwezi kufanikiwa ndani ya siku moja
Kwenye mazoezi kwenyewe Kwa mara ya kwanza,viungo vinauma balaa !Kesho unatamani usirudie, Lakini kadri unavyofanya mazoezi,ndivyo viungo vinazoea na kutamani uendelee,hata kwenye utafutaji,unaweza kuuza na usiuze kabisa,kadri unsvyokomaa,ndivyo mafanikio yanakujia!
 
Kwa hiyo baada ya wewe kupata ualimu sisi kulilia ajira unatuona hatuna akili au hatuzioni hizo kazi za kuuza vitumbua
 
Kwa hiyo baada ya wewe kupata ualimu sisi kulilia ajira unatuona hatuna akili au hatuzioni hizo kazi za kuuza vitumbua
Hapana mkuu sio kwamba hatutaki mpate ajira ila wakati tunasubiri hizo ajira tunaweza kuendelea na shughuli zingine za kujipatia kipato kuliko kukaa na kusibiri tu ajira, miaka inakwdnda umri unakwenda mkuu
 
Back
Top Bottom