Kuchepuka haachi mpaka atakapopata anavyovitaka

Kuchepuka haachi mpaka atakapopata anavyovitaka

ruhi

JF-Expert Member
Joined
Feb 26, 2012
Posts
5,157
Reaction score
8,359
Jana nilikua naongea na binti mmoja nikiwa na lengo la kumpa ushauri iliaweze kuacha tabia ya kuchepuka, kwani huyo binti anadate na jamaa ninayemfahamu lakini binti anachepuka sana.

Nilimwambia kwanini usiache kuchepuka na ukae na mmoja ili uweze kutulia. Alinijibu kuwa awezi kuacha kuchepuka kwani hata angekuwa na mimi kuchepuka ni lazima.

Nikamuuliza, kwani kuchepuka uko unatafuta nini. Alinijibu anatafuta yenye mwanya, matege, ATM na CCTV kweli nikabaki niko hoi bila kujua maana yake,nikauliza utachepuka hadi lini. Akajibu pale ambapo atapata zote alizoniambia hapo juu.

Nilishindwa kumwelewa huyu binti jamani, mwenye kuelewa alichokua anamaanisha huyu binti anaisaidi, je ni vyema nikamwambie huyo jamaa anadate nae au nitakua mmbeya.


Kuchepuka siyo dili, baki njia kuu.
 
We muache achepuke tuu,jamaa yake mueleze in-direct,ukimuambia kifala atahisi unavizia demu wake,tumia busara sana kumuokoa jamaa.
 
we muache achepuke tuu,,,, jamaa yake mueleze in-direct......ukimuambia kifala atahisi unavizia demu wake,,,,tumia busara sana kumuokoa jamaa.

Demu anapata kila kitu kwa jamaa, kweli watu wengine hawaridhiki!
 
Kama umepata ujasiri wa kumwambia huyo demu basi ujasiri huohuo ukuongoze kumweleza huyo rafiki yako.
 
Ndugu ruhi kuna vitu tunafanya kwa mazoea, Tabia, Tamaa, Nguvu za giza(pepo), kujitakia, shauku, kuamua na vingine tunafuata tu mkumbo au maneno ya vijiweni. Ni ngumu kujua huyu anasumbuliwa na kipi hapo juu ili umsaidie.

Ukiongea naye kama nawe ukimsapoti anachofanya au ukawa hueleweki (kwa muda) unaweza ukajiridhisha ni kipi kati ya hivyo ili umshauri sawasawa na hitaji lake. vingenevyo hutaweza kumsaidia kwa urahisi kwa namna moja au nyingine.
 
Last edited by a moderator:
Ndugu ruhi kuna vitu tunafanya kwa mazoea, Tabia, Tamaa, Nguvu za giza(pepo), kujitakia, shauku, kuamua na vingine tunafuata tu mkumbo au maneno ya vijiweni. Ni ngumu kujua huyu anasumbuliwa na kipi hapo juu ili umsaidie.

Ukiongea naye kama nawe ukimsapoti anachofanya au ukawa hueleweki (kwa muda) unaweza ukajiridhisha ni kipi kati ya hivyo ili umshauri sawasawa na hitaji lake. vingenevyo hutaweza kumsaidia kwa urahisi kwa namna moja au nyingine.

Watu tusipobaki njia kuu, tutaanza kutumia nguvu nyingi na kubwa sana kwa siku za usoni kurekebisha watoto wetu ndo dalili ninazoona...hizi ni rasharasha
 
Demu anapata kila kitu kwa jamaa, kweli watu wengine hawaridhiki!
Iwapo anapata mahitaji yote kwa jamaa yake basi binti ana pepo la ngono. Labda mshauri jamaa amuoe kabisa na kwa kuwa watakuwa wanaishi wote anaweza kuacha uchepukaji.
 
Iwapo anapata mahitaji yote kwa jamaa yake basi binti ana pepo la ngono. Labda mshauri jamaa amuoe kabisa na kwa kuwa watakuwa wanaishi wote anaweza kuacha uchepukaji.

Demu anaaga jamaa kua anaenda kusalimia ndugu yake kumbe anaenda kwa mchepuko wake, unadhani wakiishi pamoja hataweza kuchepuka?
 
umejuaje anapata.kila kitu???kama jamaa ako ni jogoo la kuchora??haliwiki utajuaje???

Alisema ata angekua mimi angechepuka, amejuaje kua nami jogoo langu haliwikii? Huyu hata umpe nini atachepuka tu....chanzo cha haya ni nini?
 
Alisema ata angekua mimi angechepuka, amejuaje kua nami jogoo langu haliwikii? Huyu hata umpe nini atachepuka tu....chanzo cha haya ni nini?

ntajuaje kama linawika wakati.sijakaa nalo ili nisikie kama alfajiri litawika???
katika mahusiano hakuna mtu anaetoa kila.kitu binadamu wa.hivo hayupogo
 
Demu anaaga jamaa kua anaenda kusalimia ndugu yake kumbe anaenda kwa mchepuko wake, unadhani wakiishi pamoja hataweza kuchepuka?

Inawezekana, tatizo labda hatujui hasa nini sababu ya yeye kuchepuka. Huenda pia hajampata mwanaume anayemridhisha katika mahusiano, kama ni hivyo basi ni shida.
 
ntajuaje kama linawika wakati.sijakaa nalo ili nisikie kama alfajiri litawika???
katika mahusiano hakuna mtu anaetoa kila.kitu binadamu wa.hivo hayupogo

Kwa hiyo kila mtu lazima achepuke ili kupata hivyo anavyokosa kwa huyo jamaa yake?

Mtu yeyote anapotaka kufanya au akifanya kosa lazima ajenge hoja kuhalalisha kosa lake.
 
Mwambia aongeze spidi ya kujichepesha, ila mwisho wa yote ni kuzeeka kabla ya wakati, bint kufanya ovyo ovyo hayo mambo kutamfanya achakae hadi mwenyewe atakuwa anajiogopa. ila mpe hongera.
 
Hicho anachokitumia ni chakwake mwenyewe, kwa hiyo asikupe tabu wala kukumiza kichwa.
 
Unataka umweleze nn jamaa ako kuhus dem wake hebu waache wewe cha kufanya tafta mbinu za kumueleza akuelewe mana hawakawii kusema unamtaka dem wake
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom