Kuchangia harusi/send off

ommymbwambo

Senior Member
Mar 25, 2014
192
66
Hii tabia ya kumchangia mtu ambaye kimsingi hajakurupushwa ni matakwa yake binafsi michango eti anataka kuoa au kuolewa ni sahihi?mtu mmoja unapewa kadi za uanakamati zaid ya saba na kila kamat mchango laki moja na zaid.maoni yenu wakuu.
 
Hii tabia ya kumchangia mtu ambaye kimsingi hajakurupushwa ni matakwa yake binafsi michango eti anataka kuoa au kuolewa ni sahihi?mtu mmoja unapewa kadi za uanakamati zaid ya saba na kila kamat mchango laki moja na zaid.maoni yenu wakuu.
Utamaduni tuliojiwekea sidhani kama kuna tatizo mambo yanakuwa mzunguko leo wewe kesho mwingine, maisha yanaendelea
 
Hii tabia ya kumchangia mtu ambaye kimsingi hajakurupushwa ni matakwa yake binafsi michango eti anataka kuoa au kuolewa ni sahihi?mtu mmoja unapewa kadi za uanakamati zaid ya saba na kila kamat mchango laki moja na zaid.maoni yenu wakuu.

Michango ni sawa..ila kitu ambacho sikubalianinacho ni kuweka minimum amount (cutt-off).
 
Michango sio mbaya kwani ni kusaidiana na kufahamiana zaidi ila kuna wale wanaweka kiwango cha chini labda 50000/= hlf mwenye elfu 30 au 20 je?
 
Michango sio mbaya kwani ni kusaidiana na kufahamiana zaidi ila kuna wale wanaweka kiwango cha chini labda 50000/= hlf mwenye elfu 30 au 20 je?

Toa elfu 20 au 30 upate kadi ya shukrani na elfu 50 upate kadi ya mwaliko mjini hapa atiii....
 
Mi siwez kuchangia watu wanaenda kutusuana..mhudum ongeza bia naona watu wanaleta maada za ajabu..loading error...
 
Kibongo bongo michango muhimu kusaidiana, bila support nouma, maisha yenyewe ya kuunga unga. kama mtu yupo na kipato kizuri, powa afanye peke yake atoe mialiko tu.
 
Mi huwa sipendi zile msg za kila wiki mtu anatuma kwa watu woooote eti "siku zimekaribia, tafadhali wasilisha mchango wako kupitia ...kabla ya tarehe..."! Siku zimekaribia kwa nani, kuoa uoe wewe sisi utupe deadline. Kama mtu ni wa karibu kwako atachanga tu bila reminder kumi kumi. Mtu hajui una responsibilities zako analeta kadi ya mchango ya ndugu yake na binamu yake ya yule shemeji yake wa kule anapokaa anaoa! Some nonsense, u have never even met the person!
 
Michango sio mbaya kwani ni kusaidiana na kufahamiana zaidi ila kuna wale wanaweka kiwango cha chini labda 50000/= hlf mwenye elfu 30 au 20 je?

Unachagua ile inayokuhusu unatoa kiwango stahiki na kuhudhuria,ile ya binamu wa rafiki ambaye wala hujui anafananaje unapeleka 20 au 30 kwa huyo rafiki kum support tu na usiombe card wala kuhudhuria!!
Unakuta siku moja una card 3 za harusi na zote umechangia hujui uende ipi!!!!
 
Back
Top Bottom