Kuchakata mafuta ghafi/petroleum - TANZANIA

Mparee2

JF-Expert Member
Sep 2, 2012
2,585
4,270
Wakati nikiwa mdogo kulikuwa na kiwanda cha kuchakata mafuta ghafi Kigamboni (Kama sijakosea). Nafikiri Mwalimu Nyerere alijua kuwa tukinunua mafuta ghafi, bei itakuwa nafuu sana lakini pia tutabakiwa na end products nyingine kama lami nk ambazo tunazihitaji sana, lakini bado kuna faida za kukuza Ajira nk.

Nafikiri kuna umuhimu wa kufufua hiki kiwanda au pengine kuanzisha Kipya kama kile kimekuwa chakavu. Nasema hivyo nikijua kuwa, hivi karibuni Uganda itaanza kuzalisha mafuta ghafi kwa kiasi kikubwa tu; kwa nini tusitumie hiyo fursa kuchakata hayo mafuta na kuyauza hapa ndani na East Africa hata kama sio yote yanayo baki ndio yakaenda ughaibuni?

Naona kama ni fursa ya wazi wazi.
 
Aiseee! nchi yako ni kama imelaaniwa, inarudi nyuma badala ya kwenda mbele.......fanya utafiti kwenye taasisi mbalimbali kuhusu hali iliyokuwepo miaka 40 nyuma halafu linganisha na leo, utakuja kuniambia. Kwa sasa uchumi unajengwa kwenye mifuko ya wapiga dili....
 
Kuna watu wameshika hiyo biashara ya mafuta Tanzania hawawezi kukubali biashara zao zife baada ya kufufua hicho kiwanda.
 
Back
Top Bottom