Kubenea: Lowassa ameonesha njia

Kubenea: Lowassa ameonesha njia

Hata mkileta maelezo marefu vipi, Lowassa bado sio mtu sahihi kuwepo cdm. Anaweza kurudi tu ccm na kutoa huo ushauri wake mzuri akiwa huko. Ama anaweza kwenda hata TLP na kuongeza nguvu huko na hizo siasa zake. Watavuna watu wengi tu tunaombiwa walimpa kura mpaka cdm ikapata wabunge wengi.
Ikiwa wenye dhambi tu wakitubu tena hata mmoja tu inakua sherehe mbinguni vipi shetani atapoamua kuwa miongoni mwa waliotubu huko mbinguni kutakuwaje?

Hii falsafa inatufundisha nini? Mfumo wa vyama vingi umeanza juzi kiasi ambacho wengi wa wapinzani walikua CCM msipende kuhukumu ilhali nanyi mna dhambi!! Kama mbinguni hata wenye dhambi watubuo hufanyika sherehe vipi huko CDM? Vipi habari za akina sauli kuwa wainjilisti?

Hii hoja yako inasikitisha!!!
 
Kubenea kaamua kuchagua kuwa Upande wa kumuunga Mkono Lowassa dhidi ya Mentor wale Mbowe

Msimamo wa Kubenea unategema uwezo na ujasiri wako wa kumuhonga
Kubenea yupo sahihi. Siasa za kiharakati za akina Lema kwa karne hii hazisaidii
 
Saed Kubenea

Lowassa amekutana na Magufuli, kipindi ambacho chama chake kiko kwenye mkwamo. Hakiwezi kufanya mkutano wa hadhara.

Kimefika mbali zaidi; sasa hata uchaguzi mdogo hakiwezi kushiriki.

Baadhi ya viongozi wakuu chama badala ya kuwaongoza wanachama, nao wamegeuka kuwa walalamishi.

Ni kwa sababu, Chadema ya mwaka 2010 hadi 2014 ya maandamano na mikutano haipo tena.

Katika muktadha huo, njia pekee ya kutoka hapa tulipo ni kujadiliana adui yako. Lowassa amefungua njia hiyo. Ni vema ikatumiwa.

Mwisho

Kubenea kaeleza jambo muhimu sana.
 
Kwa wasiofahamu tu ni kwamba Lowasa na Kubenea wana ukaribu wa miaka mingi hivyo inawezekana kabisa anachoongea kina baraka zake
 
Hilo halina shida maana hakuianzisha cdm yeye bali aliikuta tena ikiwa kwenye hali nzuri ile mbaya. Lakini baada ya yeye kuingia hapo ndio chama kikaanza kuingia nuksi. Aonyeshe kiwango cha mauziano aliyofanya tena kwa EFD receipt na terms za hiyo biashara, wanachama na sisi washabiki tuonyeshwe. Kisha tutaamua tulipe kulingana na faida aliyoingiza huku tukipima madhara aliyoiletea cdm. Ila kama alifanya biashara ya kitapeli itabidi aondoke na waliopeana naye hizo hela. Una lingine?
Makamanda mnahaha. Mbowe hathubutu kumfukuza Lowasa kamwe.
 
Kubenea mzushi sanaaa wewe. Na uko njiani kununuliwa na ccm? Wameshakupandia kidau? Aibu iliyoje kwako!
 
Kubenea yupo sahihi. Siasa za kiharakati za akina Lema kwa karne hii hazisaidii
Kupishana mawazo na kutofautiana na msimamo wa mwenyekiti hii ndio demokrasia tunsyoitaka.

Hatutaki akili za kiccm wote muwe kama treni kinapoelekea kichwa mabehewa yote yanafuata.

Ccm hakuna mwenye jeuri wala uthubutu wa kutofautiana na mwenyekiti wao, hawa ni wafu.

Hii ndio demokraia tunayoitaka watu kutofautiana mawazo na mitazamo. Siyo one size fit all.
 
Ikiwa wenye dhambi tu wakitubu tena hata mmoja tu inakua sherehe mbinguni vipi shetani atapoamua kuwa miongoni mwa waliotubu huko mbinguni kutakuwaje?

Hii falsafa inatufundisha nini? Mfumo wa vyama vingi umeanza juzi kiasi ambacho wengi wa wapinzani walikua CCM msipende kuhukumu ilhali nanyi mna dhambi!! Kama mbinguni hata wenye dhambi watubuo hufanyika sherehe vipi huko CDM? Vipi habari za akina sauli kuwa wainjilisti?

Hii hoja yako inasikitisha!!!

Pole kwani najua nilichosema kinakuumiza. Vumilia tu ndio demokrasia. Huyo niliyemjibu ni wale wanaopotosha kutaka kuonyesha cdm leo iko jinsi ilivyo kwa sababu ya Lowassa.

Sasa ili kutaka kumuonyesha Lowassa ni wa kawaida sana nimemwambia Lowassa arudi ccm ili cdm ife.

Halafu turudi kwenye uhalisia, Lowassa alitakiwa kuwa mwanachama wa kawaida na sio kuwa mgombea wa cdm wakati hakuwahi amekitumikia chama wala kujua itikadi yake. Nafasi nyeti kama ile ilipaswa kupewa mtu anayekifahamu chama kwa undani.

Kibaya zaidi wakati ule wa kampeni alikuwa mgonjwa na hakuweza kufanya kampeni nchi nzima kwa ufanisi. Naomba univumilie sana kamanda mwenzangu, ukweli unaumiza na mimi nafahamu lakini nivumilie tu.
 
Kwa hiyo baada ya katiba mpya Zanzibar CUF wamepata nn na wana nini sasa.

Nimesoma naona kilichopo ktk habari hii ya Kubenea ni kujaribu kutongoza watu ambao wana fikra na wameshaelewa ukweli.

Lowassa alienda kutetea maslahi yake full stop.

EL sio mpinzani na hamjawahi kuwa mpinzani.

Si akapande daladala za gongo la mboto ili aendelee kupata wafuasi kama wkt ule wa kampeni.

Maigizo ni kitu cha ajabu sana ktk uhalisia.

Tuna bahati magazeti ya kubenea yamefungiwa angeanza story zake za kutunga uongo uongo tu..

Kubenea maslahi..
 
Makamanda mnahaha. Mbowe hathubutu kumfukuza Lowasa kamwe.

Anyway naona unajaribu kuniprovoke kitu ambacho nina uelewa nacho na wewe nakumudu sana kwenye hoja za aina zote. Subiri wenye uelewa wako ndio utawavuta kwenye hiyo corner ya kichovu. Nina uelewa mpana, najua wakati gani una hoja na wakati gani unaleta utoto.
 
Siamini sana hii story kama imeandikwa SK, nahisi amelishwa maneno. Na muktadha wa andiko hauna mashiko, chama hakiwezi kujikita kwenye kususia na kutaka suluhisho la mezani wakati kinacho daiwa kuwakwanza ni vitendo vya kukiuka katiba na sheria tulizokubaliana kama taifa.

Nilitegemea CHADEMA waonyeshe kutokubaliana na hali hiyo kisheria mahakamani. Ningekubaliana na andiko hilo endapo utaratibu wa kisheria ungekuwa umeshindwa kutoa suluhu. Ni rubbish...
 
Kwahiyo unadhani Lowasa kaenda kuongea na Magufuli kuhusu Serikali ya Kitaifa au Magufuli aruhusu siasa shindani za kukosoana?

Hahaha.... Poor you.
Lowasa kaenda kwa ajili ya maslahi yake binafsi. Hutu kubenea ni mpuuzi na mpika story.

Bora mkuu umewachana laivu..

Washenzi kabisa hawa.

Watu wamebomolewa makazi anaenda kusifu ujinga ili biashara zake zisisumbuliwe..

EL hajawahi kuwa mpinzani
 
Back
Top Bottom