Kubemendwa kupo????

Pdidy

JF-Expert Member
Nov 22, 2007
50,956
22,144
Kubemenda!




(Miezi saba sasa kubemendwa kupo wapi?)​
SWALI:
Shalom mtumishi wa MUNGU!
Ni matumaini yangu kuwa wewe na familia mnaendelea vizuri.
Sisi pia BWANA anaendelea kututunza na kutufanikisha ktk yote.
Kama ambavyo nimewahi kusema awali kuwa nimekuwa msomaji sana wa blog yenu na imekuwa shule nzuri kwangu kama ambavyo naamini wengi wamenufaika nayo.
Juzi nilisoma comment ya mtu mmoja ambaye alikuwa ana criticize kunena kwa lugha wakati wa tendo la ndoa; nilifurahia sana jibu lako kwani MUNGU anahusika sana na tendo hilo.
Sasa leo nina concern ambayo najua mtanisaidia kwa sababu ya uzoefu wako kama watu mliotangulia ktk kuwa wazazi.
Kuna hili suala linaloitwa 'kubemenda' mtoto, watu wanadai kuwa sperms huwa zinaleta madhara kwenye maziwa ya mama na kumdhoofisha mtoto kiafya na wengine wanasema ukimshika mtoto baada ya sex pia ina madhara.
Tunaomba uzoefu wenu watumishi ktk hili kwani nimewahi kusoma article ya mtu mmoja kwenye mtandao ambaye alijiita daktari na kusema hakuna kitu kama hicho ni imani tu.
MAY GOD RICHLY
BLESS YOU!
JIBU:
Asante sana kwa swali zuri ambalo naamini si geni sana kwa wanandoa wapya katika jamii za kitanzania.
Kama alivyosoma kwenye article ya huyo Daktari ni kweli suala la Kubemenda ni imani potofu (myth) na hakuna uhusiano wa sperms na maziwa ya mama katika kudhoofisha afya ya mtoto; iwe kwa kushirikiana tendo la ndoa au kumshika mtoto baada ya sex.
Je, nini maana ya kubemenda mtoto?
Kwanza hii imani potofu inaeleza kwamba kubemenda mtoto ni pale wanandoa wanapojihusisha na tendo la ndoa baada ya mtoto Kuzaliwa (pale mke anapokuwa tayari kiafya kwa tendo la ndoa baada ya kujifungua) kwa maana kwamba sperms huharibu maziwa ambayo mtoto ananyonya, si kweli hakuna uhusiano wowote kati ya maziwa ya mama na sperms katika kuathiri afya ya mtoto.
Pili kubemenda mtoto ni kitendo cha wanandoa kujihusisha na tendo la ndoa na mke kushika mimba miezi mwili tu au mitatu tu baada ya kujifungua na kupelekea kuzaa mtoto mwingine baada ya mwaka na matokeo yake mtoto aliyetangulia Kuzaliwa huwa dhaifu kiafya (huchelewa kutembea) na huitwa ni mtoto ambaye amebemendwa, kitu ambacho ni imani potofu kwani kuna wanandoa wengi tu wamezaa watoto waliopishana mwaka na wote wana afya njema kabisa.
Tatu kubemenda ni kitendo cha mwanandoa mmoja kutoka nje ya ndoa (sex) na akirudi ndani huendelea na tendo la ndoa na matokeo yake mtoto wa ndani ya ndoa huwa dhaifu, pia ni imani potofu hakuna kitu kama hicho.
Je, Biblia inasema nini kuhusu tendo la ndoa baada ya kujifungua.
Ndiyo kuna andiko (Mambo ya Walawi 12:1-5) linalotaja lini mwanamke ajihusishe na tendo la ndoa baada ya kujifungua na si hivyo tu bali ni wakati gani mtoto wa kiume atahiriwe.
Hata hivyo sheria hii ni moja ya sheria na maagano 6 ambayo Mungu alitoa kwa watu tofauti kwa wakati maalumu na leo wayahudi hufuata zaidi huo utaratibu kwetu sisi Kristo amemaliza yote msalabani na jambo la msingi ni kufuata ushauri wa kitaalamu ambao ni wiki sita baada ya kujifungua.
Je, kuna ukweli wowote kuhusiana na hii imani potofu
Iwe wanandoa kujihusisha na tendo la ndoa baada ya mtoto Kuzaliwa au kuzaa mwingine baada ya mwaka au hata kutoka nje hakuna uhusiano na mtoto aliyezaliwa kama suala la usafi na lishe bora litazingatiwa kwa mtoto anayehusika.
Je, kulikoni mababu zetu wakaweka imani kama hiyo kwa wanandoa?
Kama zilivyo imani zingine potofu kama vile mwanamke mjamzito kutokula mayai mababu zetu walikuwa na somo ndani yake, inawezekana walitaka kuhakikisha wanandoa wanashiriki vizuri katika kulea mtoto kwa pamoja bila kupendekeza tabia za uchafu na kujirusha nje na ndani ya ndoa bila utaratibu.
Pia labda mababu zetu walihofia kitendo cha mwanamke kutoa maziwa (chuluzika) wakati wa tendo la ndoa hasa anapofika kileleni (tangu akifungue hadi miezi 8 hivi) na wakawa wanahofia kinaweza kuathiri kiwango cha chakula cha mtoto hivyo ili kuzuia ni kutunga imani (potofu) kwamba mtoto ataathirika kwa mke na mume kushiriki tendo la ndoa.
Je, ili mtoto asionekane amebemendwa wanandoa wanahitaji kufanya kitu gani?
Ni vizuri kufahamu kwamba hakuna uhusiano wa sperms kuharibu maziwa ya mama wakati wa kumnyonyesha mtoto hivyo wanandoa kushiriki tendo la ndoa halina uhusiano wowote na mtoto kuwa na afya mbaya kiasi cha kuchelewa kutembea.
Mtoto anahitaji watoto chakula bora chenye viini-lishe vyote vinavyohitajika ili kukua vizuri pia mama anahitaji kujiweka mazingira safi (kuwa msafi) wakati ananyonyesha, ahakikishe anasafisha chuchu zake na mikono yake au kuzingatia usafi kimwili kabla ya kumnyonyesha mtoto iwe baada ya sex au muda wowote.
Ni jukumu la baba na mama wa mtoto kuhakikisha wanatumia muda wao kuhakikisha mtoto anapata lishe bora na mahitaji yote ya msingi ya mtoto ili kukua na kuwa na afya njema na si kujinyima kujihusisha na tendo la ndoa wakihofia mtoto kuonekana amebemendwa.
Pia suala la usafi wa mazingira ya mtoto anapoishi (vyombo vya kutumia kwa chakula cha mtoto, usafi wa mwili wa mtoto na mama na baba pia) ni muhimu sana kwani baada ya tendo la ndoa ni muhimu kwa mume na mke kuhakikisha wanakuwa safi tena bila kujihusisha na kumnyonyesha mtoto huku hawajanawa au kuoga.
NB:
Suala la kubemenda (binafsi naweza kuita ni utapiamlo au kwashakoo kingereza- Kwashiorkor) huzungumzwa sana na jamii za “mtanzania wa kawaida” huwezi kusikia katika nchi zilizoendelea na watu ambao wameenda shule na wanafuata misingi ya afya na uzazi katika kulea watoto wao na pia mke na mume kuwa karibu kimapenzi.
Huwezi kusikia takataka za neno kubemenda katika nchi zilizoendelea kama Canada, Sweden, Australia, Ujerumani nk why? Ni traditions (Myth).


FRM
MBILINYI.L
 
Ila hii picha ya mtoto uloweka mkuu,halafu hayo maneno huko chini nadhani pia haki ya mtoto imevunjwa hapo...rekebisha,
 
Mie sijafahamu ok wazazi ndio wanajihusisha na tendo la ndoa baada ya mtoto Kuzaliwa sasa inamhusu vipi mtoto? kwanini wakaita kumbemenda mtoto? This is very new to me honestly... I am just curios ...what do they normally do? throw a party or something like that?
 
Je, Biblia inasema nini kuhusu tendo la ndoa baada ya kujifungua.
Ndiyo kuna andiko (Mambo ya Walawi 12:1-5) linalotaja lini mwanamke ajihusishe na tendo la ndoa baada ya kujifungua na si hivyo tu bali ni wakati gani mtoto wa kiume atahiriwe.
Hata hivyo sheria hii ni moja ya sheria na maagano 6 ambayo Mungu alitoa kwa watu tofauti kwa wakati maalumu na leo wayahudi hufuata zaidi huo utaratibu kwetu sisi Kristo amemaliza yote msalabani na jambo la msingi ni kufuata ushauri wa kitaalamu ambao ni wiki sita baada ya kujifungu.
Is this true? hamfati imeendikwa nini kwenye Bible kwa sababu Jesus amemaliza yote msalabani?.. hawa wataalamu wamekuja lini..Ok guys no disrespect intended but I dont understand how could u ignore what GOD has written and follow what man has right?
 
Hana iana kijana ukiwa na maswali muwashe anajibu kama anaongea na yesu.....
 
Back
Top Bottom