Mtu Akichagua kukuona sio wa Thamani kwake hata Ufanye nn Bado wewe sio wathamani kwake.
No Call, No Sms Kubali kua Hakuitaji na Ujipe Tumaini kua Maisha yanaendelea, nilijenga mpaka nyumba Ili nimpe chumba awe anachukua Kodi lakini aliniacha kwa Dharau na nyodo kibao.
Niilijifunza kukubali kukataliwa, Hiyo nyumba Imekua kumbukumbu yangu ya Upendo kwake. Nilikua nampenda sana Tena sana, nimejifunza mwanadamu ukimpenda anakudharau.
Nilimpenda sana mpaka nilikua kama mjinga kwake Dharau zilizidi ananiblock Kila nikimtafuta kwa namba ngeni anablock. Nilijipa Moyo kua Yatapita tu na nitamsahau.
Upaswi kumpenda mtu sana. Hata siku Moja usimpende mtu sana utateseka. Mtamani ila usimpende maana Binadamu unapompenda yeye anakuletea Dharau.
Nilidharaulika sana.Ktk Maisha usiombe Kumpenda mtu.
Miongoni mwa jambo Baya Ktk Maisha ni kumpenda mtu na yeye asikupende. Utaona Kila Dharau ambazo ujawai ziona mtu anakutazama kama Kinyesi au Funza wa Chooni, Binadamu sio Poa ni Bora umpende Hata mnyama ataelewa Upendo wako ila sio mwanadamu ukimpenda nyodo na dharau atakazokuonyesha.