Kuanzia leo nimeamua kuachana na kushabikia siasa

ina hitaji jicho pevu kuni elewa nilicho kipost hapo juu..watanzania tume logwa.
 
ndio hivyo tena huto niona naside na upande wowote ule nyie endeleeni na kujipa moyo wakati wanasiasa wote ni familia moja wana tuzuga tu.

Wewe ni magamba uliyeumizwa na msimamo wa Ukawa kuhusu kuwajibishwa kwa mawaziri, Katibu Mkuu na wote waliohusika. Unakuja na propaganda ya kitoto
 
Siasa ni Sayansi; si kama wapumbavu wanavyofikiri ni mchezo wa kijinga; bali unataka werevu kuliko Nyoka na kinyonga !
 
mtoa mada unaakili km yakwangu wakati niko chekechea ndo nilkua nafikili kwa style hio, poor argumement and poor thnkng
 
Mbowe ni very strategic. Kama sio yeye mngeona issue ikipotea kwa ushauri wa Chenge yule mwizi mkubwa
Zitto nae alikosea sana kutaka ushauri wa chenge uende kote .Sikujua nia yake ila nilipata kichefuchefu cha ghafla.Na hii ilishawapa advantage ccm.
 
Mbowe ni very strategic. Kama sio yeye mngeona issue ikipotea kwa ushauri wa Chenge yule mwizi mkubwa
Zitto nae alikosea sana kutaka ushauri wa chenge uende kote .Sikujua nia yake ila nilipata kichefuchefu cha ghafla.Na hii ilishawapa advantage ccm.
 
Kipi kimebadilika katika mapendekezo?

Kwangu mie wakifanikiwa kutaifisha huo mtambo ndo reward tosha.

Siasa haishabikiwi bali unajihusisha nayo maana maisha yetu yanazungukwa na siasa hata kama hautaishabikia
waombe ushauri kwa laigwenan lowassa, mtu wa maamusi ngumu jinsi alivyorejesa dawasa mkononi kwa umma na kuwaonyesha njia nyeupe wawekezaji
wezi kimoja.
 
Zitto nae alikosea sana kutaka ushauri wa chenge uende kote .Sikujua nia yake ila nilipata kichefuchefu cha ghafla.Na hii ilishawapa advantage ccm.


Wewe siku nyingi unachuki binafsi na zitto.....

Tunataka askofu Kilaini nae awajibishwe kwa kudhalilisha ukristo wetu
 
Pole sana mkuu, unajua si kila wakati kuwe na kutofautiana, ebu tujipe muda tuone kama mapendekezo yatafanyiwa kazi. Kikatiba si kila mtu anaweza kuwajibishwa na Bunge
 
Pasco alitoa thread kuhusu ignorance ya Watanzania... akachambuliwa, kukejeliwa, kukashifiwa na kupewa kila aina ya mzaha wa kuchukiza! Lakini ukweli unabaki pale pale kwamba wengi wetu tu ignorant bali ni mazuzu!

Pasco huyu tena pamoja faizaFox walitamka kabla kwamba hakuna atakayjiudhuru... mazuzu ya Kitanzania kama kawaida yetu tuaendeleza uzuzu na kukejeli!
OPERA MINI amesusa kushabiki siasa... Sababu alizotoa Opera ndizo zilinifanya niishiwe hata hamu ya kuendelea kufuatilia mijadala ya hapa JF... niseme tu kwamba mara baada ya kusomwa kile kilichoitwa ni kamati ya maridhiano, comepletely nikawa down haijapata kutokea! Hata hivyo, pamoja na sababu alizotoa Opera hapa, bado mazuzu ya Kitanzania tunaendelea kukejeli huku tukipiga shangwa na vigelegle huku nikijiuliza hivi hawa mazuzu wenzangu wanashangilia nini hasa!!! Wanashangilia kutimia kwa utabiri wa FaizaFox na Pasco kwamba hakuna atakayejiuzulu au tuna-prove uzuzu wetu ambao ulisemwa na Pasco???!!

Narudia tena... hivi mazuzu wenzangu mnashangilia nini hasa? Kiongozi mzembe kuliko wote kwenye serikali ya Jakaya ni Pinda! Zitto, Mbowe na wenzao, wamekutanishwa kwenye kikao tusichokijua na huko kunyweshwa maji ya bendera ya CCM kutoka kwa Brain Tankers wa CCM, wanarudi huko kauli tofauti na ile ya awali ya kumtaka Pinda ajiuzulu! Mazuzu yenzangu yanashangilia huku yakipiga vigelegele huku yakisahau kabisa kwamba Pinda, Mtendaji Mkuu wa Serikali, anabaki clean... tumeshindwa angalau kutoa nafasi kwa JK ya kumuangilia Pinda na kuchukua maamuzi anayoona yanafaa dhidi yake! Hakuna shaka kwamba JK amembeba Pinda kwa miaka mingi sasa... lakini kama sasa alisema enough is enough baada ya Pinda tena kukutwa kati kati ya tuhuma za uzembe;enough is enough ya JK kashaachana nayo kwavile Pinda "ameshasamehewa!"

Hivi nyie mazuzu wenzangu mnadhani ni nini CCM na JK walikuwa wanakitaka zaidi ya kumnusuru Pinda?? Mazuzu wenzangu yanafurahi kwa sababu moja tu... "Muhongo amepigwa chini"!! Kwa mazuzu wenzangu, kuchinjiwa baharini kwa Muhongo kunatosha kabisa hata kama wengine wangeachwa huru!! WHY? Sidhani kama kuna mwenye sababu ya msingi zaidi ya zile sababu za hovyo hovyo kwamba Muhongo ana dharau, jeuri, na mambo mengine kama hayo! Mtu anaweza kujiuliza, hivi unakerwa vipi na dharau au jeuri ya mtu ambae mnaishi kwenye dunia mbili tofauti? Yaani dharau anayoletewa Mnyika, au labda Mbowe, au labda Zitto na wengine kama hao, inakuja kumkereketa aishie Buguruni Malapa huku akiwa hana access yoyote na hayo... kama sio uzuzu ni nini?? Yaanii Muhongo kwavile amekuwa mpiga mashuti live, huku akiwa achagui nani wa kumpa ili mradi tu aliyepewa anastahili mashuti husika kama walivyopewa akina Mengi... basi tena, ili mradi Muhongo anachinjiwa baharini, it's enough hata kama mzembe namba moja anaachiwa!!!

Patamu zaidi, kuondolewa kwa Muhongo kumo mikononi mwa JK... yale ya awali kwamba bunge limuwajibishe limegeuka na kuwa la mamlaka husika liangalie na kuchukua hatua stahiki! Niwakumbushe mazuzu wenzangu kwamba JK halazimiki kufuata ushauri wa mtu yeyote yule ikiwa pamoja na huu! Watendaji wake katika chama wakiwa wanaongozwa na Kinana na hatimae NEC ya CCM ilishawahi kumshauri JK kuwavhukulia hatua wale ambao walifahamika kama mawaziri mizigo! Hata hivyo, JK hakuchukua ushauri huo kwa sababu, pamoja na mambo mengine, halazimiki kufuata ushauri wa yeyote!! Hata kama inachukiza, naombea na hili JK afanye hivyo hivyo ili uzuzu wetu udhihirike bayana!!

Kutokana na uzuzu wetu tumeshindwa kabisa kuona nafasi ya Gavana wa Benki Kuu! Hili faizaFox alilielezea! Nami nikawaelezea wadau ni namna ganii hata yule Teller wa kawaida kabisa tunayemkuta kwenye hizi benki zetu jinsi alivyo na power kubwa kuliko mtu mwingine yeyote yule katika kufanya maamuzi ama transaction fulani ilipo mbele yake ilipwe au isilipwe!

Muundo wa benki ulivyo, among the banking staffs, uki-exclude supporting staffs, Teller ndie mwenye daraja la chini kuliko wote!! Lakini pamoja na kwamba yeye ndie mwenye rank ndogo zaidi kuliko wote, lakini yeye ndie mwenye maamuzi ya mwisho kabisa katika kulipa! Hata kama Branch Manager amehidhinisha kulipa, kama hajajiridhisha ikiwa transaction ni genuine; Teller anao uwezo wa kukataa na usimfanye chochote! Hata kama iliyopo mbele yake ni cheki yenye mihuli ya Ikulu, PCCB, TISS, n.k, n.k n.k, bado Teller anaweza kukataa kulipa provided ana mashaka na transaction husika! Huyu ni Teller mpuuzi puuzi tu anayelipwa laki 6 kwa mwezi huku akiishi Buguruni lakini oneni alivyopewa maguvu ya kutisha katika suala zima la kuamua kufanya malipo! Sasa ikiwa Teller tu ana maguvu yote hayo... what about Gavana wa Benki Kuu? Muangalieni Zitto alivyokuwa anafanya jitihada za kumuonesha Ndulu asivyo na hatia!! Kivipi asiwe na hatia wakati pesa zilikuwa chini yake?

Ndulu alikuwa anatakiwa kufanya one of the two! Ama kugoma kabisa kuhidhinisha kutolewa kwa fedha za Escrow au, ikiwa alikuwa analazimishwa na mamlaka zilizo juu yake basi alitakiwa kuachia ngazi ili dhambi hiyo ifanywe na mwingine na sio yeye! Hata hivyo, Ndulu aka-opt kuinda unga wake in exchange of acceptable decisions.

Hata hivyo, mazuzu wenzangu hatulioni hili na kubaki tukipiga makofi wakati kila kitu tupo wazi!!! Mwenye akili timamu wala hakosi kufahamu kwamba PAC iliyokuwa inawataka ni Maswi na Muhongo kwavile Muhongo na Maswi wamekuwa kwenye mgogoro n baadhi ya members wa hii kamati.... Kutokana na hilo, PAC walikuwa tayari wote wasionekane wana hatia provided Muhongo na Maswi wanachinjiwa baharini!!

Prof. CV yake iko vizuri. Ila ukiangalia anavyotoa majibu yake kwa umma hana sifa za uongozi hasa siasa, labda utendaji zaidi. Wanamtwara watakumbuka walishawahi kuitwa CHURA,wafanyabiashara wa Kitanzania wamewahi kuitwa Madalali wenye uwezo wa kuuza Juice tu. Kiukweli hakufaa kuwa mtendaji ambae ni political figure, alifaa kuwa ni mtendaji wa taasis ambazo ziko Active nje na siasa!
 
Last edited by a moderator:
Prof. CV yake iko vizuri. Ila ukiangalia anavyotoa majibu yake kwa umma hana sifa za uongozi hasa siasa, labda utendaji zaidi. Wanamtwara watakumbuka walishawahi kuitwa CHURA,wafanyabiashara wa Kitanzania wamewahi kuitwa Madalali wenye uwezo wa kuuza Juice tu. Kiukweli hakufaa kuwa mtendaji ambae ni political figure, alifaa kuwa ni mtendaji wa taasis ambazo ziko Active nje na siasa!
Nakubaliana na wewe na hata mimi nimeshawahi kulizingumzia hili la Muhongo la kutokuwa na diplomasia ya kuongea lakini kwa upande wangu, ni bora ya kiongozi msema hvyo lakini anatekeleza wajibu wake kuliko muongeaji mwenye maneno matamu hata wakati mwingine kufikia kulia kama Pinda huku utendaji ukiwa ni wa hovyo hovyo!!!
 
Nakubaliana na wewe na hata mimi nimeshawahi kulizingumzia hili la Muhongo la kutokuwa na diplomasia ya kuongea lakini kwa upande wangu, ni bora ya kiongozi msema hvyo lakini anatekeleza wajibu wake kuliko muongeaji mwenye maneno matamu hata wakati mwingine kufikia kulia kama Pinda huku utendaji ukiwa ni wa hovyo hovyo!!!

halafu leo huyo pinda ana onekana msafi kisa kamati ya maridhiano wakati madudu yote yanayo tokea leo ni kutokana na uronya ronya wake ,
 
Wewe ni magamba uliyeumizwa na msimamo wa Ukawa kuhusu kuwajibishwa kwa mawaziri, Katibu Mkuu na wote waliohusika. Unakuja na propaganda ya kitoto

ongea vyote uwezavyo wewe utabakia kua mjinga wa siasa usio waelewa wana siasa.
 
Wadau nasikitika kusema naachana na kushabikia wana siasa,

nilio waamini hawa aminiki tena.

nafanya yangu kimpango wangu

chadema niliipenda sana but ndio hivyo tena yaliyo tokea bungeni leo hii ni ujumbe tosha sana kwangu.

Nadhani wadau wamecomment vizuri, siasa haihitaji watu wa matukio, siasa ni maisha ya kila siku, sasa wewe kama unaenda na matukio, endelea na maisha mengine, kwa upande wa siasa wewe ni MZIGO
 
Siasa waachie wanasiasa bro, kulikua nz ugumu gani kusema pinda z
achomoke? eti kamati ya maridhiano , Upuuzi mtupu!
 
Back
Top Bottom