Hivi kweli nyie watu wa TPA mtauweza ushindani kweli!? Nasikia mtu akiomba invoice za kulipia mzigo saa nyingine zinaweza kutoka baada ya masaa 48 (arobaini na nane)! Huu sio utani wala uzushi bali ni kweli.
Sasa mnadhani kuna Mzambia, Mmalawi au Mkongo achana na sisi wenyeji atakayekubali kuishi hotelini siku mbili za ziada kwa ajili ya kusubiria invoice ili alipie na saa nyingine kupelekea gharama za ziada (storage)!
Bado mnasuasua sana na haya mambo wateja wa bandari ya Dar es Salaam wanayajua vizuri.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.