Kuangushwa kwa Yusuph Kikwete ni kura ya maoni kwa Jakaya Kikwete?

Tikerra

JF-Expert Member
Sep 3, 2008
1,702
146
Jumuiya ya Wazazi mkoa wa Pwani imefanya uchaguzi wa ngazi ya mkoa.Katika uchaguzi huo ambao ulifanyika Kibaha,Yusuph Kikwete ambaye ni mpwa wa Rais Jakaya Kikwete, alibwagwa vibaya na John Machemba, kwa kuambulia kura 82 tu ya kura 302 zilizopigwa.Labda wote tujiulize swali hili, kubwagwa huku kwa Yusuph kuna maana gani hasa?Kwangu mimi kuna maana moja tu,hii ni kura ya maoni kwa Kikwete binafsi na Chama cha Mapinduzi.Kama hoja za msingi ambazo wananchi zina wakera hazitatafutiwa ufumbuzi, Kikwete kushinda 2010 itakuwa kioja.Kazi kwako Kikwete.
 
...Tatizo letu wabongo ndio hilo huenda huyo Yusuph alidhani akitumia surname ya Kikwete inawezas kumpa chati kumbe ndio anaharibu kabisa...Tikerra, hiyo yawezekana ikawa ni ishara ya muungwana kutimuliwa vumbi jina limechuja hilo!!!!!!!!!
 
Jamani huyo Yusuph Kikwete alikwenda kwenye uchaguzi akiwa na ajenda na sera zake, kamwe sera na ajenda zake haziwezi kuwakilisha ajenda na sera za JK. Kama umemchoka JK ni wewe lakini si vyema kumhusisha yeye JK na ndugu au uzao wake! mambo mengine naona kama yanaboa sasa! JK ahukumiwe kwa matendo yake na si matendo ya ndugu au jamaa zake au marafiki!
 
Jumuiya ya Wazazi mkoa wa Pwani imefanya uchaguzi wa ngazi ya mkoa.Katika uchaguzi huo ambao ulifanyika Kibaha,Yusuph Kikwete ambaye ni mpwa wa Rais Jakaya Kikwete, alibwagwa vibaya na John Machemba, kwa kuambulia kura 82 tu ya kura 302 zilizopigwa.Labda wote tujiulize swali hili, kubwagwa huku kwa Yusuph kuna maana gani hasa?Kwangu mimi kuna maana moja tu,hii ni kura ya maoni kwa Kikwete binafsi na Chama cha Mapinduzi.Kama hoja za msingi ambazo wananchi zina wakera hazitatafutiwa ufumbuzi, Kikwete kushinda 2010 itakuwa kioja.Kazi kwako Kikwete.

weak point, poor argumentation! hakuna hata cha kujadili maana kila kitu ni out of point.
 
Wabongo bwana!Mlitaka achaguliwe au apitishwe tu kwa vile ana surname ya Kikwete.
Watu siku hizi si mambumbumbu kama zamani watu wanaangalia ufanisi wa kazi na sera zinazo tekelezeka wewe unakuja na sera za kufikirika utaambulia patupu ndo kama huyo.
 
Mtoa hoja ana point.Ni vigumu,kwa mfano,kuzungumzia mafaniko ya kisiasa ya Ridhiwani Kikwete pasipo kumhusisha baba yake.Na kwa namna hiyo hiyo,kushindwa kwa Yusuph hakuwezi kuzungumzwa pasipo kumhusisha mpwawe,regardless ukweli kwamba uamuzi wa kugombea ulikuwa ni wa mtu binafsi.Yayumkinika kuamini kwamba laiti nyota ya JK ingekuwa inang'aa kwa nguvu miongoni mwa wapiga kura katika uchaguzi huo basi ingemsaidia mpwawe kushinda pia.Tusijifanye wagumu kuelewa kwamba chuguzi nyingi,na sio za Afrika pekee,haiba na jina la mgombea ni muhimu zaidi pengine zaidi ya sera zake.I agree na mtoa hoja,hii ni warning message kwa JK.
 
Mambo sio "straight forward" kama unavyodhani,kaa chini na utafakari.
 
Yaani umeonesha ni kwa kiwango kipi fikra zako zinapofikia kikomo. Kibaha ni sehemu ndogo sana ya Jamhuri ya Muungano wa Tz. achilia mbali YK kushindwa vibaya katika uchaguzi huo, hata ingekuwa ni JK mwenyewe kagombea nafasi hiyo huko kibaha(kama inawezekana) na kushindwa hivyo bado kushindwa kibaha isingeweza kuwa ni kipimo cha kuanguka kwake katika uchaguzi wa kitaifa.
Japo siwezi kusema kwamba JK atashinda 2010, lakini kibaha si kipimo.
 
By the way akina Kikwete wanachukua Sir names toka kwa mama? au baba yake yusuf naye ni Kikwete kama alivyo baba wa mama yake Yusuf (dada yake Jakaya)?
 
Nziku, polepole mzee! Out of point kwa kigezo kipi? mbona wengine wamejadili?

Jibaba,
unapotoa hitimisho la jumla (generalization) lazima uwe umefikia vigezo vya msingi japo kwa kugusia tu. ona yafuatayo:-
1) Uchaguzi ulikuwa wa Jumuiya ya Wazazi ya CCM wilaya ya Kibaha (sehemu ndogo ya CCM).
2) Sababu za kushindwa huyo Bwana ndani ya chama chake hazijasemwa.
3) Kuwa na jina la Kikwete si tiketi ya kuchaguliwa
4) Kibaha haiwezi kuwa sample ya wana-CCM au watanzania wote tena wapiga kura walikuwa chini ya 500.

Maneno niliyoyapiga yapo chini ya kiwango cha kujadiiliwa ni "Kwangu mimi kuna maana moja tu,hii ni kura ya maoni kwa Kikwete binafsi na Chama cha Mapinduzi".

Jibaba unakubaliana na haya? kwamba kushindwa kwa huyo mpwa wa Kikwete kunamaana moja tu nayo ndiyo hiyo?
 
jumuiya ya wazazi mkoa wa pwani imefanya uchaguzi wa ngazi ya mkoa.katika uchaguzi huo ambao ulifanyika kibaha,yusuph kikwete ambaye ni mpwa wa rais jakaya kikwete, alibwagwa vibaya na john machemba, kwa kuambulia kura 82 tu ya kura 302 zilizopigwa.labda wote tujiulize swali hili, kubwagwa huku kwa yusuph kuna maana gani hasa?kwangu mimi kuna maana moja tu,hii ni kura ya maoni kwa kikwete binafsi na chama cha mapinduzi.kama hoja za msingi ambazo wananchi zina wakera hazitatafutiwa ufumbuzi, kikwete kushinda 2010 itakuwa kioja.kazi kwako kikwete.

comparing incomparable
 
Jamani huyo Yusuph Kikwete alikwenda kwenye uchaguzi akiwa na ajenda na sera zake, kamwe sera na ajenda zake haziwezi kuwakilisha ajenda na sera za JK. Kama umemchoka JK ni wewe lakini si vyema kumhusisha yeye JK na ndugu au uzao wake! mambo mengine naona kama yanaboa sasa! JK ahukumiwe kwa matendo yake na si matendo ya ndugu au jamaa zake au marafiki!

tuna deal na wanaomzunguka kwanza kwani tumegutuka wanao kamatwa kwa ufisadi ni maswaiba wake na ndugu zake ni anatakiwa aelewe tukiamua kumpa kura yeye tutawamwaga ndugu zake na maswaiba wake kwani inaonekani aanagalie uwezo anaangalia ukaribu.....kama hayuko tayari kufanya kazi bila ndugu na maswhibaas hana haja ya kugombea 2010
 
Tena hana sera na hafai kweli...kazi yake ni kupika majungu tu na kuwatishia watendaji wa wilaya bagamoyo kwa miaka mingi sasa.....watu walishawahi kuhamishwa kwa simu mnaweza mkaamini?ulizeni meneja wa tanesco alihamishwa kwa simu...sasa yuko Mbeya(Kibona).....sababu huyu Yusuph...anatishia hata OCD,Mkuu Wilaya ,Afisa Usalama.....wote wanamuogopa na JK akienda Bagamoyo wakati ule waziri.....huwa anazunguka na Yusuph tuu...hapo anapewa umbea wote....Jamaa (Yusuph)aligombea ujumbe wa NEC akapata......sasa alitaka amalize kwa Mwenyekiti Wazazi Mkoa....heko wajumbe maana namjua sana sana..hafai.....na hana jipya wala mtazamo....nawasilisha.
 
Mtoa hoja ana point.Ni vigumu,kwa mfano,kuzungumzia mafaniko ya kisiasa ya Ridhiwani Kikwete pasipo kumhusisha baba yake.Na kwa namna hiyo hiyo,kushindwa kwa Yusuph hakuwezi kuzungumzwa pasipo kumhusisha mpwawe,regardless ukweli kwamba uamuzi wa kugombea ulikuwa ni wa mtu binafsi.Yayumkinika kuamini kwamba laiti nyota ya JK ingekuwa inang'aa kwa nguvu miongoni mwa wapiga kura katika uchaguzi huo basi ingemsaidia mpwawe kushinda pia.Tusijifanye wagumu kuelewa kwamba chuguzi nyingi,na sio za Afrika pekee,haiba na jina la mgombea ni muhimu zaidi pengine zaidi ya sera zake.I agree na mtoa hoja,hii ni warning message kwa JK.

Na kushindwa kwa Makongoro Nyerere yuko wapi? Mwenyekiti wa CCM Musoma...heheheh....Kama ingekuwa jina linauzika basi angekuwa Rais au Waziri fulani.Huwezi kuchanganya sifa za mzazi na mwanae.
 
Mimi nakubaliana na mtoa hoja kuwa kushindwa kwa nduguye Jakaya kwenye uchaguzi wa TAPA huko Kibaha ni ishara tosha kuwa jina hilo halilipi tena kwenye mambo ya siasa.Performance yake kama Rais ingekuwa ya kururidhisha nadhani huyu Yusuf angeshinda kwani wajumbe wangetegemea kuwa utendaji wake ungekuwa mzuri kama nduguye; lakini kwavile Jakaya amefanya "USANII" miaka yote hii jamaa wakajua na huyu nduguye angekuwa hivyo hivyo!! Kushindwa kwa huyu bwana ni "RED" light kwa muungwana.
 
Mtoa hoja ana point.Ni vigumu,kwa mfano,kuzungumzia mafaniko ya kisiasa ya Ridhiwani Kikwete pasipo kumhusisha baba yake.Na kwa namna hiyo hiyo,kushindwa kwa Yusuph hakuwezi kuzungumzwa pasipo kumhusisha mpwawe,regardless ukweli kwamba uamuzi wa kugombea ulikuwa ni wa mtu binafsi.Yayumkinika kuamini kwamba laiti nyota ya JK ingekuwa inang'aa kwa nguvu miongoni mwa wapiga kura katika uchaguzi huo basi ingemsaidia mpwawe kushinda pia.Tusijifanye wagumu kuelewa kwamba chuguzi nyingi,na sio za Afrika pekee,haiba na jina la mgombea ni muhimu zaidi pengine zaidi ya sera zake.I agree na mtoa hoja,hii ni warning message kwa JK.
Kwa hiyo naye Yusufu alitaka atumie surname ya Kikwete apite? Aaa wapi, watanzania siyo wapumbavu hivyo tena.
 
Si kweli kuanguka kwa Yusuph Kikwete ni kura ya maoni kwa JK. That is too general. Ukweli ni kwamba JK 2010 bado watanzania watamchagua JK japo si kwa sunami!!!! Andika kwenye diary yako ikifika siku ya siku tukumbushane hapa JF. Tuombe uzima.

Tatizo la sisi Watanzania, wengi wa wapiga kura wapo kijijini. Wanateseka sana na maisha lakini bado kisiasa wamelala. Elimu ya Demokrasia na uraia ni ndogo sana kule. Wale wa kijijini wakishaelimika na viongozi wabaya regardless ya chama watokacho hawatachaguliwa tena. Hebu upinzani hata ssm kwenyewe ajitokeze dedicated individual ambaye analeta ilani zinazotekelezeka na ambaye ataisoma ilani ili asije akana tena baada ya uchaguzi kama nanihi na nanihi. Yaani kicheko kwelikweli.

Pia kwa wapinzani kushinda ni lazima kuwe na kiongozi imara wa upinzani ambaye umma wa wapiga kura (ambao wengi si mimi na wewe maana wasomi wengi wanapiga makelele tu hata humu ndani ya Jf lakini hawapigi kura) utamkubali. Kwa kuanzia hebu 2010 wasomi wote mliopo tanzania jiandikisheni kupiga kura na mpige kweli siku ya uchaguzi. You will make a difference!!!!
 
Hapana, inategemea huyo Yusuph Kikwete ni mtu wa namna gani na alijieleza vipi kwa wapiga kura wake.
 
Back
Top Bottom