KOTI la Mpendazoe lamshinda NAPE

Hakuna koti litakalomtosha chadema.. . . . .aluta continua!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!

masihara ayo! Ata la mjumbe wa baraza kuu la Bavicha? Mmh hapana! Una maana kama yeye mti basi mpapai hafai kwa kuni wala mkaa? Siamini!
 
Hivi koti likikushinda linakudhuru vipi, linakuangusha? Misemo ya kibongo mingi kwangu hai make sense.

Anyhow, bomu la Mpendazoe halijawa na devastating, lasting impact kwa Nape, labda amejisikia aibu mbele ya kina Kikwete siku mbili tatu, lakini hakuna atakae dai, kwa mfano, ajiuzulu kwa sababu alitaka kuhama chama. Scandle hazimuangushi mtu Tanzania.

Lakini kikubwa zaidi kuhusu udhaifu wa Nape ni kwamba kwa kweli toka aingie kumekuwa na chaos rather than calmness kwenye chama, kutokana na motormouth yake magazetini, mitandaoni, majukwaani, na mabarabarani. Kazi inamshinda.

Hiyo unayosema "misemo ya kibongo huwa haimake sense" - ni lugha imetumika kwa ufundi, nadhani jamaa anahitaji kupongezwa kwa kutumia "uvaaji wa koti" kufikisha ujumbe wake. mtu akivaa nguo, mfano koti, ambayo tuseme ni several sizes greater, kwanza anakuwa kichekesho. watu hata hawasikilizi anachosema, wanatazama alivyovaa. wakati mwingine watu wa COMEDY wanatumia mbinu hiyo. lakini pia koti kubwa mpaka unaliburuza chini unaweza kulikanyaga na ukaanguka. maana yake umerushiwa jambo ambalo umeshindwa jinsi ya kujibu mapigo vizuri, ukadhurika. hiyo ndio ladha ya lugha. tujivunie lugha yetu ya kiswahili, na tuitumie vizuri kufikisha ujumbe. ndio kukua kwa lugha. ukianza kuidharau kwamba ni "misemo ya kibongo", utapoteza nafasi ya kuiendeleza, labda Kenya wakusaidie kwa faida yao wenyewe.

Nape hakutakiwa kujiingiza kuishambulia CHADEMA. angetakiwa kujipanga vema ili aanzishe kitu na kukimaliza vizuri. mwanasiasa makini harukii mambo wala hakurupuki. anajenga reputation ya kusimamia machache na kuyakamilisha vizuri, badala ya kushika hiki mara kile, na hakuna hata moja unalofanikisha. hiyo ni signature ya JK, na hatumshangai, lakini Nape alitakiwa angalau alete ladha mpya basi.

Na hata kama ni kuishambulia CHADEMA, alitakiwa aende kwa hoja basi, badala ya kufanya personal attacks. yale yale, "simple minds discuss people..." Nape ajipange upya, ajijengee signature ya kwake mwenyewe, na itakayomsaidia na kuleta fresh breath katika CCM, ni signature ya umakini na uhakika
 
Kotiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiii!!hahahah...katika makosa makubwa ambayo jamaa atayajutia daima ni kuanza kazi kwa kuiparamia CDM, alipaswa aanze kwanza kwa kushughulikia vipaumbele vyake na Chama chake baada ya kuzawadiwa hicho cheo (siamini kama kipaumble cha kwanza ilikuwa kuanza kushambulia watu binafsi eg.Dr. Slaa)...Heee..shule tena?!mmh kwani huko India alienda kusoma nini?tujuzane
 
Tueleze endapo kama nchi inamwelekeo sahihi ndugu yangu mpendwa. Je suala la Ufisadi ilikuwa hoja ya nani, na neno fisadi limekuwa likitumiwa na chama gani na kwa nini ndio umekuwa wimbo wa taifa? EPA ulikuwa ni mradi wa nani na umesababisha nini ndani ya mfumo wa maisha ya kila siku ya mtanzania? Msemo wa mapacha watatu ambao wanatakiwa kujiondoa wametokana na mawazo ya watu gani? na sasa yanaendelezwa na nani? Suala la Katiba mpya? Ujenzi wa reli nk!
 
endelea kufurahisha barza.
hayo maneno si mageni kwangu, eti chadema wameibana kila kona ccm, mara chadema wafanya kweli, mara chadema wazoa mamia ya wanachama wa ccm...ikija kwenye uchaguzi chadema chali, tupa kule

You think so, keep thinking until you see it.
 
Hiyo unayosema "misemo ya kibongo huwa haimake sense" - ni lugha imetumika kwa ufundi, nadhani jamaa anahitaji kupongezwa kwa kutumia "uvaaji wa koti" kufikisha ujumbe wake. mtu akivaa nguo, mfano koti, ambayo tuseme ni several sizes greater, kwanza anakuwa kichekesho. watu hata hawasikilizi anachosema, wanatazama alivyovaa. wakati mwingine watu wa COMEDY wanatumia mbinu hiyo. lakini pia koti kubwa mpaka unaliburuza chini unaweza kulikanyaga na ukaanguka. maana yake umerushiwa jambo ambalo umeshindwa jinsi ya kujibu mapigo vizuri, ukadhurika. hiyo ndio ladha ya lugha. tujivunie lugha yetu ya kiswahili, na tuitumie vizuri kufikisha ujumbe. ndio kukua kwa lugha. ukianza kuidharau kwamba ni "misemo ya kibongo", utapoteza nafasi ya kuiendeleza, labda Kenya wakusaidie kwa faida yao wenyewe.

Nape hakutakiwa kujiingiza kuishambulia CHADEMA. angetakiwa kujipanga vema ili aanzishe kitu na kukimaliza vizuri. mwanasiasa makini harukii mambo wala hakurupuki. anajenga reputation ya kusimamia machache na kuyakamilisha vizuri, badala ya kushika hiki mara kile, na hakuna hata moja unalofanikisha. hiyo ni signature ya JK, na hatumshangai, lakini Nape alitakiwa angalau alete ladha mpya basi.

Na hata kama ni kuishambulia CHADEMA, alitakiwa aende kwa hoja basi, badala ya kufanya personal attacks. yale yale, "simple minds discuss people..." Nape ajipange upya, ajijengee signature ya kwake mwenyewe, na itakayomsaidia na kuleta fresh breath katika CCM, ni signature ya umakini na uhakika

Great Thinker. Well said:frusty::frusty::frusty::frusty::frusty::frusty:
 
Kotiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiii!!hahahah...katika makosa makubwa ambayo jamaa atayajutia daima ni kuanza kazi kwa kuiparamia CDM, alipaswa aanze kwanza kwa kushughulikia vipaumbele vyake na Chama chake baada ya kuzawadiwa hicho cheo (siamini kama kipaumble cha kwanza ilikuwa kuanza kushambulia watu binafsi eg.Dr. Slaa)...Heee..shule tena?!mmh kwani huko India alienda kusoma nini?tujuzane

Kimyaaaaaaaaaaaaaaaaa. Hasemi tena.
 
KATIBU wa Itikadi na Uenezi wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), Nape Nnauye sasa amebeba “gunia la kokoto” na hajui mahali pa kulitua.

Hadi sasa Nape amejiingiza katika mgongano wa ndani kwa ndani katika chama chake; amepanua wigo wa maadui kwa kuandama anaowaita “watuhumiwa wakuu wa ufisadi;” na anabembea katika malumbano na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA).

Hadi sasa Nape hajui ni jinsi gani anaweza kuisaidia ccm baada ya kuona kila sehemu anapoenda kujisafisha haungwi mkono wa wananchi. Kwa sasa Nape kaamua kukaa kimya baada ya kuona hamna matokeo mazuri ya kukinusuru chama kilichojaa magamba, sasa anajiuliza apotelee wapi ili ccm wenyewe walichuka pesa za wananchi wajisafishe wenyewe.
 
Baada ya Dk Slaa kutuhumiwa kwamba halipi kodi, naomba niwaulize wanamagamba Je Nape, Msekwa, Mukama na Malisa wanalipa Kodi?

Mtupe TIN (Tax Payer Identification Number) za kila mmoja.
 
Hawa jamaa hawajui hata watu ambao hawalipiu kodi,kama mafuta yao yanaingia bila kulipiwa kodi je hao akina Nape watalipa wapi...
 
Hapo sawa.

Binafsi naomba kama kuna mtu wa karibu na Nape humu jamvini basi amshauri huyu dogo arekebishe details fulani kwenye wall yake facebook. Nape kaandika anapenda 'wanawake na wanaume'! Is he really? Inawezekana dogo alitaka kuonesha yeye ni mtu wa watu but kupenda wanawake na wanaume means something else Nape. Unless kweli uko hivyo basi badilisha.
 
Hapo sawa.

Binafsi naomba kama kuna mtu wa karibu na Nape humu jamvini basi amshauri huyu dogo arekebishe details fulani kwenye wall yake facebook. Nape kaandika anapenda 'wanawake na wanaume'! Is he really? Inawezekana dogo alitaka kuonesha yeye ni mtu wa watu but kupenda wanawake na wanaume means something else Nape. Unless kweli uko hivyo basi badilisha.

Kama alivyo andika ndivyo kwanini abadilishe?
 
Nilifanikiwa kuhudhulia pindi mkama alivyokua Musoma ikanibidi niinamishe kichwa maaana waliokuwepo pale walikua ni viongoz wa chama pekee na watoto wa shulu sasa kwa hii hali Nape kasoma alama za nyakati na kuamini huuu mzigo ni mzito...:mod::dance:
 
Kwa sasa Nape Nnauye ni MTUMBA wa kisiasa.

Nafikiri tatizo la huyu Bwana alianza kazi kama kilanja mkuu, hakusubiri kupewa semina elekezi sasa amelikologa na moto anao na hana msaada Baba ake alifariki VISSION yake ni kuongeza maadui ndani na nje ya chama.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom