plan z
JF-Expert Member
- Jun 10, 2019
- 1,381
- 1,414
Ilikuwa asubuhi nzuri sana iliyojaa uchangamfu wa aina yake. Hali ya hewa ilikua rafiki kwa kila mtu, mawingu mazito yalitanda anga zima la jiji la Dar es salaam na kulimeza jua lililokua kero kwa wakazi wengi wa jiji hilo sababu ya joto lake kuwatesa wengi.
Kijimvua laini kilinyesha kila mahali na kuiosha miili ya wahangaikaji wengi wa jiji hilo ambao kwao kuoga lilikuwa jambo la bahati nasibu sababu ya kujali muda.
Ilikua ni jumatatu ya kivutia siku ambayo watu wengi walikua wanawahi mihangaikoni kutafuta ridhiki za kila siku.
Mitaani kote watu walitapakaa kila kona, hawakuijali ile hali ya mvua wengi waliifurahia, si barabarani , kivukoni kwenye madaladala kote watu walijaa, msemo wa mjini cha bure salamu ulithibitika hapo.
Mimi na baba yangu Mzee Kamba tulikua miongoini mwa watu walioijaza mitaa.
Tulikua tunaenda chuoni Baltimore key health kufanya usajili ili nianze mwaka wangu wa kwanza wa masomo chuoni hapo.
Tulitumia usafiri binafsi, namshukuru Mungu kwa kiasi fulani maisha ya wazazi wangu yalikua mazuri kiasi chake walikua na nyumba nne magari matatu ya kutembelea na moja kwa ajili ya kazi za shamba.
Ukubwa wa foleni na umuhimu wa watu kuwahi kazini na mihangaikoni siku ya jumatatu ulitukawiza barabarani, baba yangu Mzee Kamba alitumia muda huo kunipa mawaidha, yale yote niliyopewa na mama nyumbani aliona ni kama hayatoshi. Baba yangu alikua anapenda sana mafanikio barabara nzima maongezi yake yalihusu kutengeneza pesa, habari za wanawake hakutaka kuzisikia hata kidogo, muda wote huo alikua akinihusia kua nikitaka kufaulu masomo yangu vizuri na kupata kazi nzuri ni lazima nifunge zipu yangu na kusahau kila kitu kuhusu wanawake mpaka muda sahihi ukifika, na muda sahihi ni pale nitakapokua nimetimiza ndoto zangu zote.
Tulifika chuoni Baltimore key health, uzuri na mpangilio wa majengo na kila kitu chuoni hapo uliungana na mawaidha ya baba yangu Mzee Kamba kuniongezea motisha. Foleni tuliyoikuta ofisi ya msajili ilinipa nafasi ya kutembea na kuzunguka chuo kizima. Kila nilichokiona chuoni hapo kilinivutia, majengo makubwa ya kisasa na bustani nzuri za maua zilipendezesha sana mazingira ya hapo ilikua ni lazima nifanikiwe, ni lazima niwe daktar sikuona kitu chochote cha kunizuia.
Zamu yetu ya kufanya usajili ilifika, baba yangu Mzee Kamba alinilipia ada na michango yote, taratibu zote na kila kitu kilikamilika.
Nilipewa chumba cha kukaa, chuo kilikua kipya, kilimilikiwa na familia ya Baltimore Woodward kutoka nchini Canada, kwa taratibu zao walizojiwekea ilikua ni lazima wanafuzi wote wakae hostel ili kuzuia matabaka kati ya waliokua nacho na wasiokua nacho.
Baada ya kila kitu kukamilika baba yangu alinikabidhi pesa za matumizi kwa ajili ya mambo mengine pamoja na chakula maana tulikua tunanunua kutoka cafeteria za chuo hata nje ya chuo pia tuliruhusiwa kununua sababu kila mtu alipenda kula chakula anachokitaka.
Wiki moja ilipita usajili na kila kitu kilimalizika. Wanafunzi wote waliwasili tayari, Baltimore key health chuoni masomo yalianza yalikua ni magumu mno kuliko sehemu zote nilizopita awali.
Ma lecture wote walikuwa wazungu, lafudhi zao na kingereza chao orijino vilitutesa sana ilihitajika umakini mkubwa sana kuwaelewa.
Tulikuwa wanafunzi wa kwanza chuoni hapo, wote tulikua wapya kabisa asilimia kubwa tulikua tumetokea kidato cha sita wachache sana walitokea diploma.
Hakukua na wa kwanza wala wa mwisho kama sekondari lakini kila mtu alisoma kwa bidii, hakuna hata mmoja aliyetaka kufeli wala ku supp kila mtu alitaka kupata matokeo mazuri kuwafurahisha wazazi wake.
Nilisoma kwa bidii sana, maneno ya baba yangu yalikua kama kimvuli changu kila muda yalijirudia masikioni mwangu.
Sio yeye peke yake sikutaka kuwaangusha wote pamoja na mama yangu. Nilifanya kila nilichoweza kuhakikisha nafanya vizuri.
Darasani nilishirikiana na kila mtu katika mambo yote ya kitaaluma jambo lililofanya nijulikane na watu wote kwa sababu ya ucheshi wangu pamoja na akili nilizokua nazo.
Kila mara jina la Alfred Kamba lilikuwa miongoni mwa wanafunzi waliofaulu vizuri kwa kupata GPA ya juu kabisa kitu kilichofanya niwe mwanafunzi bora karibu katika kila semista.
Jambo hili lilifanya niwe mtu wa furaha mara kwa mara, kupeleka matokeo mazuri nyumbani lilikua jambo la ufahari na la kujivunia kwangu.
Itaendelea.
Kijimvua laini kilinyesha kila mahali na kuiosha miili ya wahangaikaji wengi wa jiji hilo ambao kwao kuoga lilikuwa jambo la bahati nasibu sababu ya kujali muda.
Ilikua ni jumatatu ya kivutia siku ambayo watu wengi walikua wanawahi mihangaikoni kutafuta ridhiki za kila siku.
Mitaani kote watu walitapakaa kila kona, hawakuijali ile hali ya mvua wengi waliifurahia, si barabarani , kivukoni kwenye madaladala kote watu walijaa, msemo wa mjini cha bure salamu ulithibitika hapo.
Mimi na baba yangu Mzee Kamba tulikua miongoini mwa watu walioijaza mitaa.
Tulikua tunaenda chuoni Baltimore key health kufanya usajili ili nianze mwaka wangu wa kwanza wa masomo chuoni hapo.
Tulitumia usafiri binafsi, namshukuru Mungu kwa kiasi fulani maisha ya wazazi wangu yalikua mazuri kiasi chake walikua na nyumba nne magari matatu ya kutembelea na moja kwa ajili ya kazi za shamba.
Ukubwa wa foleni na umuhimu wa watu kuwahi kazini na mihangaikoni siku ya jumatatu ulitukawiza barabarani, baba yangu Mzee Kamba alitumia muda huo kunipa mawaidha, yale yote niliyopewa na mama nyumbani aliona ni kama hayatoshi. Baba yangu alikua anapenda sana mafanikio barabara nzima maongezi yake yalihusu kutengeneza pesa, habari za wanawake hakutaka kuzisikia hata kidogo, muda wote huo alikua akinihusia kua nikitaka kufaulu masomo yangu vizuri na kupata kazi nzuri ni lazima nifunge zipu yangu na kusahau kila kitu kuhusu wanawake mpaka muda sahihi ukifika, na muda sahihi ni pale nitakapokua nimetimiza ndoto zangu zote.
Tulifika chuoni Baltimore key health, uzuri na mpangilio wa majengo na kila kitu chuoni hapo uliungana na mawaidha ya baba yangu Mzee Kamba kuniongezea motisha. Foleni tuliyoikuta ofisi ya msajili ilinipa nafasi ya kutembea na kuzunguka chuo kizima. Kila nilichokiona chuoni hapo kilinivutia, majengo makubwa ya kisasa na bustani nzuri za maua zilipendezesha sana mazingira ya hapo ilikua ni lazima nifanikiwe, ni lazima niwe daktar sikuona kitu chochote cha kunizuia.
Zamu yetu ya kufanya usajili ilifika, baba yangu Mzee Kamba alinilipia ada na michango yote, taratibu zote na kila kitu kilikamilika.
Nilipewa chumba cha kukaa, chuo kilikua kipya, kilimilikiwa na familia ya Baltimore Woodward kutoka nchini Canada, kwa taratibu zao walizojiwekea ilikua ni lazima wanafuzi wote wakae hostel ili kuzuia matabaka kati ya waliokua nacho na wasiokua nacho.
Baada ya kila kitu kukamilika baba yangu alinikabidhi pesa za matumizi kwa ajili ya mambo mengine pamoja na chakula maana tulikua tunanunua kutoka cafeteria za chuo hata nje ya chuo pia tuliruhusiwa kununua sababu kila mtu alipenda kula chakula anachokitaka.
Wiki moja ilipita usajili na kila kitu kilimalizika. Wanafunzi wote waliwasili tayari, Baltimore key health chuoni masomo yalianza yalikua ni magumu mno kuliko sehemu zote nilizopita awali.
Ma lecture wote walikuwa wazungu, lafudhi zao na kingereza chao orijino vilitutesa sana ilihitajika umakini mkubwa sana kuwaelewa.
Tulikuwa wanafunzi wa kwanza chuoni hapo, wote tulikua wapya kabisa asilimia kubwa tulikua tumetokea kidato cha sita wachache sana walitokea diploma.
Hakukua na wa kwanza wala wa mwisho kama sekondari lakini kila mtu alisoma kwa bidii, hakuna hata mmoja aliyetaka kufeli wala ku supp kila mtu alitaka kupata matokeo mazuri kuwafurahisha wazazi wake.
Nilisoma kwa bidii sana, maneno ya baba yangu yalikua kama kimvuli changu kila muda yalijirudia masikioni mwangu.
Sio yeye peke yake sikutaka kuwaangusha wote pamoja na mama yangu. Nilifanya kila nilichoweza kuhakikisha nafanya vizuri.
Darasani nilishirikiana na kila mtu katika mambo yote ya kitaaluma jambo lililofanya nijulikane na watu wote kwa sababu ya ucheshi wangu pamoja na akili nilizokua nazo.
Kila mara jina la Alfred Kamba lilikuwa miongoni mwa wanafunzi waliofaulu vizuri kwa kupata GPA ya juu kabisa kitu kilichofanya niwe mwanafunzi bora karibu katika kila semista.
Jambo hili lilifanya niwe mtu wa furaha mara kwa mara, kupeleka matokeo mazuri nyumbani lilikua jambo la ufahari na la kujivunia kwangu.
Itaendelea.