Kosa la Kebwe ni lipi?

Kosa la Kebwe ni lipi?

Hawa jamaa kweli wamedhamiria kuinyoosha nchi.

Ni zaidi ya mara tatu nimeshuhudia aina hii ya utumbuaji wa viongozi!

Nilianza zengwe la hivi kule Songwe kwa Chiku Galawa, akaja Kamishina wa Tra, sasa na huyu!

Unaonywa hadharani ili ujirekebishe juu ya utendaji wako wenye mapungufu, kumbe huku memo za kukutumbulia zikiendelea kutembezwa chini ya meza!

Nilichokigundua kwa hao viongozi ni kwamba, ukiona ziara ya mkubwa imekubadikikia, upepo umevurugika, aidha hata kwa watendaji wako wanaokuwajibikia, usijione 'umesevu' ukaanza kujipendekeza kwa maneno ya kimbelembele, kama alivyofanya Mchechu wa NHC kule dodoma kwa kumwita Jpm 'baba' badala ya 'mheshimwa' utakuwa unajidhalilisha tu.

Yakikutokea hayo nuna kabisa, usicheke na mtu, wala kujipendekeza kwa maneno ama kwa vitendo.

Jiandae kupokea walichokipanga kukufanyia.
Kufanya chochote hakibadilishi maamuzi, maana utakuwa umeshachelewa.
 
Mwana wa Adamu alipenda mvinyo wakasema mlevi, Yohana mbatizaji mvazi yake yalikuwa ngozi ya ngamia na chakula chake ilikuwa nzige wa porini wakasema kichaa.
Katika Inchi hii Viongozi wakuu walioko amdarakani na Wastaafu ni walevi sana na wengine wana stroke za kudumu kwa sababu ya pombe lakini bado wanaheshimika na kukubalika. Huyu Mkuu wa mkoa wa Morogoro kilichomtoa madarakani ni ufanisi mdogo katika kuwasimamia viongozi walioko chini yake lakini ni Kiongozi mzoefu na aliyefanya mengi kwa Watanzania. Nafikiri imefika muda amechoka na aliamua kuacha bora liende.
Wanafalsafa husema." Wape maskini mvinyo kidogo wapate kusahau matatizo yao.
Mfalme na asipende sana mvinyo asije akafanya maamuzi yasiyo sahihi."
Du kiongozi naona una mafungu ya biblia moto moto... Naomba unitajie yanatoka vitabu gani ili nitetee gambe langu
 
Back
Top Bottom