Kortini kwa kutaka kumuua Lubuva

Kortini kwa kutaka kumuua Lubuva

Movie hii mwisho wa siku sijui nani stelingi!
Sipati picha kabisa!




Wakili wa Serikali, Hellen Moshi
alidai kati ya Oktoba 23 na Novemba 16, mwaka huu katika maeneo tofauti Dar es Salaam na maeneo mengine nchini, washitakiwa na wengine ambao hawajafika mahakamani, walikula njama za kumuua Jaji Lubuva na familia yake.


Washitakiwa hao, Mwalimu Samwel Gikaro (30) na Mwanasheria Angela Mbonde (32) walifikishwa mahakamani hapo jana na kusomewa mashitaka mbele ya Hakimu Mkazi Thomas Simba.
 
WATU wawili wakiwemo Mwanasheria na Mwalimu, wamepandishwa kizimbani katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar es Salaam wakikabiliwa na mashitaka ya kula njama za kumuua Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), Jaji mstaafu Damian Lubuva na familia yake.

Washitakiwa hao, Mwalimu Samwel Gikaro (30) na Mwanasheria Angela Mbonde (32) walifikishwa mahakamani hapo jana na kusomewa mashitaka mbele ya Hakimu Mkazi Thomas Simba.

Wakili wa Serikali, Hellen Moshi alidai kati ya Oktoba 23 na Novemba 16, mwaka huu katika maeneo tofauti Dar es Salaam na maeneo mengine nchini, washitakiwa na wengine ambao hawajafika mahakamani, walikula njama za kumuua Jaji Lubuva na familia yake.

Washitakiwa walikana mashitaka na upande wa Jamhuri ulidai kuwa upelelezi wa kesi hiyo unaendelea na kuomba tarehe nyingine ya kutajwa. Wakili wa upande wa utetezi, Moses Kaluwa ambaye alifika mahakamani hapo kwa niaba ya Wakili Peter Kibatala, aliiomba mahakama itoe dhamana kwa washitakiwa kwa kuwa mashitaka yanayowakabili yana dhamana.

Wakili Moshi alidai Jamhuri inatambua mashitaka hayo yana dhamana kisheria, lakini inaomba dhamana izuiliwe kwa muda hadi watakapoona inafaa kwa sababu ya asili ya kosa, washitakiwa hawawezi kuwa nje wakati upelelezi unaendelea.

Hata hivyo, Wakili Kaluwa alidai sababu zilizotolewa na upande wa jamhuri hazina msingi kisheria, suala la msingi ni mashitaka yanayowakabili kuwa na dhamana na washitakiwa wapo tayari kutimiza masharti yatakayotolewa na mahakama.

Hakimu Simba alisema pamoja na mashitaka hayo kuwa na dhamana kisheria, kutokana na kosa pamoja na hatua ya upelelezi, mahakama imekubali hoja za upande wa jamhuri hivyo washitakiwa watakuwa rumande. Kesi itatajwa tena Desemba 15, mwaka huu.


Chanzo: Habari Leo.

Mbona Werema alipotaka kumuua Kafulila hajapandishwa Kizimbani??
Kafulila alitoa taarifa Polis
 
Amen amne. mbona wapinzani wengi tu walikiri kumpa kura Magufuli hilo halina mjadala na Magufuli ameshinda kihalali kwa kujipambanua na udhalimu!

Hao wapinzani wengi uliwaona wapi wakakuambia kuwa walimpa kura Magufuli. Acha uzushi.
 
Babu Lubuva ana bahati sana,ila hakuna haja ya yote haya.

Ingekuwa bora zaidi kabla hawajaenda huko wangemnyoso.
 
Hao wapinzani wengi uliwaona wapi wakakuambia kuwa walimpa kura Magufuli. Acha uzushi.

Weeeeeeeengi mno! Tatizo siwezi kuwataja majina! na wengine humuhumu mitandaoni including JF wanasononeka kutompa kura zao!
 
Nawakumbusha wachangiaji kwamba hiki tukio linetokea Kabla ya tarehe ya uchaguzi, tarehe 23/10, nani alikua na interest ya kumuua Lubuva at that time?
 
Na wewe sijui utaenda wapi! baada ya mamvi kuliwa hela sasa hana dili na sidhani kama atagawa hela tena!Na wewe hata mkorosho mmoja huna! vp ishu ya kugombania maiti inalipa or?

Mimi siyo mtumwa kama wewe
 
Lubuva bila kutubu jinamizi la wizi wa kura litamwandama maisha yake yote.



Tatizo ulilokuwa nalo ni kuishi kwa akili za kushikiwa. Uicho tuletea hapa ni jinsi gazeti la habari leo lilivyoripoti kutoka mahakamani, zaidi ya hapo, sijaona ulichotaka kutuambia juu ya tuhuma hizo, kwamba ama wamesingiziwa au kuna element za ukweli katika tuhuma hizo. Zaidi nilichokionana, ni kutumia habari ya habari leo kama mahali pa kuanzia ili uanze kutuaminisha unachotaka wewe.

Wenye ukawa wameishakaa, wenye viherehere ndio waliobaki hasa huku kwenye mitandao. Nina imani hata hao akina mbowe, lowassa na mbatia walikuwa wameisoma namba zamani sana na ndio maana huwasikii wakiongelea hekaya zenu. Muda wa kuwarudisha watz kwenye jambo la matokeo umeisha. JPM kasema hivi, kila mmoja kwa nafasi yake afanye kazi, enzi za blabla zimekwisha. FANYA KAZI
 
U group administrator una cosquences !!! Ngoja kesi ianze mtacheka
 
Back
Top Bottom