Kongwa vs Hai ,wapi kuna maendeleo?

Kongwa vs Hai ,wapi kuna maendeleo?

Cosovo

JF-Expert Member
Joined
Jul 8, 2018
Posts
667
Reaction score
1,820
Nimemsikia Spika Ndugai wa jimbo la Kongwa amesema mh Mbowe alikuwa anazurura na hakuna alichokifanya wakati akiwa mbunge wa Hai kule Hai

Tunaangalie maendeleo katika majimbo mawili kwa wale waliowahi kufika majimbo haya mawili

1,Barabara za Halmashauri na TANROADS za Hai na Kongwa zikoje (Barabara za lami) ni km ngapi

2,Huduma ya afya,hospital, zahanati na vituo vya afya

3,Elimu,miundo mbinu ya shule za awali,msingi,sekondari na vyuo vikoje majimbo mawili

4,Maji,asilimia ngapi ya wananchi wa Kongwa na Hai wanapata maji safi,maji ya bomba na miundombinu yake

5,Shughuli za kibiashara,kilimo,ufugaji na kipato,na masoko,minada ,pia tuangalia ni Jimbo gani kati ya Hai na Kongwa kuna mazingira mazuri katika shughuli orodheshwa na kipato kutokana na shughuli husika

6,Watumishi wa umma,wapi watumishi wa umma wanapewa makazi bora ,support na matokeo mazuri kwa huduma zitolewazo na watumishi wa umma

7,Umeme,tuangalie usambazaji wa umeme wa REA na vijiji vingapi vimepata umeme kwa kila jimbo na vingapi bado

Wale ambao mnayafahamu haya majimbo haya mawili tunaomba mtuwekee data za majimbo haya mawili ili tuondoa utata wa walichofanya Spika Ndugai na mh Mbowe kwenye majimbo hayo mawili
 
Haha wananchi wa kongwa ni kama wako utumwani ni kama wamelogwa hivi na mbunge wao.
Ndugai huwa anawapoza na Pombe za kienyeji na kuwatisha kuwaroga Wananchi wa Kongwa

Huwa anafikia kuwahadaa ati atawaletea wawekezaji ili wawekeze kwenye Shamba la Mibuyu.

Tokea lini Mibuyu ikalimwa hata ikilimwa mpaka uvune ni Miaka 200.
 
Hii ndio Kongwa ,Mbunge wake Ndungai!
FB_IMG_1618339332146.jpg
FB_IMG_1618339343027.jpg
 
Back
Top Bottom