Kongamano: Mwanza ya kijani

Kongamano: Mwanza ya kijani

Hivi kumbe CCM wanaruhusiwa kufanya mikutano ya hadhara eehh!!
 
Wazee wa kusaidiwa na Police kwa mbwembwe!!
 
Itakuwa ya kijani kwa kuwauzia waokota makopo kitambulisho elfu ishirini nyie 2020 hata police wataona aibu kuwatetea
 
Use ya brain unapoongea na watu!
Mbona kukiwa na maendeleo kwa wakulima mnasema serikali ya sisiem ndo imewainua?
Mbona mama lishe wakipata mabanda mapya mnavaa jezi zenu kwenda kuyazindua?
Huwezi kutenganisha maendeleo ya wananchi na serikali iliyopo madarakani!!
Wala huwezi kutenganisha umasikini wa wananchi na uongozi wao!
Hakuna mifumo bora ya kumuinua mkulima!
Hakuna mifumo bora ya kuwainua machinga!
Yeyote anaeotoboa ni kwa ujanja ujanja tu na sio mifumo halisi!
Vua koti la chama kabla hujaja kuongea mbele yangu.
Kweli wewe "mdomo Bakuli "

Maendeleo ya mtu binafsi ni matokeo ya juhudi zake. Sione uhusika wa Serikali.

Uvivu wako wa mawazo ndyo umasikini wako.
Sasa endelea kulalamika bila kufanya kazi uone cha moto.

Utanyooka mpaka ukome... Siasa za kuongea bila kujishughulisha hazina tija, hata chama gani au mtu gani aingie madarakani,... Bila kujituma wewe binafsi, hatakuletea Maendeleo yako binafsi
 
Ulivyokuwa mjinga unafikiri wanaokosoa kuwa wanalalamika!!
Wanaosema hali ngumu hawafanyi kazi!
Wanaosema biashara ngumu sio kwamba hawana biashara bali ndo wafanyabiashara wenyewe!
We vaa jezi lako la kijani endelea kushangilia kwakuwa unapokea posho!
Mie ni mwananchi wa kawaida ndo nazifahamu hali za wenzangu!
Endeleeni kuwaza hivyo hivyo kuwa Wanaosemasem eti hawana kazi wala cha kufanya!
 
Mtizamo wa kila mtu hauhitaji kubezwa,ni mtizamo tu kuwa CCM Mwanza itashinda saa mbili asubuhi

Nisaidie ni kwa lipi litakalofanya ishinde asubuhi?

Tuko Mwanza mjini jimbo la Ilemela just few kms from lake victoria....Nyasaka tuna zaidi ya miezi sita hata tone la maji hatuna! Hayo ndo maendekeo unayoyaongea?

Jimbo la Nyamagana, Nyegezi majengo anakoishi mbunge mwenyewe maji ni shiiiidaaa kila leo mnakuja na song lilelile kuwa kuna mradi kabambe utamaliza tatizo la maji jiji la Mwanza...Are we crazy?

Kampeni unaruhusiwa endelea kufanya lakini mnafeli sana tu. Huwezi kutuambia maji yamekuwa kidogo sababu ya ongezeko la watu.....hivi serikali haina master plan?

Mkitaka kujipima kama mnakubalika unavyodai,wekeni tume huru na muachane na polisi halafu muone muziki ulivyo mnene!
Kura yako wewe mlalamikaji wa kila siku peleka Chadema ruksa mkuu. Shida haziwezi kuisha siku moja mkuu haya mambo ya shida mbalimbali yapo tu mpaka mwisho wa dunia lakini juhudi tunaziona mkuu!
 
Membe akifanya anaambiwa kuwa kaanza kampeni mapema, ila kwa kuwa mwanza ni wasukuma, wana haki ya kufanya kila jambo
Naam Mkuu... ndio maana hata wao wanabaguana "huyu mwenzetu na huyu si mwenzetu..."
Maendeleo hayana chama...
 
Membe anasababisha watu na mambo kama kwani hawapati usingizi.
Huku Membe huku Lissu mambo sio ya kubeza lakini ndio hivyo tena siasa ni hoja
Sio vibaya kujipa matumaini.
Unawafahamu wasukuma wewe wakisha choka?
Haya yakifanywa na chadema, mtasema tu, wameanza kampeni kabla ya mda.
 
Wametupora uhuru wetu kwa kisingizio cha madaraja
 
Back
Top Bottom