Kongamano la Katiba Mpya larindima Buchosa

Kongamano la Katiba Mpya larindima Buchosa

Shikilia hapo hapo.

Lakini sasa ni lazima muwe na mkakati maalum na mpangilio mzuri wa haya mambo yote mnayofanya, isije ikawa ni moto wa mabua.

Hawa wanaohudhuria makongamano, inaelekea wengi wao tayari ni wanachama wenu au wapenzi wa chama. Hakikisheni hawa wanaiva vizuri kutokana na makongamano hayo, na hawa ndio watakaoeneza habari kwa wananchi wote nchi nzima.

Yasije yakawa madoidoi tu, wanapotoka hapo na wao wasiwe wanajuwa kitu!

Kumbukumbu zenu zinaonyesha maendeleo mnayofanya hadi sasa? Mnayo 'feedback' ya kujuwa wapi pana udhaifu ili mrekebishe mapema?
Mnajuwa mmepata mafanikio kiasi gani hadi sasa, tokea muanze shughuli hizi?

Ni lazima mfanye mambo kisayansi, vinginevyo hata wakati mkiboronga bila ya kufanyiwa faulo yoyote, msigeuke kulaumu wengine kwa lawama zinazowahusu nyinyi wenyewe kwa kutojuwa mnachofanya na matokeo yake ni yapi.

Ushauri ni ushauri tu.
Ni ushauri mzuri
 
Kuna lile kundi lililoshikiwa akili la UVCCM wao wanaendana na fursa na biti za Rais, kwasasa msimamo wao ni kua katiba mpya siyo hitaji la waTanzania kisa tu mtu flani amesema.
Siku huyo mtu akisema jamani tunahitaji katiba mpya utawaona wanageuka Kama matete au tiyara inavyopelekwa na upepo.

CCM ingekua chama kizuri Kama ingekua haifungamani na Serikali, nikiimanisha viongozi wa kiserikali watokane usahili siyo uteuzi.
Kwa mfano chama gani unachokitambua wewe hapa Duniani kinachopata viongozi kwa usaili?
 
Naomba tuanze kampeni ya kumtangaza Zitto Kabwe kwamba ni adui number moja wa madai ya Katiba mpya .
Zitto ana wivu na ghilba. Alidhani alivyohama Chadema itakufa. Yuko ladhi kufanya jambo lolote baya hata kama litawakost wananchi lakini Chadema isifanikiwe.
 
Wale vijana bora na tegemeo la Taifa wanaoitwa Bavicha , leo wameendesha kongamano kabambe la Katiba Mpya kwenye Jimbo la Buchosa , ambapo viongozi mbali mbali wametoa mada kuhusu umuhimu wa Katiba mpya na Tume huru ya uchaguzi .

Mwitikio na hamasa ya wananchi si haba .

Hapa ni Kata ya Kazunzu

View attachment 2163084
Mungu ibariki CHADEMA!
 
Back
Top Bottom