Kombe la Shirikisho Azam: Simba kukipiga dhidi ya African Lyon

Shadida Salum

Journalist at JamiiForums
Sep 11, 2020
69
104
IMG_20210226_145027_551.jpg

Baada ya kutoa kichapo cha goli 1-0 kwa Al Ahly ya Misri katika mchezo wa Klabu Bingwa Afrika, Simba SC hii leo inashuka tena katika dimba la Mkapa kukipiga na African Lyon.

Mchezo huo wa Kombe la Shirikisho la Azam Simba itakuwa ugenini na utapigwa majira ya saa moja usiku kwa saa za Afrika Mashariki.

Kocha wa Simba Mfaransa, Da Rosa amethibitisha kuwa atapumzisha idadi kubwa ya wachezaji ambao walifanya jukumu dhidi ya mabingwa wa Afrika na kuwapa nafasi wachezaji wengine kwenye kikosi kuonesha walichonacho.

"Tutatoa nafasi kwa wachezaji wengine kwenye kikosi kuonesha mashabiki wao pia wako katika hali nzuri na wanaweza kufanya kazi kama kikosi kingine," Alisema Da Rosa

"Tunataka kutoa mapumziko kwa wanaoanza mara kwa mara, wamefanya kazi nzuri na lazima pia wapate likizo ya siku ili kupata utulivu, wanahitaji kupumzika ." Aliongeza Da Rosa

Simba ni mabingwa watetezi wa kombe hilo na wanatarajia kushinda tena msimu huu kwahiyo wamehimiza kikosi kutodharau African Lyon kwani wao pia wanataka kwenda mbali kwenye mashindano hayo.

Michezo mingine itakayopigwa hii leo ni kati ya Mwadui fc dhidi ya Gwambina saa 10 jioni, Mtibwa Sugar dhidi ya Jkt Tanzania saa 10 jioni, Rhino Ranger dhidi ya Tunduru Korosho na KMC dhidi ya Kurugenzi Fc.
 
Dah! Huyu Dada Rosa naona kama anatafuta sababu za kujitetea kama simba itachezea kichapo kutoka kwa African lion
 
Kudadeki,kwani Simba ina timu ngapi?
Iki kikosi mbona ndo kibaya zaidi!!
Iki kikichezeshwa klabu bingwa waarabu kula 4-0 ni kugusa tu.
Simba Sports Club wanakiungo mkabaji timu ya Under 20 anaitwa Salum Shaban, nilimuona msimu uliopita mashindano ya under 20 waanze kumpa game time kwenye mechi za wakubwa huyu ndiyo Matola/Mkude ajaye katika kikosi chetu.
 
Simba Sports Club wanakiungo mkabaji timu ya Under 20 anaitwa Salum Shaban, nilimuona msimu uliopita mashindano ya under 20 waanze kumpa game time kwenye mechi za wakubwa huyu ndiyo Matola/Mkude ajaye katika kikosi chetu.
Tatizo la wachezaji wetu wa ndani,misifa na uspuni ukimkolea wanabweteka.
 
View attachment 1712373
Baada ya kutoa kichapo cha goli 1-0 kwa Al Ahly ya Misri katika mchezo wa Klabu Bingwa Afrika, Simba SC hii leo inashuka tena katika dimba la Mkapa kukipiga na African Lyon.

Mchezo huo wa Kombe la Shirikisho la Azam Simba itakuwa ugenini na utapigwa majira ya saa moja usiku kwa saa za Afrika Mashariki.

Kocha wa Simba Mfaransa, Da Rosa amethibitisha kuwa atapumzisha idadi kubwa ya wachezaji ambao walifanya jukumu dhidi ya mabingwa wa Afrika na kuwapa nafasi wachezaji wengine kwenye kikosi kuonesha walichonacho.

"Tutatoa nafasi kwa wachezaji wengine kwenye kikosi kuonesha mashabiki wao pia wako katika hali nzuri na wanaweza kufanya kazi kama kikosi kingine," Alisema Da Rosa

"Tunataka kutoa mapumziko kwa wanaoanza mara kwa mara, wamefanya kazi nzuri na lazima pia wapate likizo ya siku ili kupata utulivu, wanahitaji kupumzika ." Aliongeza Da Rosa

Simba ni mabingwa watetezi wa kombe hilo na wanatarajia kushinda tena msimu huu kwahiyo wamehimiza kikosi kutodharau African Lyon kwani wao pia wanataka kwenda mbali kwenye mashindano hayo.

Michezo mingine itakayopigwa hii leo ni kati ya Mwadui fc dhidi ya Gwambina saa 10 jioni, Mtibwa Sugar dhidi ya Jkt Tanzania saa 10 jioni, Rhino Ranger dhidi ya Tunduru Korosho na KMC dhidi ya Kurugenzi Fc.
Kituko Cha mwaka

Simba anaaga mashindano leo

Au nasema uwongo Ndugu zangu...
 
kwahiyo kulee Misri tusipeleke kikosi kipana
Kikosi cha wastani kipelekwe.
Unajua pale Misri kwa mfano ukawapiga Al Ahly 4-0,alafu ndo iwe mechi yao ya mwisho wakifungwa wanatolewa klabu bingwa,haki ya Mungu amtoki salama,kwa waarabu walivyo wabaguzi na roho zao mbaya kulipuliwa na sekunde tu.
 
Back
Top Bottom