Richard
JF-Expert Member
- Oct 23, 2006
- 14,939
- 20,400
Umenena mkuu.Unavyokuwa mtu mzima.. maringo huwa yanaisha automatically. Kutokana na experience na mafunzo uliyoyapata maishani. Kwa umri wa koffi ameshazika marafiki na ndugu zake wengi sana .
Mtu mzima anakuwa anajua siku zake za kuishi zimefikia ukingoni.. anaamua kujipa raha na kuwapa watu raha maana hana cha kupoteza..
Kwa mtu kama koffi ambaye ameshatafuta hela sana ujanani... ana kila kitu.. koffi wa sasa hivi hawazi kujenga nyumba wala kununua gari.. anachowaza ni yeye kujipa raha na kuwapa watu wanaompenda raha.. hata kama kwa hela ndogo yeye hana hasara.. maana kusafiri safiri napo ni kujipa raha ya kukutana na mashabiki wake na kuwapa raha...
Koffi anamwona nandy kama mmojawapo wa washabiki wake. Na kwa heshima nandy anayompa koffi kofi hata hajali vyombo vya plastiki wala nini.. hata bill gates alivyokuja tanga alikula wali maharage huku ana smile kwenye sahani ya ajabu. Ama tajiri akiwa na ndugu zake anakula chakula bila maringo hata kama juu ya majani ya mgomba
Maisha ni mafupi hapa duniani, hivyo hakuna sababu ya kujikweza.
Koffi ameanza maisha chini sana hivyo anayafahamu maisha ni nini.
Hata Bill Gate ni hivyohivyo aliacha shule na akaanzia maisha ya chini sana.
Kuna mzee mmoja mtalii alipenda kwenda Uturuki na familia yake kufanya utalii na alipenda kukaa kwenye hoteli moja tu miaka yote ya maisha yake.
Hapo akajenga urafiki na mmoja wa vijana wa hapo hotelini na wafanyakazi wengine maana walimchukulia kama baba yao maana alikuwa mzee.
Huyo jamaa ana familia yake na anasomesha watoto.
Juzijuzi kafariki na kwenye usia watoto wake wameshangazwa na ujumbe kwenye usia ametaka sehemu ya fedha zake wapewe wale wafanyakazi wa ile hoteli na yule kijana aliekuwa akimsaidia.
Kijana alishangaa kupokea simu yenye taarifa hiyo na sasa ana fedha za kutosha kuendesha maisha ya familia yake.
Wale wafanyakazi wengine nao wameshtushwa kuingizwa mpunga kwenye akaunti zao tena ikiwa ni fedha ya kigeni.