SAYVILLE
JF-Expert Member
- Mar 25, 2010
- 5,168
- 7,950
Katika press ya kabla ya mechi ya Yanga vs Mtibwa, Kocha Gamondi alisema ukweli mchungu ambao inawezekana wanachama, mashabiki na wapenzi wa Yanga wangekuwa wanajua ngeli na ung'eng'e wakaweza kumuelewa, angekuwa na wakati mgumu sana.
Gamondi alianza kwa kuomba msamaha kwa wale ambao watakwazika kwa maneno yake halafu akasema Kombe la Shirikisho ni kombe dogo na lisilo na hadhi. Vitimu ambavyo vingine vimeshindwa kwenye Klabu Bingwa vinaangukia huko, ghafla vinajikuta kwenye fainali halafu vinaanza kusumbua watu.
Akamalizia kwa kusema huku Klabu Bingwa ni kugumu mnoo maana kila unayekutana naye ni timu ya viwango, hakuna timu unayoweza kuita ni kibonde.
Sasa kama hadi kocha wako anasema hivyo, wewe mshabiki hoya hoya unabisha nini?
Gamondi alianza kwa kuomba msamaha kwa wale ambao watakwazika kwa maneno yake halafu akasema Kombe la Shirikisho ni kombe dogo na lisilo na hadhi. Vitimu ambavyo vingine vimeshindwa kwenye Klabu Bingwa vinaangukia huko, ghafla vinajikuta kwenye fainali halafu vinaanza kusumbua watu.
Akamalizia kwa kusema huku Klabu Bingwa ni kugumu mnoo maana kila unayekutana naye ni timu ya viwango, hakuna timu unayoweza kuita ni kibonde.
Sasa kama hadi kocha wako anasema hivyo, wewe mshabiki hoya hoya unabisha nini?