Koboko (Black Mamba) - Nyoka hatari zaidi duniani


Black Mamba au Koboko ni moja ya kiumbe hatari kuliko hapa duniani na hii ni kwa sababu ya mkusanyiko wa sumu kali alionao, nyoka huyu ana aina mbili za sumu ambazo hufanya kazi kwa pamoja na endapo mtu atang’wata basi ndani ya dakika 3 hadi 10 mtu huyu akikosa matibabu hupoteza maisha.

Nyoka hawa huwa na maeneo maalumu ya kung’ata ambayo ni kichwani, shingoni au kifuani kwani mara nyingi hukaa juu ya mti, na ukiwakuta chini urefu wao ni futi 16 na akiwa na hasira husimama nusu mwili wake ambapo ni sawa na futi 8.

Wataalamu wanashauri jinsi ya kumuua ni kuchemsha chungu cha maji ya moto au uji kisha kujitwika kichwani na kupita maeneo ambao wanapatikana nyoka hawa, wakitaka kung’ata katika maeneo yao huishia kudumbukia ndani ya chungu hiko chenye kimiminika cha moto, hufa.

Lakini pia nyoka huyu unaambiwa anauwezo wa kutembea mwendo kasi mkubwa sana ambapo anaweza kukimbia 23km hadi 25km ndani ya saa moja, huku binadamu wa kawaida ana uwezo wa kukimbia 12km ndani ya saa moja na endapo mnyama huyu ataamua kung’ata sehemu yenye kundi kubwa la watu basi anauwezo wa kung’ata kunzia watu/wanyama 70 nakuendelea bila kuchoka.

Hapa nchini kwetu nyoka aina hii hupatikana kwa wingi mkoani Tabora na sehemu zenye misitu mikubwa kama vile, Iringa, Morogoro, Milima ya Udzungwa huko wapo wegi sana.

Pia nyoka aina hii hutajwa katika orodha ya wanyama wanaoongoza kuuwa watu wengi zaidi duniani.

Na unaambiwa nyoka huyu akiwa msituni hapendelei kusikia kelele au milio ya gari na mara nyingi endapo atasikia mlio wa gari hupendelea kuufuatilia mlio huo nakufanya shambulio hivyo inashauriwa kufunga vizuri vioo vya magari wakati wa kupita msituni.

Na wataalamu wanashauri kuwa endapo nyoka huyu atakuwa amejificha katika upenyo wa gari basi ni vyema dereva kukimbiza gari hilo kwa mwendo kasi usiopungua 80 na kuendelea kwa ndani ya dakika 10 hadi 15 ili kusaidia kummaliza nyoka huyo kutokana na joto kali au kumchosha nyoka huyo na kumpunguzia makali ya sumu yake ya kudhuru watu.
Mambo ya Kutembea na Jungu achana na huo ujingaa mkuu... Vingine vyote point!!
 
Secretary bird kana miguu mirefu hivi yule ni kiboko ya nyoka.Watemi wengine wa nyoka ni honey badger na mangoose
mongoose anaweza akakimbia msosi akikutana na nyoka mbabe,ila huyo ndege ni balaa,ana miguu mirefu,anarusha mateke vibaya mno.
nyoka ndiyo msosi wake pendwa,siyo kama nyegere,anakula nyoka for fun tu.
 
Chungu cha moto kikikumwagikia?
Kofia ngumu je akikupapasa shingoni ushahisi kitakachokutokea mkuu?maana bora chungu akishuka akikigusa hata kwa bahati mbaya atakuta nacho ni cha moto atainuka juu hiyo kofia ngumu akiigusa si ndo atatelezea hapo shingoni.
 
mongoose anaweza akakimbia msosi akikutana na nyoka mbabe,ila huyo ndege ni balaa,ana miguu mirefu,anarusha mateke vibaya mno.
nyoka ndiyo msosi wake pendwa,siyo kama nyegere,anakula nyoka for fun tu.
Honey badger yeye akigongwa na nyoka anazimia baadae anananyanyuka
 
Tukiwa safarini kuelekea Karatu na Noah, kabla hatujafika mto wa Mbu. Mwanadada mweupe mmoja aliekaa mbele aliomba kushuka ili ajisadie. Akaenda kwenye vichaka karibu kwenye kichuguu cha mchwa. Hapo tuliona tamthilia ya aina yake.kwani mara tu tulisikia kelele na mwanadada yule alikuwa anarudi akikimbia huku chupi nusu mlingoti ikiwa inamkwaza na kumdondosha.Kinachomkimbiza ni nyoka wa kijivu mwenye hasira kali, cha kushangaza nyoka yule aliendelea kumng'ata yule Mwanadada zaidi ya mara moja. Gari nzima tulipaniki na hakuna alieshuka kumsaidia hadi tulipoona nyoka yule akiondoka huku kichwa kikiwa juu. Baada ya majibizano Kwa ushauri wa abiria mara afungwe sehemu alizong'atwa, mara mtu mmoja anyonye sumu, tutafute jiwe la nyoka n.k, vyote kumbe useless! Abiria walishuka na gari na mgonjwa wakarudi hadi Meserani snake park hapo kuna Ant-venom za nyoka aina mbalimbali. Hio ndio iliokoa maisha ya Abiria yule.
Angalizo
Usifunge sehemu kuzuia mzunguko wa damu juu ya jeraha au chini palipong'atwa na nyoka
Usinyonye sumu kwenye jeraha la nyoka. Unaweza kuwa na kidonda mdomoni usichokijua hapo madhara utayaona.
Jiwe la nyoka halisadii, wahi kwenye kituo cha tiba na ni vizuri ukawa na maelezo ya Jinsi nyoka alivyo
 
Back
Top Bottom