KIZOTA-Chumbani kuhesabu kura

KIZOTA-Chumbani kuhesabu kura

Chadema mbona mnaangaika sana na uchaguzi wa CCM mpaka mnatia huruma aisee! Kila mmoja anakuja na lake. Chezea JK.
 
Mzee Tupatupa huenda hukuwepo kwenye chumba cha kuhesabia kura lakini uliyoyaandika nayaamini mara 1000 zaidi kuliko matokeo yaliyotangazwa na Makinda.
Kuchaguliwa kwa asilimia 99.92 seems too good to be true. Waliochakachua hawakutumia hekima, wangeweka angalau kura 100 za No na bado ungekuwa ushindi wa kishindo na unoheshimika zaidi kuliko hizi cosmetics
 
ilikuwa balaa.usalama wa taifa waliingia na kuteka uhesabuji kura. Wakadai kuwa wametumwa kuilinda nchi na mipasuko. Lahaula! Ccm imeshakuwa nchi tena? Sisi tuliokuwa na jukumu la kuhesabu kura tukapigwa vikumbo. Tukaonekana hatufai.wakati huo,tulikuwa tumeshahesabu nusu ya kura za mwenyekiti baada ya zile za makamu wa mwenyekiti wa bara na visiwani.

Si kweli kuwa dr.shein na mangula walipata kura zote. Dr.shein alikataliwa na wapiga-kura 43 huku mangula akikataliwa na 50. Hawa hawakushinda kwa asilimia 100. Kwa zile za uenyekiti,mchuano wa 'ndiyo' na 'hapana' ulikuwa mkali. Hapo ndipo ndugu mackson chizii alipotoka chumba cha kuhesabia kura na kwenda kusikojulikana.aliporudi,akarudi na usalama wa taifa na green guard.

Jana,nimeamini kuwa kura zinazotangazwa sizo zilizopigwa hasa. Ndugu zangu,kwa umafia tuliofanyiwa jana,itakuwa ngumu kwa upinzani kushinda urais wa nchi hii kama wachache watakwenda sirini kuhesabu kura kisha kuzitangaza. Amini nawaambia,kura huibwa.matokeo hugeuzwa.na sisi ccm ndio mchezo wetu.hatutaachia kirahisi ushindi kwa mwingine.

Iko haja kwa mfumo wa kuhesabu kura kurekebishwa.ikiwezekana,na mgombea naye awepo pamoja na wakala wake. Ni jana tu,jk alibadilishiwa matokeo ili ionekane ameshinda kwa asilimia 99.2. Kuanzia jana,nipo tayari kujiunga na upinzani ili tuikomboe nchi hii.sijiungi kwakuwa namchukia jk,najiunga kwa kuchukia uibaji wa kura ambao unakandamiza demokrasia nchini.tunaongozwa na tusiowachagua na tunachagua wasiotuongoza.ni hatari!

Chanzo: Mimi mwenyewe niliyekuwa chumba cha kuhesabia kura kizota chini ya uangalizi wa spika anne semamba makinda. Sina muda tena wa kuogopa. Hawa watu hawafai.
walitengeneza mazingira ya wizi kisha wakaiba wakijua fika kuwa hamuwezi kusema wala kujitokeza. Kama kweli nyie ni vidume kama chama chenu jitokezeni
 
tokea jana niliwaambia jamaa niliokuwa nao...... Haya matokeo yamechakachuliwa haiwezekani yakawa kama yalivyotangazwa....bado mengi yatafumuliwa..................mwanahalisi: Mambo yote yangekuwa hadharani

Mi nashangaa Mwanahalisi na Kubenea wameshindwa hata kuanzisha gazeti lingne? Gazeti limefungiwa kwa muda usiojulikana, sasa wao wanataka wasubiri mpaka lini? Tumekosa vitu vingi adimu kwa kutokuwapo kwa gazeti hili.
 
Hapa tunalishana upepo tu...niaminivyo mimi kama pangekuwa na watu angalau 50 waliopiga kura za hapana halafu matokeo yanatangazwa kuwa eti hakuna kura za hapana,LAZIMA kungeibuka miguno na zomeazomea ya chinichini..
 
Chanzo: Mimi mwenyewe niliyekuwa chumba cha kuhesabia kura Kizota chini ya uangalizi wa Spika Anne Semamba Makinda. Sina muda tena wa kuogopa. Hawa watu hawafai.

Mimi Mwenyewe Ndio Nani? Unless wewe ni Tupa Tupa anayeigiza na Mzee Small; Vinginevyo Ujasiri wako wa kutaka mabadiliko utaanzia na wewe kuacha uwoga na kuanza kwa kuthubutu kuweka jina lako la kweli au picha yako humu; Vinginevyo CCM ni chama cha ovyo, wakuue, wasikuue kwa kuasi, itabakia kuwa hivyo;
 
Chezea chama cha wenyewe wewe! Hakuna demokrasia, ni ndiyo au hapana kwa kwenda mbele. Uchaguzi huru na wa haki ni msamiati ndani ya ccm!
 
Election riging aka wizi wa kura ni sawa na KULA NYAMA YA MTU, CCM haiwezi kuacha kamwe.

Pamoja na Mapenzi yangu kwa Baba wa Taifa JK Nyerere na pia pamoja na kutoipenda CUF, lakini ukweli lazima usemwe to put the reckord in perspective.

Mwasisi wa wizi wa KURA Tanzania ni JK Nyerere, pale alipopora USHINDI wa CUF wa kiti cha Urais wa SMZ wa Maalim Seif (CUF) dhidi ya Komandoo Salmin Amour (CCM) 1995. Nyerere aliiamurisha ZEC ibadilishe matokeo ya URAIS wa ZNZ in favour of Salmin Amour (CCM).

Tangu wakati huo Nyerere alipowalisha CCM NYAMA YA MTU, CCM kamwe haitaacha kuendelea kula nyama ya mtu (read riging election).

Just imagine wakati Kenya wanataka general election Wakenya wapige kura electronically, Mkutano mkuu wa CCM bado wanapiga KURA za makaratasi?! Is it coincidency? NO ni mpango mkakati wa kuendelea ku-rig election.

Wakati Mawaziri wa Kenya wanasoma budget zao kwa Ipad, bado bunge letu la JMT linapiga kura za NDIYO na HAPANA (shouting). Why not introdunce electronically voting in the HOUSE. CCM hawataki kura za haki na huru.

Hii Nyama aliwaolisha Nyerere CCM hawataicha kamwe kabisa. Counts my words.

I will only mark your words because, counting them will take long time.

Even those from the so called diaspora sensed for a long time the smell of it and were all invited to share hivyo vipande ya nyama hii ni hatari kweli kweli.
 
Mtajua wenyewe magamba wizi ndo jadi yenu

Jibu hilo silioni kama ni zuri. Ni la mtu asiyetaka kifikiri kwa wakati huo ama asiyetaka kuongea kwa wakati huo. Unaonaje kama ungenyamaza kimya kisha baadaye ukaja na hoja zenye nguvu? Unaweza na unazo hoja hizo.

Mzee Tupatupa kaleta habari ambayo si njema. Si njema kuendelea kuisikia, ni njema kwa upande wa pili kuwa sasa tutiwe ganzi na kuuvua woga na kufanya zaidi ya vile tulivyoweza huko nyuma dhidi ya dhuluma katika chaguzi mbalimbali; twende hatua tano mbele.

What the hell is this Usalama wa Taifa?
Kwa Kikwete kuendelea kuongoza katika CCM au Serikali ndiyo Usalama? Ndiyo nchi inakuwa salama? Mbona ni vitu vya aibu.

Kwanikaza kuwalinda mnaowataka katika CCM na kwenye vyama vya upinzani mnavuruga. Sipendi na sitopenda mnalolifanya mnaojiita Usalama wa Taifa.

Kikwete utangazie Umma wa watanzania, kama unajeuri hiyo; ni uchaguzi gani ulioshinda hapa nchini bila ya msaada wa rushwa na the so called Usalama wa Taifa?
 
Kuchamba kwingi mwishowe unatoka na Kinyesi, unafahamu vyema kwamba kuna typing error, yeye alikuwa anamaanisha Matson Chizii, sasa tueleze na wewe una undugu na Bambo?

Nakumbuka hata Saddam Hussein naye alishinda uchaguzi kwa 100% lakini nilishangazwa wale wale tulioaminishwa kwamba wanampenda sana ndio walikuwa wa kwanza kuliangusha sanamu lake baada ya utawala wake kuondolewa. yo can fool some people for some time, but you can not fool all people for all time.

Hapa hakuna unalolijuwa sana sana nenda kwenye Blogu ya shosti wako Mange Kimambi ulete picha nyingine za bikini.

sishangai,najua uko kwenye siku zako!
 
ya ccm yameisha na ulimwengu mzima ukiwemo wa chadema umeshuhudia jinsi walivyomalizana,sasa ni zamu ya chadema nao kuwa tested kwenye uchaguzi wao wa ndani tuone nao watakavyolimaliza suala la uchaguzi wao ndani ambao inasemekana kuna vipeperushi kutoka kundi la vijana wa chama hicho linalodhani sasa imetosha mwenyekiti wa sasa apumzike na kumpisha zitto
 
Kwa kweli mashabiki wengi wa CHADEMA wana upeo mdogo sana! Na hii ndo sababu CHADEMA itasubiri sana kushika dola! Ukisoma uzi huu vizuri unatambua kuwa uwezo wa mwandishi hawezi kuwa hata msafisha choo anachotumiwa Mjumbe yeyote wa Kamati Kuu ya CCM achilia kufikiriwa hata kuwa karibu na kura za CCM zinazokohesabiwa!
 
Election riging aka wizi wa kura ni sawa na KULA NYAMA YA MTU, CCM haiwezi kuacha kamwe.

Pamoja na Mapenzi yangu kwa Baba wa Taifa JK Nyerere na pia pamoja na kutoipenda CUF, lakini ukweli lazima usemwe to put the reckord in perspective.

Mwasisi wa wizi wa KURA Tanzania ni JK Nyerere, pale alipopora USHINDI wa CUF wa kiti cha Urais wa SMZ wa Maalim Seif (CUF) dhidi ya Komandoo Salmin Amour (CCM) 1995. Nyerere aliiamurisha ZEC ibadilishe matokeo ya URAIS wa ZNZ in favour of Salmin Amour (CCM).

Tangu wakati huo Nyerere alipowalisha CCM NYAMA YA MTU, CCM kamwe haitaacha kuendelea kula nyama ya mtu (read riging election).

Just imagine wakati Kenya wanataka general election Wakenya wapige kura electronically, Mkutano mkuu wa CCM bado wanapiga KURA za makaratasi?! Is it coincidency? NO ni mpango mkakati wa kuendelea ku-rig election.

Wakati Mawaziri wa Kenya wanasoma budget zao kwa Ipad, bado bunge letu la JMT linapiga kura za NDIYO na HAPANA (shouting). Why not introdunce electronically voting in the HOUSE. CCM hawataki kura za haki na huru.

Hii Nyama aliwaolisha Nyerere CCM hawataicha kamwe kabisa. Counts my words.

Bobuk: Ninakubaliana na wewe 100% kuhusu matumizi ya teknologia ya habari na mawasiliano kwamba hatuna ujanja ni lazima itumike zaidi katika nyanja zote hapa Tanzania ikiwa ni pamoja na ndani ya siasa. Kukua kwa maendeleo ya nchi kwa ujumla ikijumuisha ukuaji wa demokrasia yatategemea sana matumizi bora ya teknologia ya habari na mawasiliano.

Kama anayosema mleta uzi ni kweli basi CCM ni ya ajabu sana na kwa mtindo huu nchi itakufa tukiangalia. It is pathetic Tatizo hiki chama tawala CCM kitatuumiza sana watanzania kwa kutumia vyombo vya dola kuhakikisha kinadumu daima na milele kushika madaraka.
 
Back
Top Bottom