KIZOTA-Chumbani kuhesabu kura

KIZOTA-Chumbani kuhesabu kura

VUTA-NKUVUTE

JF-Expert Member
Joined
Nov 25, 2010
Posts
6,140
Reaction score
18,006
Ilikuwa balaa.Usalama wa Taifa waliingia na kuteka uhesabuji kura. Wakadai kuwa wametumwa kuilinda nchi na mipasuko. Lahaula! CCM imeshakuwa nchi tena? Sisi tuliokuwa na jukumu la kuhesabu kura tukapigwa vikumbo. Tukaonekana hatufai.Wakati huo,tulikuwa tumeshahesabu nusu ya kura za Mwenyekiti baada ya zile za Makamu wa Mwenyekiti wa Bara na Visiwani.

Si kweli kuwa Dr.Shein na Mangula walipata kura zote. Dr.Shein alikataliwa na wapiga-kura 43 huku Mangula akikataliwa na 50. Hawa hawakushinda kwa asilimia 100. Kwa zile za Uenyekiti,mchuano wa 'NDIYO' na 'HAPANA' ulikuwa mkali. Hapo ndipo Ndugu Mackson Chizii alipotoka chumba cha kuhesabia kura na kwenda kusikojulikana.Aliporudi,akarudi na Usalama wa Taifa na Green Guard.

Jana,nimeamini kuwa kura zinazotangazwa sizo zilizopigwa hasa. Ndugu zangu,kwa umafia tuliofanyiwa jana,itakuwa ngumu kwa upinzani kushinda Urais wa nchi hii kama wachache watakwenda sirini kuhesabu kura kisha kuzitangaza. Amini nawaambia,kura huibwa.Matokeo hugeuzwa.Na sisi CCM ndio mchezo wetu.Hatutaachia kirahisi ushindi kwa mwingine.

Iko haja kwa mfumo wa kuhesabu kura kurekebishwa.Ikiwezekana,na mgombea naye awepo pamoja na Wakala wake. Ni jana tu,JK alibadilishiwa matokeo ili ionekane ameshinda kwa asilimia 99.2. Kuanzia jana,nipo tayari kujiunga na upinzani ili tuikomboe nchi hii.Sijiungi kwakuwa namchukia JK,najiunga kwa kuchukia uibaji wa kura ambao unakandamiza demokrasia nchini.Tunaongozwa na tusiowachagua na tunachagua wasiotuongoza.Ni hatari!

Chanzo: Mimi mwenyewe niliyekuwa chumba cha kuhesabia kura Kizota chini ya uangalizi wa Spika Anne Semamba Makinda. Sina muda tena wa kuogopa. Hawa watu hawafai.

Mzee Tupatupa wa Lumumba
 
Mtajua wenyewe magamba wizi ndo jadi yenu
 
Mzee Tupatupa it mighty be true what you say
but how should i believe the source of information??
 
Last edited by a moderator:
wanakazania kuongoza ya duniani, huku roho zao wakiziteketeza, tena wao wenyewe! TUWE NA HOFU YA MUNGU JAMANI!
 
Sasa Kikwete amefikia viwango vya ujambazi anakwiba mpaka kura za uongozi wa Chama??
 
“Ifuatayo ni risala fupi ya marehemu Chama cha Mapinduzi (CCM). Marehemu CCM alizaliwa 05/02/1977. Enzi za uhai wake marehemu alijishughulisha na kuua mazao ya biashara kama kahawa, tumbaku, korosho, pamba na katani. Marehemu pia atakumbukwa sana kwa kazi kubwa aliyoifanya kwa bidii ya kuua viwanda vyote kama Mutex, Mwatex, Ufi, Kiltex, Tanelec, Bora, viwanda vya kusindika nyama na maziwa, kiwanda cha karatasi na viwanda vyote unavyovikumbuka. Alijishughulisha sana pia na kuwaleta wageni na kuwapa mali za watanzania. Hadi anafariki ameacha Wachina kariakoo, Waarabu Loliondo, Makaburu Mererani na Wazungu wa kila aina kwenye migodi yote ya madini na gesi. Marehemu pia atakumbukwa kwa operesheni kadhaa za kuhujumu uchumi hasa zile za EPA, Meremeta, Deep Green Finance. Mwaka 2008 marehemu alifunga ndoa na (kinatajwa chama kimoja cha siasa nchini). Ameacha watoto watatu wa kiume mmoja aitwaye (chama kingine) na wa kike wawili (vyama vingine viwili). Bwana ametoa, Bwana ametwaa, jina la Bwana libarikiwe”. Safari njema kurejea makwenu wajumbe wa mkutano mkuu wa CCM.
 
....Chanzo: Mimi mwenyewe niliyekuwa chumba cha kuhesabia kura Kizota chini ya uangalizi wa Spika Anne Semamba Makinda. Sina muda tena wa kuogopa. Hawa watu hawafai.

Mzee Tupatupa hapo kwenye red umetupia. Ni vigumu kukuamini!!
 
Ee Mungu tuponye na huu unafiki wa wanasiasa hasa wa CCM. Tumewachoka kupita kiasi. Kama haya yametendeka kweli, basi CCM ianze kujiandalia kaburi lake, maana wakati wa kafariki kwake umekaribia
 
Hata ingekuwa ni uchaguzu wa kiongozi wa dini na wapiga kura ni waumini wakiwa kumi na kuendelea hawezi pata kura zote.Ccm hawana chaguzi huru.kikubwa kwao ni majigambo.Mkamba Tembo halemewi na mkonga,Je akizeeka au akiugua?
 
It is no surprise. Afu ati jk anatangazwa anapiga makofi as if nae kawa surprised na ushindi.

Bora muifisadi hii nchi, ikifikia tukaanza kuhesabu kura kiteknikali mtashangaa!
 
Election riging aka wizi wa kura ni sawa na KULA NYAMA YA MTU, CCM haiwezi kuacha kamwe.

Pamoja na Mapenzi yangu kwa Baba wa Taifa JK Nyerere na pia pamoja na kutoipenda CUF, lakini ukweli lazima usemwe to put the reckord in perspective.

Mwasisi wa wizi wa KURA Tanzania ni JK Nyerere, pale alipopora USHINDI wa CUF wa kiti cha Urais wa SMZ wa Maalim Seif (CUF) dhidi ya Komandoo Salmin Amour (CCM) 1995. Nyerere aliiamurisha ZEC ibadilishe matokeo ya URAIS wa ZNZ in favour of Salmin Amour (CCM).

Tangu wakati huo Nyerere alipowalisha CCM NYAMA YA MTU, CCM kamwe haitaacha kuendelea kula nyama ya mtu (read riging election).

Just imagine wakati Kenya wanataka general election Wakenya wapige kura electronically, Mkutano mkuu wa CCM bado wanapiga KURA za makaratasi?! Is it coincidency? NO ni mpango mkakati wa kuendelea ku-rig election.

Wakati Mawaziri wa Kenya wanasoma budget zao kwa Ipad, bado bunge letu la JMT linapiga kura za NDIYO na HAPANA (shouting). Why not introdunce electronically voting in the HOUSE. CCM hawataki kura za haki na huru.

Hii Nyama aliwaolisha Nyerere CCM hawataicha kamwe kabisa. Counts my words.
 
Back
Top Bottom