Hajatamka kwamba ana mpango wa kugombea urais mwaka 2015. Lakini kila anachofanya kinahusianishwa na urais. Hii inaonesha wazi kuwa, Lowasa ni tishio iwe ndani ama nje ya CCM. Na ni wazi hakuna wa kumzuia asikanyage kitalu namba 1, Magogoni iwapo ataamua kujitosa ktk kinyang'anyiro hicho iwe anatokea CCM ama chama kingine na hata akiwa mgombea binafsi. Wapi na lini alitangaza kuwa atawania urais baada ya JK? Kama kishindo chake kinatetemesha, vipi akitokea mwenyewe?