Kituo cha polisi Bumbuli chachomwa moto

Kituo cha polisi Bumbuli chachomwa moto

Hawahawii kusema wana video ya chadema ikipanga mipango ya kuchoma ofisi ya kata na kituo cha policcm
 
Ni kweli kimeharibiwa na wananchi tatizo ni kufungwa kwa mganga wa kienyeji kwa jina Manyaunyau anayefanya kazi ya kuondoa majini kwa wachawi.
Inavyosemekana wazee wachawi wa Bumbuli mjini wamekataa mganga huyo kufanya kazi hiyo kuhofia kuingia aibu.
Source mtu wa karibu aliyepo Bumbuli.
Kwa hiyo sababu ni ushirikina! Funny. Shida ya Polisi wa sasa wanakosa busara hivyo maamuzi yao huwa ni utata tu. Jambo dogo sasa limezaa kubwa.
 
Yupo twira..........

mbunge wa twita na fesibuku mjinga sana huyu dongo lakini nashukru wana bumbuli wamesha mshitukia juzi wamemuonyesha kwa kijiji kumchagua kiongozi wa chadema, huwezi kuongoza jimbo kwa twita hukuùkijua wananchi wako hata asilimi tano hawajui fb na twita..watu wa hivyo ni akina mnyika hao hata wakishinda twita nitamwelewa..
 
Kuna watu kila kitu lawama kwa serikali nahisi hata wakipigana na wake zao lawama kwa serikali.

sana tu mimi mmoja wao, hivi unajua maisha yakiwa magumu hata hata tendo la ndoa hulitoi ipasavyo, hivi unajua maisha yakiwa tight ndai hakukaliki ndoa ni mifalakano naniaànasababisha.. Kama unaongezwa mshahara elfu kumi kisha mchele,mafuta,nauli,kodi ya pango, kifupi kila kitu kikapanda nani anani alaumiwe...
 
Siwashangai kwakuwa kila kitu kwenu ni mtaji. Suala hapa ni wazee wa stendi pale bumbuli ambao inasemekana ni washirikina sasa wamekataa huyo mganga kuwatoa majini na wakahonga polisi ili akamatwe huyo manyaunyau kuepusha aibu sasa wapi ccm kuchokwa hapo?

kama kikwete alikubali kuwekewa majini kwanini manyaunyau anawatoa majini au anataka wawe wanadondoka hovyo kama kikwete kipindi hajawekewa majini na sheikh yahaya..
 
Mwanangu we muongo sana haufai kuaminiwa hata kidogo mambo ya ushilikina na siasa wapi na wapi?

Kama amesema uongo ushuhudie uongo wake lakini kama amenena vyema mbona unamkashifu?
 
Ni manyaunyau huyu huyu wa tbt mawenz au kaibuka mpya?Nimemmis sn huyo jamaa!
 
duh,hii ni hatari sana,mbona wananchi wamebadilika sana siku hizi?

Kuna mtu ambaye hajachoka kweli?? Raisi alipoongea na watanzania pale uholanzi alisema anashangaa watu wanasema nchi imemshinda wakati haijamshinda. Wakati wa Mwalimu, Mwinyi, Mkapa sikuwahi kuyaona haya.
 
Kama amesema uongo ushuhudie uongo wake lakini kama amenena vyema mbona unamkashifu?

sijamkashifu labda haujasoma uzi tangia mwanzo issue iliopo kule ni masuala ushirikina na sio siasa.
 
Siwashangai kwakuwa kila kitu kwenu ni mtaji wa kisiasa na usishangae mkalianzishia majadiliano ili kuonyesha mambo hayaposawa bumbuli ila mtakuwa mnajidanganya wenyewe. Suala hapa ni wazee wa stendi pale bumbuli ambao inasemekana ni washirikina sasa wamekataa huyo mganga kuwatoa majini na wakahonga polisi ili akamatwe huyo manyaunyau kuepusha aibu sasa wapi ccm kuchokwa hapo?
Mkuu watu wanapenda kuja na hoja za ufitinishi.! Labda tu unijuze ule uchaguzi wa serkali za mitaa bumbuli matokeo yalikuwaje? Inaelekea wanataka kuhusisha mambo hapo
 
Kumbe! But wenyewe hawaoni aibu kusema ni sisiyem. Lol

Kuna nut fulani kwenye reasoning yao iko loose. mtu hata akihelewa kununua umeme wa Luku anailaumu CCM. Mtoto wake mvuta bangi akipata zero kosa la CCM. Hela ya kodi ya nyumba akinywea pombe tatizo ni CCM. Yaani kulaumu CCM ndio imekuwa easy way out...
 
Mkuu watu wanapenda kuja na hoja za ufitinishi.! Labda tu unijuze ule uchaguzi wa serkali za mitaa bumbuli matokeo yalikuwaje? Inaelekea wanataka kuhusisha mambo hapo

Hizo taarifa sina za kueleweka ila za juujuu ni kwamba maeneo ya mlalo na kijiji cha kwekitui wameshinda cdm ila kuanzia kata ya Bumbuli, Baga, dule, na kutuko bumbuli kwenda chini tamota, mpaka kwa makamba hakuna harufu ya upinzani.
 
Nyakati hizi tulioko ni ya uwazi na ukweli flu!
Hakuna mjinga tena!

Acha wanainchi wafanye watakavyo!
Na hiyo ni traller tu 2015 hakuna mjinga!

kuchoma kituo cha polisi na ofisi ya serikali ya mtaa ndio ujinga wenyewe huo, kwa sababu hakuna sehemu duniani ambapo hakuna uongozi, watu wenye akili timamu hukaa pamoja na kuchagua uongozi wao wenyewe katika mtaa kwa ajili ya kusimamia maendeleo yao na ulinzi na usalama katika eneo lao.
 
Back
Top Bottom