Kituo cha polisi Bumbuli chachomwa moto

Kituo cha polisi Bumbuli chachomwa moto

kama kisa itakuwa ule uchaguzi wa serikali ya kijiji unadhani wachomaji watakuwa akina nani mkuu?

Watakuwa walochaka na wizi wa kura na unyanyasaji wa police ambapo sasa imekuwa siyo shm ya kupata haki tena
 
Naambiwa na ofisi ya kata nayo imehalibiwa vibaya sana wanasema hawana mbunge wa kuatetea bali wana mbunge wa kwenye magazeti mkaazi wa dar es salaam ambaye ni january makamba..

mchaguni slaa sasa.masabur kazini
 
Makamba hakuwapo?

Nimeona tweet ya januari makamba kuwa alimfukuza mganga huyo na kisha wazee wakachukia sana kwa yeye kufanya hivyo na mganga akaahidi kumuwinda januari
 
Ni kweli kimeharibiwa na wananchi tatizo ni kufungwa kwa mganga wa kienyeji kwa jina Manyaunyau anayefanya kazi ya kuondoa majini kwa wachawi.
Inavyosemekana wazee wachawi wa bumbuli mjini wamekataa mganga huyo kufanya kazi hiyo kuhofia kuingia aibu.
Source mtu wa karibu aliyepo Bumbuli.
Tatizo la kudharau elimu. Yote haya yanatokana na wenyeji kutofuta ujinga.Hivi huko hata dini hazijasaidia kuondoa imani hizi?
 
Mkuu hofu yangu ni kwamba hao wananchi wanaweza kuunganishwa kwenye kesi ya ugaidi.
nchi hii mtu ukishajitambua unaitwa gaidi

Ni kweli hata Sheikh Ponda & Ilunga (my mentor ) anaitwa GAIDI na wenye nchi yao !
 
Tatizo la kudharau elimu. Yote haya yanatokana na wenyeji kutofuta ujinga.Hivi huko hata dini hazijasaidia kuondoa imani hizi?

Ni kweli mkuu kule kuna dini za kurithi kutoka kwa mababu na sio za kutoka kwa mungu wetu tunayemwani wakweli. Kiasi unaweza mkuta mtu ni mchungaji/shekh halafu ni mshirikina.
Kuhusu elimu kwenye ushirikina hata waliosoma wameathirika na ushirikina.
 
ni kweli kimeharibiwa na wananchi tatizo ni kufungwa kwa mganga wa kienyeji kwa jina manyaunyau anayefanya kazi ya kuondoa majini kwa wachawi.
Inavyosemekana wazee wachawi wa bumbuli mjini wamekataa mganga huyo kufanya kazi hiyo kuhofia kuingia aibu.
Source mtu wa karibu aliyepo bumbuli.

kama ni hivyo wamekosea kuharibu mali ya ccm,hivi matatizo ya bumbuli atayamaliza manyaunyau?watz tumelogwa badala ya kudai vitu vya msingi tunadai ushirikina halafu mbunge wao si huyu ambaye anahamasisha digital?.
 
kama ni hivyo wamekosea kuharibu mali ya ccm,hivi matatizo ya bumbuli atayamaliza manyaunyau?watz tumelogwa badala ya kudai vitu vya msingi tunadai ushirikina halafu mbunge wao si huyu ambaye anahamasisha digital?.

Uzembe tu.
 
Kunatàrifa nimezipata
kuwa kituo cha polisi cha BUMBULI kimechomwamoto baada ya momgano wa
polisi na wananchi..naendelea kupata taarifa zaidi na kukama alienipa
taarifa kama naweza kunipatia picha..

Chadema!
 
"@Chahali Kituo hakijachomwa moto. Ila ni kweli wananchi wana hasira sababu tumemfukuza mtu waliyemuita na kumlipa kuibua wachawi. Waambie JF"

"@Chahali Changamoto kubwa kwetu kule sio tu barabara, elimu, etc. Ni pamoja na mambo kama haya. Yametubakiza nyuma miaka mingi. Tunayakabili"

Hayo ni maelezo niliyopewa na Mbunge wa Bumbuli Mh January Makamba kupitia mtandao wa kijamii wa Twitter
 
"@Chahali Kituo hakijachomwa moto. Ila ni kweli wananchi wana hasira sababu tumemfukuza mtu waliyemuita na kumlipa kuibua wachawi. Waambie JF"

"@Chahali Changamoto kubwa kwetu kule sio tu barabara, elimu, etc. Ni pamoja na mambo kama haya. Yametubakiza nyuma miaka mingi. Tunayakabili"

Hayo ni maelezo niliyopewa na Mbunge wa Bumbuli Mh January Makamba kupitia mtandao wa kijamii wa Twitter

Asante kwakuweka mambo sawa.
 
Kuna watu kila kitu lawama kwa serikali nahisi hata wakipigana na wake zao lawama kwa serikali.
 
Back
Top Bottom