Kitillya na wenzake wataka upelelezi uharakishwe

Kitillya na wenzake wataka upelelezi uharakishwe

Upelelezi ni kwenda tandale kukamata vibaka pale eeh?
Hujitambui.... kwa nini wasifanye upelelezi na wakiisha maliza ndo wawapeleke watu mahakamani badala ya kwenda warundika watu mahabusu kabla ya upelelezi kuisha kwa makosa yasiyo kuwa na dhamana? Miezi 6 mkuu.....kuna
watu walio Mahabusu kwa makosa ya madawa miaka 4..... upelelezi unaendelea... si hata hayo madawa yameisha expire.... acha ushabiki, haya ni maisha tu... kama si wewe kuna siku itamkuta
ndugu au jamaa yako na ndo utatambua hili...
miaka 4 mpaka 5 upelelezi unaendelea? .... hakimu akifuta kesi wakitoka nje wanakamatwa tena....
 
Hata Mimi najiuliza hilo Hilo. Kama mnajua upelelezi haujakamilika, ni kitu gani kinachomsukuma huyu dpp kuwafungulia watu mashtaka

Pili taasisi ya dpp inashindwa vipi kukamilisha upelelezi wa watuumiwa kwa miezi 6 tokea wafungue kesi?
Mkuu kuna watu wako mahabusu miaka 4 mpaka 5 kwa makosa ya madawa nk ....kesi zikifutwa na mahakama, wakitoka nje wanakamatwa tena... haya ni matumizi mabaya sana ya power alizo pewa DPP.... hii maana yake, nnavo fikiri, DPP anakuwa hana ushahidi wa kutosha wa kupeleka mahakamani ana amua mfunga mshitakiwa
mwenyewe.... na mahakama ndo chombo pekee kinatakiwa hukumu.... wakubwa nendeni magereza muone watu wanavo teseka....miaka 4 ndani si mchezo...
 
Hii case kama ina mkono fulani hivi au kukomoana,uchunguzi gani huo?peleka evidence kama wanakula nyundo sawa kama hawana hatia waachiwe.
Na ukiona hivi ujue evidence walizonazo there is no likelihood of conviction.
 
Uchunguzi uharakishwe ili Iweje? Wao wasubirii jamhuri inaendelea na kazi yake ya uchunguzi kama kanuni zinavyotaka. Kwani hawa wanyonge wasio kuwa na wanasheria mbona wao husubiri uchunguzi ukamilike.

Wasubiri.
Kwani hill ni kosa lake na kosa LA serikali yetu ya kuchelewesha haki ya MTU. Kumbuka hata hukumu ya kufungwa ni haki inapocheleweshwa ni uonevu uliokithiri. Waweza kufurahia sasa lkn kumbuka huu msemo "JELA HAINA MWENYEWE"
 
Duniani kote, sio kila kosa lina dhamana kisheria.

Kuna baadhi ya makosa hayana dhamana kabisa, mtuhumiwa atakaa mahabusu mpaka pale hukumu ya kesi itaposomwa.

Mfano kwa hapa Tanzania, makosa yafuatayo HAYANA dhamana:

murder, drugs trafficking, human trafficking, Armed robbery, Money laundry, Treason, kukamatwa na nyara za serikali, etc.

N.B: Hata kwa makosa yenye dhamana kisheria (bailable offences), still kuna some circumstances Mahakama imeruhusiwa kisheria kunyima dhamana. Circumstances hizo ni kama vile:
-Seriousness of the offence;
-Safety of the offender, kwamba endapo mtuhumiwa akipewa dhamana inawezekana akauawa au akadhurika huko uraiani;
-Possibility for the offender to interfere with investigation;
-Past criminal record of the offender whereas s/he had ever jumped bail in another past criminal case.

-Kaveli-


Unanieleza habari za sheria za Tanzania wakati hoja yangu ni kwamba hapa Tanzania sheria zetu za dhamana ni za ki-Kangaroo.

Nilifikiri ungenieleza duniani kwingine nako watuhumiwa kama hawa wa TRA, wa kutakatisha fedha, hawapati dhamana automatically.

Katika nchi nyingine hunyimwi dhamana automatically kwa kutakatisha fedha, biashara ya nyara, kuuza watu (human trafficking), kuhujumu uchumi, kuuza madawa, kama hakuna violence iliyoambatana na jinai.

Kuna sababu mbili za msingi za kunyima mtu dhamana katika nchi zilizopevuka kwa haki za raia:

1. Seriously violent crimes, kama kuua, armed robbery, n.k. yananyima dhamana virtually automatically.

2. Flight Risk: Kama ni mgeni, kwa mfano, unaeweza kukimbilia kwenu, au umekuwa mtu unaeshindwa kutokea mahakamani siku za nyuma...

3. Kama akipewa dhamana atakuaw tishio kwa jamii.

Hapa eti unanyimwa dhamana kwa sababu utaharibu uchunguzi. Patently Kangaroo judiciaries.
 
Mkuu kuna watu wako mahabusu miaka 4 mpaka 5 kwa makosa ya madawa nk ....kesi zikifutwa na mahakama, wakitoka nje wanakamatwa tena... haya ni matumizi mabaya sana ya power alizo pewa DPP.... hii maana yake, nnavo fikiri, DPP anakuwa hana ushahidi wa kutosha wa kupeleka mahakamani ana amua mfunga mshitakiwa
mwenyewe.... na mahakama ndo chombo pekee kinatakiwa hukumu.... wakubwa nendeni magereza muone watu wanavo teseka....miaka 4 ndani si mchezo...
Mkuu
Kuna mtu mmoja alikuwa anafanya kaz TRA .kwa muda wa miaka mi 3 sasa yuko ndani na bado hajashitakiwa na dhamana kanyimwa..sababu ni hii hii kukosa ushaidi wa kutosha..rafiki zake wengne naskia walikaa ndani miaka saba bila mashtaka kila wiki walikuwa wanafikishwa mahakamani kusomewa mashtaka na kurudishwa rumande..
Sheria zetu ni mbovu sana...dpp kapewa mamlaka makubwa sana na utawala wa nchi hii
 
Hivi kwa nini wabongo wana roho mbaya sana kwa matajiri? Naona wengi mnafurahia kwamba vigogo wapo ndani bila kujali kama wana hatia au la.
Wakati wao wanatuibia walituonea huruma? Mtumishi wa serikali hawezi kuwa na uwezo wa kumiliki VOGUE lakini hao unaowatetea wanayo magari ya aina hiyo kama takataka,kwa nini tusiwachukie?
 
Ukabila unaanza kuimaliza hii nchi au?Ila haki ya mtu haipotei ila huchelewa tu.
 
Alex Mgongolwa upelezi unacheleweshwa kwa watuhumiwa wengi tu sio hao "majizi" pekee unayoyatetea.

Waache wasote Ndani maana walikula bata kwa mabilioni ya wizi na hiyo ndio return yake.
 
Alex Mgongolwa upelezi unacheleweshwa kwa watuhumiwa wengi tu sio hao "majizi" pekee unayoyatetea.

Waache wasote Ndani maana walikula bata kwa mabilioni ya wizi na hiyo ndio return yake.
Kuna watu wanawahurumia hao majizi waliofaidi jasho la watanzania halafu wanajiona wao ni mashujaa
 
Kuna watu wanawahurumia hao majizi waliofaidi jasho la watanzania halafu wanajiona wao ni mashujaa
Wanaowatetea wengi wao ni wanufahika wa huo wizi either ndugu,family friends etc.

Ili iwe fundisho wapigwe mvua 30 ndani.Mijizi kama hiyo ndio inayosababisha madawa hakuna hospital,wanafunzi wanakosa mikopo,miundombinu kutojengwa etc.
 
Unanieleza habari za sheria za Tanzania wakati hoja yangu ni kwamba hapa Tanzania sheria zetu za dhamana ni za ki-Kangaroo.

Nilifikiri ungenieleza duniani kwingine nako watuhumiwa kama hawa wa TRA, wa kutakatisha fedha, hawapati dhamana automatically.

Katika nchi nyingine hunyimwi dhamana automatically kwa kutakatisha fedha, biashara ya nyara, kuuza watu (human trafficking), kuhujumu uchumi, kuuza madawa, kama hakuna violence iliyoambatana na jinai.

Kuna sababu mbili za msingi za kunyima mtu dhamana katika nchi zilizopevuka kwa haki za raia:

1. Seriously violent crimes, kama kuua, armed robbery, n.k. yananyima dhamana virtually automatically.

2. Flight Risk: Kama ni mgeni, kwa mfano, unaeweza kukimbilia kwenu, au umekuwa mtu unaeshindwa kutokea mahakamani siku za nyuma...

3. Kama akipewa dhamana atakuaw tishio kwa jamii.

Hapa eti unanyimwa dhamana kwa sababu utaharibu uchunguzi. Patently Kangaroo judiciaries.


Kwanza kabisa, nimegundua akili zako ni mgando, or you are just an intellectually lazy!

Hivi nilichokiandika mimi, kina tofauti gani na hicho ulichoeleza wewe? hebu tuliza akili vzuri soma tena nilichoandika na uangalie ulivyojibu, sijaona unachopinga! hehehee

Kwenye hiyo no. 1 yako, umerudia kile kile nilichoandika Mimi.

Kwenye hiyo no. 2 yako, umerudia kile kile nilichoandika. Unajua maana ya "to jump bail"? kama hujuwi, iulize Google upanue akili yako.

Kwenye hiyo no. 3 yako kwamba: "Kama akipewa dhamana atakuwa tishio kwa jamii"... yes you are right, hii pia ni another factor for the Court to deny bail. Ila sasa cha ajabu, hii no.3 yako umeipinga tena wewe mwenyewe kwenye hiyo paragraph ya mwisho ulivyohitimisha.

Hebu angalia scenario hii:

Mtuhumiwa kapata dhamana, kisha kaanza kuua mashahidi 'muhimu' kwenye kesi. (nadhani ushawahi kusikia incidents kama hizo, kwamba mashahidi kupata vitisho, au kuuawa, au kupotea kusikojulikana).

Katika mazingira hayo, hapo mtuhumiwa anakuwa:

i) Ni tishio kwa jamii coz anaua mashahidi;

ii) Ameingilia na kuharibu uchunguzi coz wale mashahidi ambao ni muhimu sana anawaua au kuwapa vitisho.

Narudia kusema kwamba, sijaona unachopinga. Ila unajionesha tu jinsi ulivyo mvivu wa kufikiri na kujikanganya mwenyewe.

-Kaveli-
 
Hivi kwa nini wabongo wana roho mbaya sana kwa matajiri? Naona wengi mnafurahia kwamba vigogo wapo ndani bila kujali kama wana hatia au la.

Anaye chukia tajiri atakuwa kichaa, kama yupo. Tuseme kuna mtu anamchukia mtu kama Carlos au Bill Gates na watu kama hao? Siamini hivyo.

Suala ni kuwa watu wanaunganisha utajiri wa watu kama hawa na ufisadi, serikalini au kwenye taasisi zake. Kwamba jamaa waliiba ndio maana wamekuwa matajiri. Kwamba jamaa walitumia nafasi zao au za washirika wao kuiba na kuwa matajiri.

Watu wana wahusisha wengi wa matajiri wa kibongo na uwizi.

Na hata wakishinda kesi haimaanishi kuwa kulikuwa hakuna uwizi au makosa mengine waliyofanya. Hebu angalia uwezo wa waendesha kesi wetu na rushwa ilivyo tawala
 
Back
Top Bottom