MAMA POROJO
JF-Expert Member
- Nov 22, 2007
- 4,974
- 785
kwa hotuba ya leo ameonyesha kwamba hataki utani kwenye mambo ya msingi yenye maslahi kwa taifa na atapambana na yeyote anayeona Rais hana mamlaka hayo
Mkuu wangu hili ni swala la logic tu halina sababu ya kubabaishana. Nahodha hawezi kupanga utengenezaji wa meli wala hakuna aliyeshika uchoraji wala utengenzaji wa Meli iwe mpya ama kukuu..
Pengine wewe hujasoma mapendekezo ya Chadema kwani unatakiwa uwe nani ili usikilizwe! Haya ndio mawazo yenu wanaCCM ama kweli hamna tofauti na Madikteta...Ikiwa Jk hajui tatizo la katiba iliyopo ama sisi wananchi tunataka nini, ataweza vipi kuwachagua watu wenye uwezo wa kujenga katiba tuitakayo!
tutizamo yaliyomo katika hotuba sio tumtizame JK tusiyemkubali
"Tume itasikiliza maoni hayo na baadaye kutengeneza rasimu ya Katiba mpya ambayo baada ya kukubaliwa na Bunge itafikishwa kwa wananchi kutoa ridhaa yao kwa kupiga kura" - JK
"Ni kutokana na hoja hizo Spika akaamua Muswada uendelee kujadiliwa na Bunge na leo Bunge limeupitisha Muswada huo. Baadae Muswada utaletwa kwangu kwa ajili ya kutiwa saini uwe Sheria. Baada ya hapo itabakia kazi yangu na Rais wa Zanzibar kuunda hiyo Tume ili mapema mwakani kazi ya kukusanya maoni ya wananchi ianze. Lengo letu ni kuwa ifikapo mwaka 2014 zoezi zima liwe limekamilika ili mwaka 2015 tufanye uchaguzi tukiwa na Katiba mpya. Itapendeza tukisherehekea miaka 50 ya Muungano na Katiba mpya. Ni matumaini yangu kwamba wananchi wote watashiriki kwa ukamilifu kutoa maoni yao kwa Tume hiyo" - JK
unataka chadema waseme nini tena wakati msimamo wao wameshautoa bungeni au ukusikia mjomba. there was no logic kuendeleaNimesoma mapendekezo yao..na walikuwa na nafasi pia ya kuyaeleza kufafanua kwenye mjadala walioukimbia??
Sioni tofauti ya chadema na tlp, umd ..wote wana haki sawa..
Wananchi watasikilizwa na kushirikishwa..kama chadema hawataki kushiriki well..
Mwita nilianza kuona umebadilka kumbe ni bomu namna hii!!! Maelezo mengi yakowapi??Ama kweli ukitaka kumumuibia Mtanzania Mwanzoni weka maelezo mazuri katikakati weka vipengengele vyako na mwisho muwekee maneno matamu halafu malizia na signature..Ndio maana tunaiingizwa mikenge kwenye mikataba chungu mzima sababu ya uvivu wa kusoma. Badilika bwana..Mkuu huwa napenda maelezo yako lakini tatizo huwa unatumia maneno meeeengi yanayojirudiarudia. Yaani hadi mtu unafika katikati hata huelewi paragraph ya kwanza inaongelea nini. Kifupi insha zako hazina muendelezo.
Nimesoma mapendekezo yao..na walikuwa na nafasi pia ya kuyaeleza kufafanua kwenye mjadala walioukimbia??
Sioni tofauti ya chadema na tlp, umd ..wote wana haki sawa..
Wananchi watasikilizwa na kushirikishwa..kama chadema hawataki kushiriki well..
Mkuu bado hata hunielewi kabisa.... Hili sio swala la CDM, CCM,TLP na kadhalika isipokuwa ni swala la Watanzania wote na mimi nazungumza kama Mtanzania na sii CDM wala NCCR.. Hakuna kati yetu mmoja mmoja mwenye mamlaka ya kuunda tume hilo kwanza..Nimesoma mapendekezo yao..na walikuwa na nafasi pia ya kuyaeleza kufafanua kwenye mjadala walioukimbia??
Sioni tofauti ya chadema na tlp, umd ..wote wana haki sawa..
Wananchi watasikilizwa na kushirikishwa..kama chadema hawataki kushiriki well..
Na. M. M. Mwanakijiji
Ndugu zangu Kitendawili kimetegwa nani atakitegua. Chama cha Mapinduzi kimetaka kutumia madaraka na wingi wake kufanya kile ambacho hakikuwa na hakijawahi kuwa ndani ya ahadi zake. Kimetaka kufanya kitu ambacho hakikupewa ridhaa ya wananchi kukifanya. Sote tunakumbuka vizuri kuwa kampeni nzima ya uchaguzi wa mwaka jana kwa upande wa CCM haikuhusiana KABISA na suala la Katiba Mpya. Katiba Mpya haijawahi kuwa sehemu ya Ilani, ahadi au mipango ya Chama cha Mapinduzi kabla ya Disemba 31, 2010.
Ni uamuzi wa kudandia tena siyo kudandia tu bali kudandia na kushupalia. Leo wanadai kuwa ajenda ya Katiba Mpya ni yao. Lakini wanafanya hivyo wakikataa kabisa kukiri wala kutambua kuwa ajenda hiyo ilikuwa ni ya upinzani kwa miaka ishirini sasa tangu lile kongamano lilillozaa vyama vya upinzani nchini.
Ajenda ya Katiba Mpya imekuwa ni moyo udundao katika mioyo ya wapinzani nchini. Tangu mwanzo ilitambulikana kabisa kuwa mabadiliko ya kweli ya kitaifa hayawezi kutokea kwa kubadili watu tu, kubadili sera tu hata kubadili vyama ilitambulikana kabisa kuwa ni lazima kugusa Kitabu chetu Kitakatifu cha watu wa dini zote ambacho watunzi wake ni sisi wenyewe! Hatuwezi kubadilisha Biblia au Qurani lakini Katiba ni kitu pekee kitukufu ambacho kinatoka kwetu na hicho pekee kinatufunga sote sawa na hivyo kinaweza kubadilishwa na sisi wenyewe tu. Ajenda hii ya Katiba Mpya haiwezi leo kuwa ni ajenda ya CCM na wengine wanakaribishwa kama watoto wasio na kwao! Leo hii tumewaona wabunge wa CCM wakizungumza kwa jazba kana kwamba waliahidi hata mmoja wao kuwa wanataka Katiba Mpya.
Siyo Komba kwa kuimba wala Wasira kwa hasira aliyesimama mwaka jana kutaka Katiba Mpya ndani ya CCM. NONE. Leo wana ujasiri wa kubeza, kukebehi na hata kupiga mkwara wale wanaotaka katiba mpya kwa mfumo ulio wazi, wenye kuweka msingi juu ya wananchi siyo wabunge au Ikulu peke yake! Leo hii watu hawa wana ujasiri wa ulevi wa madaraka kwamba wako tayari kuamuru moto unye kama vile ulivyoteremka kule Sodoma na Gomora kisa tu tumewamua kuwageukia na kuwatazama! Na wapo watu wanaomini kabisa ati ajenda hii inaweza kuongozwa na CCM kwa vile tu CCM iko madarakani! Yaani, watu ambao juzi tu hawakuwa na wazo la Katiba mpya tena wakatubeza, na kutukebehi huku wakishindana kugongana wenyewe kwa maneno wanaweza kuandika mswada wa kusimamia uandishi wa Katiba tukaubali tu kwa vigelegele, ngoma na chereko chereko za vifijo.
Ngoja niliseme hili vizuri tu na kwa uwazi Ee Mungu nisaidie - maana tunazunguka mno - CCM haina uhalali wa madaraka ya kusimamia mchakato wa Katiba Mpya. Inaweza kushirikiana na wengine, inaweza kuzungumza na wengine, lakini yenywe peke yake haina hoja, uwezo, wala mandate (ridhaa) ya kufanya hivyo. Haimo kwenye ajenda yao, na Kikwete alipoamua kufanya hivyo mwishoni mwaka jana hakukuwa na kikao chochote cha Chama cha Mapinduzi ambacho kina madaraka ya kubadilisha sera za CCM. Hakukuwepo na kikao cha Halmashauri Kuu wala Mkutano Mkuu kilichofikia uamuzi wa kuandika Katiba Mpya. Huu ulikuwa ni uamuzi wa Ikulu na Ikulu peke na matokeo yake mswada mzima umezunguka Ikulu!
Wabunge wake hawakutakiwa hata kutoa maoni juu ya Katiba Mpya. Wangeweza kufanya hivyo tu kwanza kwa kukubali kuwa hoja hii ilikuwa inatoka nje yao (kwa wapenzi na wanaharakati) na kuwa kutokana na kutambua huko mchakato mzima kuanzia Alfa yake hadi Omega yake ungehakikisha kuwa watu wote wanashirikishwa siyo wanaburuzwa kwa mikwara ya kitoto na kejeli zisizo na kichwa wala miguu.
Kikwete sasa ametegwa. Kitendawili hiki ni yeye peke yake anatakiwa kukitegua. Alikipiga mwenyewe kwenye hotuba yake ya Disemba 31, 2010 alipotangaza na kutushtua kuwa hatimaye ameona mwanga na nuru ya ajabu ikimzukia na kuwa sasa serikali yake imekubali hoja ya Katiba Mpya . Jambo hili wengine tulilipokea kwa tahadhari tukihofia kile kinachotokea sasa. Tulihofia kuwa kwa vile hoja hii imechukuliwa na Ikulu (Kikwete) basi mchakato mzima utazunguka Ikulu na hivyo ndivyo ilivyokuwa na hapa ndipo kiini cha mgogoro wa sasa kilipo.
Wanaharakati na wanamageuzi nchini, wanayo haki ya kupinga, kukataa na kudhihaki mfumo ambao unapendekezwa na CCM na serikali yake ambao umepuuzia kwa makusudi au kwa sababu ya vimulimuli vya madaraka hoja zote tulizozitoa mwezi Machi. Watanzania ambao wamekuwa wakipigania mabadiliko ya Katiba kuanzia 1992 wanayo haki kabisa siyo tu ya kutoka ukumbini hata kusimama na kuanzisha mwamko wa kupinga kubambikiziwa Katiba Mpya kwa sababu tu watu wana madaraka. Kikwete asaidie kukitegua kitendawili hiki vinginevyo ni yeye ambaye atajiikuta anabeba lawama.
Ndugu zangu, kama sisi sote tutaweka miguu chini na kusema hatusogei na kuamua kugoma tulipo tutalazimishwa kuzungumza na kukaa pamoja wakati damu imemwagika. Hivi kwanini leo Kenya hawapigani mapanga? kwanini leo Zanzibar kuna muafaka, kwanini Zimbabwe kumetulia zaidi kuliko ilivyokuwa miaka michache iliyopita? Ni kwa sababu walifikia kwenye kilele cha kushindwa kuvumiliana. Pande mbili za hizo sehemu zote ziliweka miguu chini na kila mmoja aking'ang'ania upande wake na kukataa kuzungumza na mwingine wala kukubali kwamba yule mwingine yupo. Tangu uchaguzi mkuu wa mwaka jana nimetoa ombi wazi la kusema viongozi wetu wa kisiasa nchini wakae pamoja kuzungumza na siyo kuzungumza tu lakini pia kuwa tayari kukubali upande wa yule mwingine.
Kinachonisikitisha ni kuwa hadi hivi sasa inaonekana watu hawataki kukubali upande wa yule mwingine isipokuwa kwa lazima. "Kubalini msipokubali dola itumike!" wanasema waliolewa ugimbi ule wenye povu la madaraka. Wengine wanasema "msipokubali tutaandamana hadi msitawale" na wengine wanasema "mkiandamana tutawatia pingu hadi mkome" na wengine wanajibu "hamna pingu za kutosha wala magereza ya kufunga fikra". Matokeo yake - watalazimishwa kukaa chini na kuzungumza siku ile tutakapoamka na kusikia watu 50 wameuawa katika siasa! Mtasema tunachuria lakini ndivyo ilivyo mahali pote duniani!
Kikwete tegua kitendawili.
1. Usikubali mswada huu kama ulivyo. Hata wabunge wako waupitishe kwa mbwembwe. Upande wapili hautakubali. Na hamna namna ya kuwalazimisha watu milioni mbili kuukabali. Assadi hadi leo kashindwa anaua watu wake kila siku na bado wanasimama kumpinga. Risasi hazipo za kutosha. Bahati mbaya machozi hayana kikomo... Mkisema kuwa mtaendelea na mchakato na yeyote atakayepinga "atakiona cha moto" well.. mtakuwa mmetengeneza kundi kubwa la wanaowapinga na uzoefu unaonesha kuwa Watanzania nao ni wanadamu wakivuka mstari wa 'sina cha kupoteza isipokuwa utu wangu' tutalia na kusaga meno.
2. Pande mbili zikae chini kuzungumza na katika hili ni utayari wa Rais unasubiriwa. Pamoja na matokeo yale ya uchaguzi mwaka jana nilisema kaa chini na Dr. Slaa mzungumze. Nilimuuliza Dr. Slaa swali hili katika mahojiano na alisema yuko tayari wakati wowote kufanya hivyo. Lakini inaonekana kuna watu hawataki. Na hawa wasiotaka wanafanya hivyo labda kwa hofu kuwa ukikubali kuzungumza na Slaa (nyinyi wawili) basi utakuwa umempa ujiko au Kamati Kuu ya CCM na ile ya CDM vikikaa pamoja itakuwa mmeinua CDM. Well, je ni baya kiasi hicho? Kwamba mje kulazimishwa kukaa pamoja wakati miji inaungua, watu wanakimbiana na kukimbizana na polisi wametanda kila sehemu?
Kikwete tegua. Kitendawili hiki ni cha kwako, hakuna wa kukusaidia. Ulikianzisha mwenyewe na kwa namna nakuonea huruma kwa sababu historia inaweza ikakusamehe kwa mengi sana lakini hili la Katiba Mpya likivurundwa sidhani kama jina lako katika historia litakumbukwa kwa haiba nzuri hivyo. Lincoln anakumbukwa kwa mengi lakini la kutangaza emancipation ya watumwa kumemuweka kwenye level nyingine kabisa. Naamini jinsi utakavyosimamia mchakato wa Katiba Mpya bila kuonekana umeulazimisha ndivyo historia itakavyokukumbuka. Kwanini tufike huko kama tunaweza kuepuka kwa kukaa pamoja katika hali ya amani?
Kitendawili...
MMM