Kitendawili cha Polisi kuzuia mikusanyiko, mikutamo na maandamano kama inavyoruhusiwa na Katiba chateguliwa!

Mag3

Platinum Member
May 31, 2008
13,064
22,757
Yawezekana watu wengi wanashangaa kwa nini hali imeendelea kuwa shwari toka Mh. Tundu Lissu atue nchini. Binafsi nawapongeza Watanzania wenzangu, asanteni Watanzania popote mlipo.

Watanzania kwa mamia na maelfu wameweza kujitokeza kwa wingi na kuandamana kwa amani bila misukosuko yoyote kutoka kwenye chombo chenye jukumu la kulinda amani, asanteni Jeshi la Polisi.

Kwa sasa tungetakiwa kutafakari polisi wetu kila mara kuzuia mikusanyiko huru ya wananchi inatokana na hofu gani? Hiyo hofu ya polisi kuzuia maandamano huru ya wananchi inatokana na nini?

Nina hakika kama polisi wetu wangeingilia hii mikusanyiko tuliyoishuhudia kama kawaida yao, wananchi wengi wasio na hatia wangekuwa vilema wakiuguza majeraha yaliyotokana na vipigo kutoka jeshi hilo.

Je, kama Watanzania tumejifunza chochote kutokana na hali hii? Binafsi naadhani jibu limepatikana...

Kilichodhihirika wazi ni kwamba polisi wetu badala ya kutekeleza jukumu lao kulinda amani wanatumika na chama tawala CCM kuvuruga amani kama kigezo cha kuwanyima wapinzani uhuru wao wa kikatiba.

Hakika adui nambari wani wa taifa hili ni CCM!

LissuDar.jpg
...
LissuBunda.png
LissuMusoma.jpg
LissuShinyanga.jpg
LissuKahama.jpg
LissuTarime.jpg
 
Nimeshangaa sana maandamano na shamra shamra zote za vyama hatujasikia tukio hata la simu kuibwa

Hii ina maana moja, wanaoanzisha vurugu ni Polisi. Ile hoja ya Intelejensia imebaini, ni uongo mtupu!

Inashangaza kwamba Polisi walioaminisha watu kwa miaka 4 kuna uvunjifu wa amani kutoka kwa wapinzani, kuna intelejensia za ajabu ajabu na kila ramli zisizo na kichwa wala miguu, hakuna chochote.

Huu ni ushahidi, Watanzania si tatizo, kuna nyakati Polisi ni chanzo cha uvunjifu wa amani.

Viongozi wa DINI mnaombea Taifa amani, acheni unafiki. Nendeni central Police na Barracks mkawaombee Polisi

Wananchi hawahitaji maombi yenu , hawana tatizo. Hili mlione na muache unafiki
 
Yawezekana watu wengi wanashangaa kwa nini hali imeendelea kuwa shwari toka Mh. Tundu Lissu atue nchini. Binafsi nawapongeza Watanzania wenzangu, asanteni Watanzania popote mlipo.

Watanzania kwa mamia na maelfu wameweza kujitokeza kwa wingi na kuandamana kwa amani bila misukosuko yoyote kutoka kwenye chombo chenye jukumu la kulinda amani, asanteni Jeshi la Polisi.

Kwa sasa tungetakiwa kutafakari polisi wetu kila mara kuzuia mikusanyiko huru ya wananchi inatokana na hofu gani? Hiyo hofu ya polisi kuzuia maandamano huru ya wananchi inatokana na nini?

Nina hakika kama polisi wetu wangeingilia hii mikusanyiko tuliyoishuhudia kama kawaida yao, wananchi wengi wasio na hatia wangekuwa vilema wakiuguza majeraha yaliyotokana na vipigo kutoka jeshi hilo.

Je, kama Watanzania tumejifunza chochote kutokana na hali hii? Binafsi naadhani jibu limepatikana...

Kilichodhihirika wazi ni kwamba polisi wetu badala ya kutekeleza jukumu lao kulinda amani wanatumika na chama tawala CCM kuvuruga amani kama kigezo cha kuwanyima wapinzani uhuru wao wa kikatiba.

Hakika adui nambari wani wa taifa hili ni CCM!

View attachment 1536495...View attachment 1536501View attachment 1536497View attachment 1536498View attachment 1536502View attachment 1536500
Lakini sahvi si mmeruhusiwa ndio maana hamsumbuliwi.
Kipindi kile ilikuwa nongwa kozi haikuwa wakati wenu, mkulu alikataa.
 
Nimeshangaa sana maandamano na shamra shamra zote za vyama hatujasikia tukio hata la simu kuibwa

Hii ina maana moja, wanaoanzisha vurugu ni Polisi. Ile hoja ya Intelejensia imebaini, ni uongo mtupu!

Inashangaza kwamba Polisi walioaminisha watu kwa miaka 4 kuna uvunjifu wa amani kutoka kwa wapinzani, kuna intelejensia za ajabu ajabu na kila ramli zisizo na kichwa wala miguu, hakuna chochote.

Huu ni ushahidi, Watanzania si tatizo, kuna nyakati Polisi ni chanzo cha uvunjifu wa amani.

Viongozi wa DINI mnaombea Taifa amani, acheni unafiki. Nendeni central Police na Barracks mkawaombee Polisi
Wananchi hawahitaji maombi yenu , hawana tatizo. Hili mlione na muache unafiki
Huu uzi nimeuanzisha baada kusikia tetesi za minong'ono inayoendelezwa na wana CCM wenyewe. Eti wengi wao wamekasirika kweli kweli wakiwashangaa polisi kwa nini hawaingilii hii mikusanyiko na kuwaadhibu hao ndugu zetu, kwa nini wanaachia hali hii ya utulivu iendelee, kweli?. Mwingine kaenda mbali na kuuliza eti na green guard nao wako wapi, anawataka hata hao waingilie kati kupambana na hao wananchi wanaothubutu kujitokeza kwenye mikusanyiko hii, kweli?

Wananchi wengi wamekuwa wakijiuliza, hivi hao polisi wanakuwa wapi wasiojulikana wanapowateka, kuwatesa na kuwamiminia risasi raia wa nchi hii. Watanzania ambao walijulikana duniani kote kama watu wa amani, wasio na makuu na wakarimu, wamepotelea wapi? Na kweli ukiangalia hii mikusanyiko inayompokea Mh. Tundu Lissu ni wale Watanzania original tuliowafahamu, tulioishi nao, tuliokula nao...je hii Tanzania ya akina Bashite, akina Gambo na wengine wametoka wapi?

Kuna maswali mengi sana ya kujiuliza...Mtanzania gani anayetishia kuwapiga hadi shangazi zetu? Mtanzania gani anawakebehi ndugu zake waliopatwa na maafa? Mtanzania gani ana ukatili hadi kummiminia risasi zaidi ya thelathini mwakilishi wa wananchi? Maswali ni mengi ndugu zangu. Fikiria mlinda usalama, polisi mtanzania mwenye jeuri ya kuwapiga mama zetu wanaodai haki? Kuwapiga watoto wetu wanaodai elimu bora? Kuwaziba mdomo wasitoe dukuduku zao kama raia wa nchi hii?

Machungu, machungu, machungu...
 
Na kichekesho ni kuwa Polisi wamedhira hata kuongoza barabarani ili watu wajichanganye.
Lakini ajabu wanajiongoza wenyewe, wanajilinda wenyewe na kujiheshimu wenyewe. Hakuna kibaka, hakuna muhuni.
Nimeamini maneno yaliyopata kusemwa hapa kuwa polisi wanapoanzisha purukushani basi huwa ndio waporaji wa pochi za watu, SAA na simu zao kwa kisingizio cha kutuliza ghasia hewa.
Hiyo iko wazi kabsa, angalia upande wa bodaboda toka wakatazwe kuwasumbua hao vijana ajari zimepungua na kwa sasaiv wanabebana 2 na hawana Helment
 
Lakini sahvi si mmeruhusiwa ndio maana hamsumbuliwi.
Kipindi kile ilikuwa nongwa kozi haikuwa wakati wenu, mkulu alikataa.
Hajaruhusiwa mtu hapa. Wanaowatumaga polisi wamegwaya . Katika mapokezi ya Lissu uwanja wa ndege, polisi walizuia. Watu wakakaidi. Polisi wakasalimu amri. Baada ya hapo wakakaa kimya.

Tungekubali "wameruhusu" kama siku hiyo wangesema hivyo na kuwasihi watu wampokee kwa amani. Hapo sasa ungeshuhudia nyomi ya kufa mtu. Hawasemi wameruhusu ili kupunguza idadi. Ni makusudi.
 
Strategy inayotumika kucontain maandamano msimu huu ni kuandamana pamoja na wakereketwa katika muonekano rafiki zaidi(DISGUISE), huo umati unakua na asilimia 30 ya wapiganaji kutoka all-over vikosi vyetu. Hii style wanaitumia Sana kule Hong Kong, tofauti ni kwamba TZ hawako Uniformed.

Nadhani Makamanda kila siku jioni wanagonga glass na kupongezana Kwa LOVELY JOBLY, na Wakereketwa pia wanafurahi wakiandamana bila kuona Magwanda...It is a WIN WIN Situation Kwa Mama Tanzania (in mbatia's voice)
 
Hajaruhusiwa mtu hapa. Wanaowatumaga polisi wamegwaya . Katika mapokezi ya Lissu uwanja wa ndege, polisi walizuia. Watu wakakaidi. Polisi wakasalimu amri. Baada ya hapo wakakaa kimya.

Tungekubali "wameruhusu" kama siku hiyo wangesema hivyo na kuwasihi watu wampokee kwa amani. Hapo sasa ungeshuhudia nyomi ya kufa mtu. Hawasemi wameruhusu ili kupunguza idadi. Ni makusudi.
Acha ubishi. Kwani kipindi kile anazuia mikutano ya kisiasa alisemaje.
Usijitoe ufahamu.
"Hawasemi wameruhusu ili kupunguza idadi. Ni makusudi." Kumbe unachobisha ni nini sasa?
 
Shida bado iko kwa Sirro , kuna kila dalili kwamba kazi imemshinda , tulimsamehe kwa uongo wake wa kuokota gari mitandaoni na kuudanganya umma kwamba ndio lilimteka MO lakini sasa uvumilivu unafika kikomo .
 
Back
Top Bottom