Bahati furaha
JF-Expert Member
- Jul 11, 2012
- 3,077
- 1,439
Ni sahihi sana mkuu.Mkuu sasa unaishije bila kitambulisho?
Kuna mdogo wangu mmoja alikua mgumu kama wewe juu ya kuwa na kitambulisho,siku moja yakamfika,akanipigia nimsaidie some amount,nikamrushia £350 kwa w.union,baada ya nusu saa nikampa MTCN No na Password nikamwambia nenda kachukue,kufika w.union anaambiwa lete kitambukisho cha mpiga kura,passport au driving licence,hakuwa nacho kati ya hivyo,akanipigia nikamwambia sina namna ya kukusaidia na wala siwezi kuivuta irudi ili nikutumie kwa mtu mwingine,nikamwambia wewe tafuta jitambulisho miongoni mwa hivyo kisha nenda kachukue pesa yako.Kwa bahati nzuri miezi miwili baadae kukawa na maboresho ya daftali la wapiga kura,akaenda kuchukua kitambulisho kisha akaenda kuvuta mpunga wake,ingawa cha moto akishakiona!
Sidhani kwa mfano mikoa ya Kigoma, Katavi, Mwanza, Shinyanga na Tabora kwa wanaostahili kuwa na kitambulisho cha mpiga kura walizembea maana bila kitambulisho hupati tiketi ya treni.