Kitambulisho kwenda Zanzibar

Kitambulisho kwenda Zanzibar

Viol

JF-Expert Member
Joined
Dec 15, 2009
Posts
25,419
Reaction score
18,368
Wakuu nipo Zanzibar, ila wadogo zangu wanataka kunitembelea na wapo chini ya miaka 18 hawana vitambulisho vya kupiga kura bara na hawana passport. Nitafanyaje wanitembelee?

Process iwe ndani ya huu mwezi?
 
Wakuu nipo Zanzibar,ila wadogo zangu wanataka kunitembelea na wapo chini ya miaka 18 hawana vitambulisho vya kupiga kura bara,na hawana passport,nitafanyaje wanitembelee???process iwe ndani ya huu mwezi!
Wanatakiwa wapate barua toka kwa serikali ya mtaa walipo, ikionyesha kutambulika kwao kwa majina na umri wao. Barua hizo ziambatishwe na picha zao za Passport size.
Naamini wakifika sehemu ya kukatia ticket hawatosumbuliwa na mtakuwa pamoja Zenji.
 
Hivi huo ujinga wa kwenda Zanzibar na vitambulisho haujafutwa tu?
Mkuu HATA UKITOKA DAR KUJA MWANZA AU MWANZA TO DAR KWA FAST JET.BILA KITAMBULISHO HUINGII NDANI YA NDEGE PAMOJA NA KUWA UMESHAKATA TIKETI.
KITAMBUKISHO NI MUHIMU SAAANA KWAKO WEWE BINAFSI..
LKN TATIZO SISI TUNATAFSIRI TOFAUTI UNAPO OMBWA KITAMBULISHO CHAKO
 
Sio ujinga ni sahihi ki usalama, ili kukitokea ajali ni rahisi kugundua bado nani hajaokolewa na anatokea kata gani. Mbona hata kwenda mwanza au Safari yeyote kwa Ndege ni hivyo hivyo, yani lazima uwe na kitambulisho.
Mkuu WATU WENGINE HAWAJUI NINI MAANA YA KUA NA KITAMBULISHO.AKIOMBWA ATI ANAJISIKIA KAMA KADHALILISHWA.KWELI NCHI HII KAZI IPO.
NDIO MAANA HATA MKUU AMESEMA ANAJUTA HATA KUWA RAIS WA NCHI.
 
Hivi huo ujinga wa kwenda Zanzibar na vitambulisho haujafutwa tu?
Sio Zanzibar tu hata ukikata ticket ya kwenda bara au pwani kwa treni uonyeshe kitambulisho yaani unatoka Mwanza/Kigoma kwenda Dar au Dar kwenda Mwanza/Kigoma kitambulisho lazima
 
Ukifika bandarin unawaambia Sina kuna sehemu unapelekwa palepale kuandikiwa barua .au unaenda na barua Kutoka serikali yakijiji.
 
Hivi huo ujinga wa kwenda Zanzibar na vitambulisho haujafutwa tu?
Sio ujinga kiuhalisia popote utakapokuwepo kitambulisho ni muhimu. Ikibidi hata guest house watu wasipokelewe bila vitambulisho
 
Mkuu HATA UKITOKA DAR KUJA MWANZA AU MWANZA TO DAR KWA FAST JET.BILA KITAMBULISHO HUINGII NDANI YA NDEGE PAMOJA NA KUWA UMESHAKATA TIKETI.
KITAMBUKISHO NI MUHIMU SAAANA KWAKO WEWE BINAFSI..
LKN TATIZO SISI TUNATAFSIRI TOFAUTI UNAPO OMBWA KITAMBULISHO CHAKO
Ushasema ndege.kama kuna muhalifu si anapanda basi tu
 
Mkuu hii ni kwa ajiri ya kuweka record endapo itatokea ajali wajue ni abiria gani waliokua kwenye chombo husika.
Tatizo kama hauna si watakuzuia ndo sisi tunachopinga.ina maana kama hauna kitambulisho hauingii Zanzibar?
 
Sio ujinga ni sahihi ki usalama, ili kukitokea ajali ni rahisi kugundua bado nani hajaokolewa na anatokea kata gani. Mbona hata kwenda mwanza au Safari yeyote kwa Ndege ni hivyo hivyo, yani lazima uwe na kitambulisho.
Mimi kitambulisho sina INA maana siruhusiwi kuingia Zanzibar?
 
Sio ujinga ni sahihi ki usalama, ili kukitokea ajali ni rahisi kugundua bado nani hajaokolewa na anatokea kata gani. Mbona hata kwenda mwanza au Safari yeyote kwa Ndege ni hivyo hivyo, yani lazima uwe na kitambulisho.
Hujaelewa (au hujui) na umejibu kutokana na usafiri.

Kitambulisho siyo kwenye boti asee, hii kitu ni pale unapofika kuna ofc ya uhamiaji ndiyo wanaofuatlia hiyo kitu.
 
Wakuu nipo Zanzibar,ila wadogo zangu wanataka kunitembelea na wapo chini ya miaka 18 hawana vitambulisho vya kupiga kura bara,na hawana passport,nitafanyaje wanitembelee???process iwe ndani ya huu mwezi!
Cheti cha kuzaliwa kinatosha.
Zanzibar kwasababu watalii ni wengi ndio maana wanatumia mfumo huo
 
Tatizo kama hauna si watakuzuia ndo sisi tunachopinga.ina maana kama hauna kitambulisho hauingii Zanzibar?
Kitambulisho ni document yenye kukutambulisha wewe, kutokana na usafiri wa ndege au meli hutumika sana kwa sababu zilizowekwa na mamlaka husika, kama Zanzibar watu wangekuwa wanakwenda kwa basi naona vitambulisho visingetumika. SUMATRA waliikazia nidhamu ya kuonyesha kitambulisho pindi unaposafiri kutokana na ajali za baharini zinapotokea inakuwa vigumu kutambua waliyopata ajali wakina nani ikiwa hawajaorodheshwa na kampuni husika, vile vile na kwa ajili ya usalama pia kujua nani kaenda Zanzibar na nani katoka Zanzibar kaenda Dar. Tujaribu kuheshimu taratibu zilizowekwa na mamlaka husika ni kwa ajili ya manufaa yetu.
 
Back
Top Bottom