Kitambulisho cha NIDA si kigezo cha uraia - Waziri

Analogia Malenga

JF-Expert Member
Feb 24, 2012
5,037
9,927
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe. George Simbachawene, amesema kuwa mwananchi kuwa na kutambulisho cha NIDA haina maana kwamba hicho ndicho kinachoonesha uhalali wa uraia wake kwani vitambulisho hivyo hata wananchi wasiowazawa wa Tanzania wanavyo.

SIMBAA%20WEB.jpg

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe. George Simbachawene

Waziri Simbachawene ameitoa kauli hiyo Bungeni Dodoma hii leo Juni 4, 2021, ambapo ameongeza kuwa hata yeye licha ya kwamba anatokea Dodoma ikitokea kuna wasiwasi kidogo juu ya uraia wake lazima atahojiwa juu ya uhalali wa uraia wake.

"Kupewa kitambulisho cha uraia wa Tanzania (NIDA) siyo mwarobaini kwamba wewe hauwezi ukaulizwa kuhusu uhalali na uhalisia wa uraia wako, vitambulisho hivi hata wakazi wasio raia wanavyo, hata mimi ninaweza nikaulizwa uraia na uhalisia wangu endapo utajitokeza wasiwasi wowote," amesema Waziri Simbachawene.
 
Yaani ukiniuliza kwanini serikali ilifakamia hili suala la vitambulisho vya uraia napata 0
 
Nchi yetu hii kila kikicha kunakuja mihemko ya ajabu,Pls my minister why nchi imetumia fedha yangu(kodi)kuja na ID ambayo ni useless?

Why my minister unanifanyia hivi? Why my minister huji na utaratibu huu, wakati mtoto anazaliwa mzazi au wazazi wanampatia jina ili wamtambue na jina hili atadumu nalo na kufa nalo sasa kwa nini serikali yetu isifanye the same?

Mtoto akizaliwa tu lazima apewe ID number(ndio jina lake)na serikali imtambue ikiwa ni pamoja na kuwa ndani ya central data system's ya nchi, ID hii itaishi nayo na kufa nayo, tumechelewa mno but my minister you can definitely do better than this, wake up na acha porojo suala hili nyeti la uraia.
 
Nimekuelewa vizuri sana kuwa pamoja na kuwa na kitambulisho cha NIDA bado selikari inayo nafasi ya Kuweza kunihoji endapo itakuwa na wasiwasi juu ya Uraia wangu.

Ahsante sana waziri yupo sahihi. Maana wapo watu wanauraia wa Nchi mbili hivyo sio rahisi kuweza kuwatambua. Sawa sawa
 
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe. George Simbachawene, amesema kuwa mwananchi kuwa na kutambulisho cha NIDA haina maana kwamba hicho ndicho kinachoonesha uhalali wa uraia wake kwani vitambulisho hivyo hata wananchi wasiowazawa wa Tanzania wanavyo.

SIMBAA%20WEB.jpg

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe. George Simbachawene

Waziri Simbachawene ameitoa kauli hiyo Bungeni Dodoma hii leo Juni 4, 2021, ambapo ameongeza kuwa hata yeye licha ya kwamba anatokea Dodoma ikitokea kuna wasiwasi kidogo juu ya uraia wake lazima atahojiwa juu ya uhalali wa uraia wake.

"Kupewa kitambulisho cha uraia wa Tanzania (NIDA) siyo mwarobaini kwamba wewe hauwezi ukaulizwa kuhusu uhalali na uhalisia wa uraia wako, vitambulisho hivi hata wakazi wasio raia wanavyo, hata mimi ninaweza nikaulizwa uraia na uhalisia wangu endapo utajitokeza wasiwasi wowote," amesema Waziri Simbachawene.
Daah aisee 🤔🤔🤔, sasa kumbe bado havina mantiki yoyote? Ok well, tuletewe sasa vitambulisho ambavyo vitakua vikiaminiwa juu ya uraia wetu halali kbs.
 
Kuna makosa mawili yalifanyika baada ya kupata uhuru wa nchi hii na hayajarekebishwa hadi leo.

1. Kutotoa tafsiri rasmi ya nani ni mtanzania iwe kwa chimbuko lake au kwa kulowea, kuanzia nchi ilipopata Mamlaka ya kuwa nchi huru, kutambulika kisheria na kupewa hati ya uraia.

2. Kutotambua makazi ya kila raia na mali zake ikiwemo ardhi waliyorithi kutoka kwa watangulizi wao, kuipima na kummilikisha kila raia aliyetambuliwa kisheria na kupewa hati ya umiliki.

Haya mambo mawili makuu hayakuwahi kufanyika yakimlenga raia wa nchi hii, badala yake Serikali ilijikita katika kutambua na kujimilikisha ardhi ya maeneo yote ya majimbo mikoa na wilaya ambayo yenyewe yako rasmi na kisheria.

Jukumu la kuwatambua raia, chimbuko lao na urithi na tamaduni zao lilitwikwa kwenye mabega ya taasisi za kidini na hasa dini katoliki na baadaye protestants. Hawa ndio walikuwa watu makini nadhani hadi leo kuliko hata Serikali ya leo, waliweza kutoa na kuweka kumbukumbu ya vyeti vya kuzaliwa, ubatizo, ndoa, vifo na kutambua nani ni raia wa eneo fulani na nani ni mgeni.

Vyeti vya RITA, NIDA, Hati za kusafiria, Vyeti vya kupiga kura na kadhalika, vinavyotolewa sasa ni usanii mtupu unaotumia pesa nyingi bila kuwa na manufaa yoyote. Sishangai kumsikia Simbachawene mwenye Mamlaka ya wizara ya ulinzi was raia akikiri hadharani mapungufu ya kazi anahitajika kuifanya kwa ufanisi.

Nini kifanyike... 1.kutoa tafsiri ya nani ni mtanzania kwa vigezo vipi na hadhi ipi, kumuandikisha kwenye Mamlaka maalumu, na hapa napendekeza Tume ya taifa ya uchaguzi ikishirikiana na Tamisemi ifanye kazi hii na ikikamilisha kazi watu wapewe hati ya uraia kwa kuapa kama ilivyo kwenye mahafari vyuoni.
2. Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania atangaze kuwa mtu yeyote atakayekuwa ndani ya mipaka ya Tanzania mfano kuanzia tarehe 30/06/2021 ni mtanzania kama atathibitisha asili yake na kupewa hati ya uraia, asiyetaka atambulike kama mgeni....na mgeni anayeipenda Tanzania apewe uraia hata Bure!!! ... Kuanzia hapo vyeti vya kuzaliwa vichukue mkondo wake. 3. Ardhi yote iliyoko kwenye Mamlaka za vijiji na Manispaa za wilaya, ipimwe na wananchi wamilikishwe na wapewe hati maana kimsingi huo ndio urithi wao. Kwa kufanya hayo tutakuwa tumeanza rasmi kujenga jamii ya kitanzania kwenye msingi imara, kwa sasa naona usanii tu.
 
Kuna makosa mawili yalifanyika baada ya kupata uhuru wa nchi hii na hayajarekebishwa hadi leo.

1. Kutotoa tafsiri rasmi ya nani ni mtanzania iwe kwa chimbuko lake au kwa kulowea, kuanzia nchi ilipopata Mamlaka ya kuwa nchi huru, kutambulika kisheria na kupewa hati ya uraia.

2. Kutotambua makazi ya kila raia na mali zake ikiwemo ardhi waliyorithi kutoka kwa watangulizi wao, kuipima na kummilikisha kila raia aliyetambuliwa kisheria na kupewa hati ya umiliki.

Haya mambo mawili makuu hayakuwahi kufanyika yakimlenga raia wa nchi hii, badala yake Serikali ilijikita katika kutambua na kujimilikisha ardhi ya maeneo yote ya majimbo mikoa na wilaya ambayo yenyewe yako rasmi na kisheria.

Jukumu la kuwatambua raia, chimbuko lao na urithi na tamaduni zao lilitwikwa kwenye mabega ya taasisi za kidini na hasa dini katoliki na baadaye protestants. Hawa ndio walikuwa watu makini nadhani hadi leo kuliko hata Serikali ya leo, waliweza kutoa na kuweka kumbukumbu ya vyeti vya kuzaliwa, ubatizo, ndoa, vifo na kutambua nani ni raia wa eneo fulani na nani ni mgeni.

Vyeti vya RITA, NIDA, Hati za kusafiria, Vyeti vya kupiga kura na kadhalika, vinavyotolewa sasa ni usanii mtupu unaotumia pesa nyingi bila kuwa na manufaa yoyote. Sishangai kumsikia Simbachawene mwenye Mamlaka ya wizara ya ulinzi was raia akikiri hadharani mapungufu ya kazi anahitajika kuifanya kwa ufanisi.

Nini kifanyike... 1.kutoa tafsiri ya nani ni mtanzania kwa vigezo vipi na hadhi ipi, kumuandikisha kwenye Mamlaka maalumu, na hapa napendekeza Tume ya taifa ya uchaguzi ikishirikiana na Tamisemi ifanye kazi hii na ikikamilisha kazi watu wapewe hati ya uraia kama ilivyo kwenye mahafari vyuoni.
2. Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania atangaze kuwa mtu yeyote atakayekuwa ndani ya mipaka ya Tanzania mfano kuanzia mfano tarehe 30/06/2021 ni mtanzania kama atathibitisha asili yake na kupewa hati, asiyetaka atambulike kama mgeni....na mgeni anayeipenda Tanzania apewe uraia hata Bure!!! ... Kuanzia hapo vyeti vya kuzaliwa vichukue mkondo wake. 3. Ardhi yote iliyoko kwenye Mamlaka za vijiji na Manispaa za wilaya, ipimwe na wananchi wamilikishwe na wapewe hati maana kimsingi huo ndio urithi wao. Kwa kufanya hayo tutakuwa tumeanza rasmi kujenga jamii ya kitanzania kwenye msingi imara, kwa sasa naona usanii tu.
Kaka nashukuru kwa kuwasilisha mawazo yangu pia
 
Kaka nashukuru kwa kuwasilisha mawazo yangu pia
Pamoja sana mkuu, hakuna njia ya mkato hasa unapojenga nyumba ya kukaa miaka zaidi ya mia. Nyumba imara hujengwa juu ya msingi imara, bila kufuata kanuni hizi hatupaswi kuzishangaa nyufa. Hapa ndipo huko uhamiaji kila aliyepewa mamlaka ana vigezo vyake.
 
Back
Top Bottom