ZENJIBARIA
JF-Expert Member
- Feb 26, 2014
- 677
- 1,645
ZENJIBARIA
kuna mdau
humu
nilishawahi
kuchati nae
na nilikuwa
sifahamu kama yupo
nchi za nje
ktk
mazungumzo
yetu
niligundua we are different
in time
(alinambia
kule ilikuwa
imefika usiku
so alikuwa anataka
kulala) yani
huku ilikuwa
mchana kule
usiku
unalizungumz iaje hili..?
na kuhusu
hiyo allien
belt
unazungumzi
a viumbe allien ama..? na kwanini watudanganye wanafanya hivyo kwa manufaa yapi..?
van allen belt ni ukanda wa magnetic field ambao upo juu umeizunguka dunia kwa maelezo yao, inaitwa belt kwa sifa hio ya ukanda uliozunguka dunia,
na kuhusu tafautiana time ya sehemu moja na nyengine hii ni subject yake peke yake ili uweze kuifahamu, cha kwanza kuelewa ni time ni nini hasa,whats is time exactly? time inasababishwa na nini,
kwa mitazamo yetu ya haraka tunapima time kwa kutumia jua linapochomoza na kutua na vile vile kisasa tunatumia saa
lakini jua linazama vipi na linachomoza vipi wakati dunia sio duara,wakati ikiwa hatulioni unapokuja usiku jua linakwenda wapi,hii kwanza tufahamu kuzama na kuchomoza kwa jua katika kila eneo,manake kila eneo lina time zake za kuzama na kuchomoza kwa jua.
kujua jua linachomoza vipi pasipokuwa na duara la dunia ni lazima ufahamu law of perspective, uwezo wetu wa kuona yaani vipi macho yetu yanaona
itazame hii picha ya chini hapo ichukulie wewe umesimama hapo mwanzo wa picha kisha unaangalia mwisho wa hii koridoo
kama utachunguza utaona sakafu inapanda na dari inashuka na kuta za pembeni zinajikunja kuja katu kadri ya koridoo inavozidi,mwisho wa koridoo hii kunakuwa kudogo sana yaani kumejikunja na hapa mwanzo pako kama kawaida,ki uhalisia hii koridoo iko sawa kuanzia mwanzo hapa mpaka mwsho kule yote ipo sawa lakini macho yetu ndio yanaona namna hii mwisho wa upeo wako kunakua kudogo mpaka kunatoweka kabisa
ichukulie hizo taa za juu hapo kama ndio jua linasafiri angani kwa namna unavyoliona wewe na macho yako,jua litakwenda mpaka mwisho wa upeo wako kwa hapa litazame linavyoshuka kuifata koridoo jua litaonekana kama linazama lakini kiuhalisia halizami ila linatoweka kwenye upeo wa macho yako tu kama huo mfano wa taa na hii koridoo,hivi ndio tunavyoona jua linazama au kuchomoza na tukazani linakwenda chini ya duara la dunia lakini uhalisi ni kuwa linazunguka juu ya uso wa dunia na sio kwenda chini
mzunguko huu wa jua juu ya uso wa dunia ndio unaosababisha time za kila maeneo kuwa tafauti baina ya maeneo kwa vile linapotoweka kwenye eneo letu tunapata magharibi na usiku kuingia na jua linaanza kuonekana kwenye maeneo mengine na hapo ndio wanapata alfajiri yao na mchana kenedelea kwa muangaza wa jua