Kitambue chombo VOYAGER 1

KENZY

JF-Expert Member
Dec 27, 2015
26,213
56,849
766px-Voyager.jpg

Ni chombo cha kisayansi kilichorushwa na shirika la maswala ya anga NASA mwaka 1977,kusudi la kurushwa chombo hiki ni kwaajili ya kupeleleza anga ndani na nje ya mfumo wetu wa jua.

Voyager 1 mpaka sasa kiko umbali wa kilometa billion 18.35 kutoka duniani,mwaka 2012 chombo hicho kilipita mzingo wa pluto ambapo ndo kunaaminika ndio mwisho wa mfumo wa solar system yetu,kwamaana hiyo kipo nje ya mfumo wa jua letu!

Pia mwanga wa jua unahitaji zaidi ya masaa 17 kufikia chombo hicho ambapo umbali toka jua mpaka ilipo voyager ni km billion 19 na kitu.
Kifaa hiki kinatumia madini ya uranium kujizalishia umeme ili kiweze kujiendesha na itakapofika mwaka 2020 madini hayo yanatarajiwa kuisha hivyo kitastop na itakuwa ndo mwisho wake wa kufanya kazi!

Lakini pia kifaa hicho kimeekewa DNA za binadamu endapo ikitokea viumbe wengine kukipata wanaweza gundua kuwa kuna viumbe wengine mahala fulani.

hiyo ndo voyager 1 unaweza ongezea
 
Dunia yetu ina mengi
ni kweli na hayo mengi yapo kwenye bongo zetu
Mwaka 77 wakati huku sisi tuna hangaika na chama wenzetu wanawaza kuishi huko du
ha ha! ndio maana majamaa yametutangulia sana tu wkt sisi tunahangaika na njaa,vita,ukeketaji,umaskini n.k wenyewe wanawaza mbali mno they will continue to be number one!
 
Baada ya siku 16 kupita baada ya kurushwa voyager 1 ilirushwa nyingine hii ni Voyager 2 Lengo la hizi Space vehicles mbili ilikuwa ni kuchunguza sayari mbili Yani Jupiter na Saturn haswa Mwezi mkubwa unao orbit saturn uitwao Titan, Zilivomaliza mission hizo Ndio zikapanua wigo na kujogengea anga za mbali, Vifaa hivi bado vinatuletea Feedback kupitia Deep space Network
 
Baada ya uranium kwisha naamini hakitoweza kubaki tena huko kwa maana kitarudi chini...jee hakitoweza kuleta athari kwa binadamu? Au mwisho wake utakuwaje?
Hicho chombo hakiwezi kuangukia dunia kabisa kumbuka kimeshatoka kabisa katika solar yetu yenye sayari 8 au 9 ukiweka dwarf planet Pluto, Hicho kinatuvutwa katika Object nyingine na incase kime maintain speed kita orbit, Hio energy inayodaiwa kuwa itaisha 2025 ni Power kwa ajili ya kurun transponders Zinazowasiliana na Deep Space Network (DSN) Chombo still kitakuwa active
 
Hicho chombo hakiwezi kuangukia dunia kabisa kumbuka kimeshatoka kabisa katika solar yetu yenye sayari 8 au 9 ukiweka dwarf planet Pluto, Hicho kinatuvutwa katika Object nyingine na incase kime maintain speed kita orbit, Hio energy inayodaiwa kuwa itaisha 2025 ni Power kwa ajili ya kurun transponders Zinazowasiliana na Deep Space Network (DSN) Chombo still kitakuwa active
Nimekuelewa mkuu....
 
Kwahiyo kitarudi duniani mwaka gani? Au ndo kimeenda moja kwa moja? Halafu kimeleta taarifa gani tangu kimerushwa huko?
ndo moja kwa moja hiyo.
kuhusu taarifa kabla ya kutoka kwenye solar system kilipita ktk baadhi ya sayari na kugundua gases mbalimbali zinazopatikana ktk angahewa za sayari hizo,pia kwa pamoja vayager 1 and 2 vimeweza kubaini miezi takriban 23 inayopatikana ktk sayari nyengine,kiliweza kugundua uwepo wa volcano ktk mwezi uitwao Io huu ni mwezi wa jupiter mkuu hayo ni baadhi nayoyafahamu mengine ni ktk mwaka 1990 kamera za voyager 1 zilizima ili kubalance moto.. pia inapotuma taarifa mpk kufika hapa duniani huchukua masaa 19 due to distance i mean kadri inavyozidi kusonga mbele ndivyo masaa ya uchelewaji wa taarifa unavyozidi!
 
sawa
Hicho chombo hakiwezi kuangukia dunia kabisa kumbuka kimeshatoka kabisa katika solar yetu yenye sayari 8 au 9 ukiweka dwarf planet Pluto, Hicho kinatuvutwa katika Object nyingine na incase kime maintain speed kita orbit, Hio energy inayodaiwa kuwa itaisha 2025 ni Power kwa ajili ya kurun transponders Zinazowasiliana na Deep Space Network (DSN) Chombo still kitakuwa active
 
golden_record_cover_sm.jpg

The golden record
hiki ni ki plate maalum ambacho kipo kwenye voyager ndio kina taarifa juu ya uwepo wetu means kina show direction ya wapi sisi tupo,nini kinafanyika duniani na kina sauti mbalimbali za wanyama,upepo n.k pia kina picha na maelekezo ya namna ya kuplay hizo sauti na salamu za lugha zipatazo 55 za zamani na sasa ktk maeneo tofauti tofauti.
ukitaka kujua mengi google utajua kuhusu kifaa hicho hapa me nimedodosadodosa tu.
 
hakuna voyager wala hakuna space exploration hizi zote ni propanganda za uongo mtupu,yote haya ni makatuni ya kuchora,picha zote za space sio za kweli na picha za dunia zote zilizo online zote ni uongo mtupu zote za kuchora hakuna picha ya dunia iliyo kweli,tunavyosomeshwa ni propaganda tu hali halisi ya dunia ilivyo haijasemwa ndio maana tunaaminishwa hizi fantasy
 
hakuna voyager wala hakuna space exploration hizi zote ni propanganda za uongo mtupu,yote haya ni makatuni ya kuchora,picha zote za space sio za kweli na picha za dunia zote zilizo online zote ni uongo mtupu zote za kuchora hakuna picha ya dunia iliyo kweli,tunavyosomeshwa ni propaganda tu hali halisi ya dunia ilivyo haijasemwa ndio maana tunaaminishwa hizi fantasy
Ebanah eheeee
 
hakuna voyager wala hakuna space exploration hizi zote ni propanganda za uongo mtupu,yote haya ni makatuni ya kuchora,picha zote za space sio za kweli na picha za dunia zote zilizo online zote ni uongo mtupu zote za kuchora hakuna picha ya dunia iliyo kweli,tunavyosomeshwa ni propaganda tu hali halisi ya dunia ilivyo haijasemwa ndio maana tunaaminishwa hizi fantasy
hebu tueleze ukweli wako mkuu
 
hebu tueleze ukweli wako mkuu

kuna mambo mengi sana ya kuangalia ambayo yatakuonesha kuwa elimu yote ya space na uhalisi wa dunia ilivyo ni uongo

- wanasema dunia ipo duara kama chungwa lakini ndege zikiruka hazizunguki chungwa zinafika angani zinaweka cruising speed na zinakwenda straight hazilazi pua chini au juu kulizunguka chungwa ambayo ndio shepu ya dunia
-wanasema dunia ni shape ya chungwa kwa hio kila pahala patakuwa na mpindo ili kupata shepu ya chungwa kwa maana hio ukiwa dar zanzibar huwezi kuiona popote kwa maana itakuwa upande wa pili wa mpindo wa dunia na hii zipo formula zake ambayo kwa masafa ya dar to znz ni kama 44km mpindo wa maji ulikuwa uwe kama ulikuwa uwe atleast 60m
-pia hivi majuzi wamesema wanajiandaa ili waweze kutoka kwenye low-earth orbit na waweze kupeleka watu outer sapce wakati mwanzo wamesema washapeleka watu kwenye mwezi ambayo upo beyond low earth orbit.

-sifa moja kuu ya maji popote yalipo ni lazima yawe level,maji hayawezi kupinda kufanya duara,kwa hio hilo duara la dunia maji yanapinda vipi kuweka shepu ya duara,maji ni lazima yatafute level kwa namna yeyote ile,

gravity ni uzushi ,kama gravity ndio inayozuia vitu hapa duniani iweje ndege iliyo ndogo na nyepesi iweze kuishinda gravity na iruke wakati bahari iliyo kubwa sana nzito kuliko kitu chochote hapa duniani isiweze kuishinda gravity'
au kwanini gravity iruhusu mabofu yende angani wakati vitu vizito zaidi vipeshikwa na gravity


ki uhalisia hakuna aliyewahi kufika mwezini na mwezi haupo na ardhi kama ilivyo hapa duniani,sayari zote picha tunazoziona online sio halisi ni michoro tu, picha halisi hazipo clear kama wanavyoonesha hio michoro

mambo ni mengi sana ntarudia tena mengine
 
hakuna voyager wala hakuna space exploration hizi zote ni propanganda za uongo mtupu,yote haya ni makatuni ya kuchora,picha zote za space sio za kweli na picha za dunia zote zilizo online zote ni uongo mtupu zote za kuchora hakuna picha ya dunia iliyo kweli,tunavyosomeshwa ni propaganda tu hali halisi ya dunia ilivyo haijasemwa ndio maana tunaaminishwa hizi fantasy
Wanazi huwa hamkosekani ha ha ha hah ha ha
 
hakuna voyager wala hakuna space exploration hizi zote ni propanganda za uongo mtupu,yote haya ni makatuni ya kuchora,picha zote za space sio za kweli na picha za dunia zote zilizo online zote ni uongo mtupu zote za kuchora hakuna picha ya dunia iliyo kweli,tunavyosomeshwa ni propaganda tu hali halisi ya dunia ilivyo haijasemwa ndio maana tunaaminishwa hizi fantasy
Sasa hebu wewe tupe yako ambayo unahisi ndio sahihi sio propoganda!!!
 
Back
Top Bottom