Kitambi unanitaka nini mimi masikini wa watu

Kitambi unanitaka nini mimi masikini wa watu

Kitambi aka friji kinaninyemelea na umasikini wangu huu
Ndo kabisa nishapa gundu na sijui nitatoboaje, vipesa kidogo tu kitambo kinanisonga

Bilgate hana kitambi

Elon musk hana kitambi

Aliko Dangote hana kitambi

Bakhresa hana kitambi

Mo Dewj hana kitambi

GSM hana Kitambi

Rostam hana kitambi

Alibaba hana kitambi

Mesi hana kitambi

Ronaldo hana kitambi

Jayz hana kitambi

Rais Samia hana kitambi

Kikwete hana kitambi

Diamond platinum hana kitambi

King Kiba hana kitambi

Obama hana kitambi

Naona kitambi ni ishara ya ujinga na umasikini
Mora niokoe na hili friji tumboni
Kitambi ni matokeo ya lishe mbovu.
Usile kujaza tumbo, kula virutubisho na mlo kamili kidogo kidogo. Wengi tunakula kama hatuna uhakika wa kipa tena. Sasa kwanini usivimbe???
 
Bora nyie mna kitambi mwenzenu hii ni mimba ya miezi tisa .
Nikajaribu hata kujipigisha tumazoezi na wana mtaa wanaishia kunikimbia maana ni mwendo wa kuwatolea hewa za ghafla.
Ila insh'Allah labda huu mwezi mtukufu hii mimba itaondoka.
 
Janabi Muhimbili hana kitambi.
downloadfile-81.jpg
downloadfile-140.jpg
 
Mh:Tulia Ackson hana Kitambi na amesema,,,wala hatarajii kamwe kuja kuwa na kitambi Kwa maana majukumu yameongezeka na ni mengi
 
Acha kufakamia ma vyakula kula kwa ratiba na pia changanya matunda kwenye diet yako, punguza mafuta, pia fanya mazoezi angalau mara 3 kwa wiki.
Nimekuelewa sana mkuu
 
Kwa mswahili kitambi kina heshima yake. Nakupa tu tahadhari kuwa kwenye michango ya aina yoyote utapewa kiti cha heshima wakitegemea mchango mkubwa kwako. Kumbe ni kitambi cha maharage, matembele na dona.
 
Acha kula usiku wa manane ma wanga...
Yani usile muda umeenda sana hasa wanga...
 
Back
Top Bottom