Lycaon pictus
JF-Expert Member
- Jan 31, 2021
- 10,884
- 18,824
Spoiler Alert.
Mwaka 1975-1979 dunia ilishuhudia ukichaa wa ajabu kabisa. Wakomunisti wa Cambodia(Khmer Rouge) walishika nchi. Kwanza wakapiga marufuku matumizi ya pesa kisha wakafurusha wakazi wote kutoka mjini, wakazi wa mji mkuu Phnom Penh, kama 2.5m walifukuzwa wote na kuambiwa waelekee vijijini. Walikataza kuvaa nguo za rangi, wote walitakiwa kuvaa suruali na shati jeusi.
Wakaanza kusafisha jamii kama cultural revolution ya Mao. Watu wote waliosoma, wanaovaa miwani! Madaktari na mainjinia waliuawa. Walitaka kujenga jamii safi ya wakulima.
Nchi haikuwa na madawa watu walikufa kama kuku. Pia Ili kupata silaha walichukua Mchele na kupeleka China na wao kupata silaha. Njaa ilienea watu wakapata utapiamlo huku wakila vyura, panzi, minyoo, mijusi na wadudu wengine. Ndani ya miaka minne watu karibu 2m walikufa, kwenye nchi ya watu 8m! "Wakomunisti" ni watu wa hovyo sana.
Mwaka 1975-1979 dunia ilishuhudia ukichaa wa ajabu kabisa. Wakomunisti wa Cambodia(Khmer Rouge) walishika nchi. Kwanza wakapiga marufuku matumizi ya pesa kisha wakafurusha wakazi wote kutoka mjini, wakazi wa mji mkuu Phnom Penh, kama 2.5m walifukuzwa wote na kuambiwa waelekee vijijini. Walikataza kuvaa nguo za rangi, wote walitakiwa kuvaa suruali na shati jeusi.
Wakaanza kusafisha jamii kama cultural revolution ya Mao. Watu wote waliosoma, wanaovaa miwani! Madaktari na mainjinia waliuawa. Walitaka kujenga jamii safi ya wakulima.
Nchi haikuwa na madawa watu walikufa kama kuku. Pia Ili kupata silaha walichukua Mchele na kupeleka China na wao kupata silaha. Njaa ilienea watu wakapata utapiamlo huku wakila vyura, panzi, minyoo, mijusi na wadudu wengine. Ndani ya miaka minne watu karibu 2m walikufa, kwenye nchi ya watu 8m! "Wakomunisti" ni watu wa hovyo sana.