Kiswahili ni Kiingereza, jadili.

zubek

Member
Sep 9, 2017
7
5
Habari za muda ndugu, jamaa na marafiki? Mada tajwa ni swali tosha kuwakamata kidato cha nne, cha sita na hata wanazuoni ambao wamewekeza katika elimu, hususan lugha ya kiswahili. NECTA, TUKI pamoja na vitivo mbalimbali katika vyuo vikuu hapa nchini, mtaala na vitabu kadha wa kadha, tumezoea kukutana na maswali kama vile:
1. Kiswahili ni kiarabu, jadili.
2. Kiswahili ni kibantu, jadili. N.k.
Sasa leo tujadili hili, je, kiswahili ni kiingereza? Au la?
>>>> Kwa upande wangu, kuna maneno mengi saaana ya kiingereza ambayo tunayatumia katika lugha ya kiswahili, hasa katika nyakati hizi za utandawazi na maendeleo ya kisayansi na kiteknolojia, misamiati mingi tunayakopi na kuyapesti kama yalivyo, ukiangalia hata hapo nimechanganya tayari. Maswali ya kuzingatia misamiati, hata kiarabu tunatazama uwingi wa maneno ya lugha hiyo katika lugha ya kiswahili na kukuta maneno meeeengi, tunayatumia bila shida na tumezoea.
Swali: lugha moja yaweza kuwa nyingine kwa kigezo cha mfanano wa kimsamiati? Au uwingi wa matumizi wa misamiati ya lugha moja katika lugha nyingine yaweza kusababisha lugha hiyo kuwa nyingine ???.
Ubantu na kiswahili, je, ni uchambuzi wa kipragmatikia, kisemantikia, kisintaksia, kifonolojia au kimofolojia unaotumika kusema kiswahili ni kibantu? angalieni hata misamiati niliyotumia hapo juu na matumizi yake katika pande zote mbili, je, kiswahili ni kiingereza ???
…… Tunatumia saaana maneno ya kiingereza kwenye kiswahili, tofauti na hali ilivyo kwa upande wa kiingereza, wao hawatohoi au kukopa kiasi hicho, ni maneno machache tu, na hii ni kwa sababu lugha ni sehemu muhimu ya utamaduni, hivyo utamaduni wa afrika mashariki ni tofauti na utamaduni wa mwingereza na ulaya kwa ujumla. Hivyo wazungu wanapokuja huku, wanajaribu kutohoa maneno na kuyatumia muda mwingune jinsi yalivyo iki maana isipotoshwe, kama tu hakuna namna ya kuunda msamiati mpya kwa lugha yao. Sasa sisi ambao hata hatutembelei saana kwao, kujua utamaduni wao ambao sehemu nyingine tunashea tu, imekuwa tatizo mpaka siku hizi mashuleni na vyuoni, walimu na wanafunzi ni full kiswanglish, mchanganyiko mpaka daaaa! Hata mjengoni huwa nasikia wakichanganya...je? Kiswahili ni kiingereza?
 
kwa mantiki ya "kutohoa" naweza sema kiswahili ni kiingereza,kwani kimetohoa baadhi ya maneno kutoka ktk lugha ya kiingereza na kuyafanya yatumike ktk kiswahili mf: t-shirt kwa kiswahili ni tisheti,comedy kwa kiswahili ni komedi,number kwa kiswahili ni namba..:D sikwenda shule kusoma nilienda kuelimika leta tiki yangu:D
 
NECTA=BAMITA

Ni kweli kuwa Kiswahili ni Kiingereza kwa jina lakini ni Kibantu kwa asili.
 
kwa mantiki ya "kutohoa" naweza sema kiswahili ni kiingereza,kwani kimetohoa baadhi ya maneno kutoka ktk lugha ya kiingereza na kuyafanya yatumike ktk kiswahili mf: t-shirt kwa kiswahili ni tisheti,comedy kwa kiswahili ni komedi,number kwa kiswahili ni namba..:D sikwenda shule kusoma nilienda kuelimika leta tiki yangu:D
Mkuu hayo maneno yanakiswahili chake kabisa tena kinaeleweka sehemu yoyote ukizungumza kwa mfano t-shirt = fulana na comedy = mahoka( hapa naweza kusahihishwa )

Ila bado kuna maneno mengi kweli tumetohoa kutoka kwenye kizungu. Nitarudi baadae
 
Ni lugha ambayo imekosa kuwa na herufi zake zenyewe. Hizi herufi zote tunazozitumia katika kuumba maneno ya kiswahili tumechukua kwa wazungu (a,b,c,d,e... na a, e, i, o, u). Ikasababisha baadhi ya maneno tuyatohoe kutoka kwenye lugha ya kiingereza kwasababu tulikuwa bado hatujajiandaa kimisamiati. Huwa nawaza kama wazungu wasingekuja nadhani Kiswahili kingeandikwa tofauti na kinavyoandikwa leo. Ila Kiswahili sio Kingereza
 
Kiswahili si kingereza. Hoja ya kukopa na kutohoa misamiati kutoka lugha ya kingereza hakutoshi kukifanya kiswahili kuwa ni kiingereza.

Zipo sababu zingine kadhaa kama muundo wa sentensi katika lugha. Ukizama kwa undani utakuja kuona muundo wa sentensi katika lugha ya kiswahili na kingereza ni tofauti.

Lingine ni kwamba sisi waswahili tumeathiriwa tu na lugha hiyo na si kila maneno unayoyasikia tunayatohoa kutoka kwenye kingereza ni sahihi kwenye kiswahili.
Umetoa mfano wa neno tisheti kiswahili sahihi cha neno hiLo kama sikosei ni fulana. Yapo maneno mengi kama juisi, kompyuta nk ambayo Yapo kwa lugha za kiswahili lakin hatuyajui na hatuyatumii.

Wacha wataalamu waeleze zaidi mimi nimetumia elimu ya kidato cha tatu kwenye mada ya historia ya lugha.
 
Back
Top Bottom